• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

KETE MUHIMU KWA TAIFA STARS AFCON

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 27, 2025
in Burudani, Kimataifa, Michezo
0
KETE MUHIMU KWA TAIFA STARS AFCON
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na AMINA KASHEBA

KETE muhimu iliyobeba matumaini makubwa kwa timu ya taifa ‘Taifa Stars’ kupata ushindi wake wa kwanza katika historia ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON), itasukumwa leo wakati miamba hiyo itakapochuana na Uganda ‘The Cranes’.

Mtanange huo wa dabi ya Afrika Mashariki utapigwa saa 2:30 usiku katika Uwanja wa Al Medina uliopo Rabat, Morocco.

Timu hizo kutoka ukanda wa CECAFA zitachuana katika mchezo wa kundi C wa AFCON 2025, baada ya awali kila moja kuanza kwa kichapo.

Katika michuano hiyo, Tanzania ilianza kwa kichapo cha mabao 2-1 dhidi ya Nigeria wakati Uganda ikipigwa mabao 3-1 dhidi ya Tunisia.

Ili kufufua matumaini yake ya kutinga mtoano na kuweka rekodi ya kupata ushindi wake wa kwanza, Stars inapaswa kuifunga Uganda leo. 

Katika michuano hiyo ya nne kwa Tanzania kushiriki, miamba hiyo haijawahi kushinda hata mechi moja kati ya mechi 10 ilizocheza katika AFCON, ikitoka sare mara tatu na kufungwa mara saba.

Akizungumza maandalizi ya mchezo huo, Kaimu Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Miguel Gamondi, alisema wachezaji wake wako tayari kupambana kupata ushindi katika mechi hiyo.

Alisema Uganda siyo timu kubwa huku Stars ikiwa na wachezaji mahiri wakiwemo Simon Msuva na Mbwana Samatta ambao wana uwezo wa kuipa ushindi timu hiyo.

“Uganda siyo timu kubwa, wao na sisi ni kama sawa tu, angalia hata utofauti wao uwiano wa wachezaji ndani na nje, kisha utaona ni dabi na itakuwa mechi ngumu, lakini ubora utendaji uwanjani utaamua mchezo.

“Kwa upande wetu tuna wachezaji wanaoweza kushinda huu mchezo tuna kina Msuva na Samatta na hilo ni jambo ambalo Watanzania wanapaswa kulifahamu, ” alisema Gamondi.

Kocha huyo alifafanua kuwa katika mechi ya leo mchezaji, Feisal Salumu atakuwepo katika timu baada ya kumaliza adhabu aliyokuwa akiitumikia, hivyo Watanzania wategemee mambo mazuri kutoka kwa Stars.

“Feisal Salumu ni mchezaji muhimu, alikuwa na adhabu anaitumikia ya mchezo mmoja hivi sasa tuko naye, kikubwa kwetu ni kuwa na maandalizi mazuri ambayo yatatupa matokeo mazuri,” alisema Gamondi.

Kocha huyo aliongeza kuwa watapambana kuhakikisha wanapata ushindi katika mchezo dhidi ya Uganda.

“Khalid Aucho ni mchezaji mzuri sana anafanya kazi nzuri mtu, humuoni akifunga lakini kwangu ni kiungo aliyekamilika mwenye ushawishi mkubwa, sijui historia ya Uganda nadhani ni moja kati ya wachezaji wakubwa waliowahi kutokea Uganda.

“Nimemfundisha akiwa na Yanga hivi sasa Singida Black Stars, mchezaji nzuri sana lakini wachezaji wangu wamejipanga kupata matokeo mazuri, japokuwa tunaelewa utakuwa mchezo wenye ushindani kubwa,” alisema.

Naye Simon Msuva alisema malengo yao ni kupata ushindi katika mchezo wa leo, hivyo watapambana kuhakikisha wanatimiza malengo yao ya kupata ushindi katika mechi ya leo.

Katika michuano mingine na mechi za kuwania kufuzu AFCON, miamba hiyo miwili ya Afrika Mashariki imewahi kukutana mara 61.

Katika mchanganuo huo, Uganda ndiyo kinara wa ubabe ikishinda mechi 33, Tanzania mechi 12 na timu hizo zimetoka sare mara 16.

Hivi karibuni, miamba hiyo ilikutana katika mechi za kuwania kufuzu fainali za AFCON 2023, ambapo Tanzania ilishinda bao 1-0 ugenini na Uganda ilipata ushindi kama huo ugenini.

Katika kundi hilo, Tanzania ilimaliza nafasi ya pili juu ya Algeria na kufuzu fainali hizo zilizopigwa nchini Ivory Coast.

Previous Post

WAZIRI MCHENGERWA AAGIZA UCHUNGUZI HOSPITALI YA TEMEKE

Next Post

MOROCCO ATOA TANO KOMBE LA MAPINDUZI

Next Post
MOROCCO ATOA TANO KOMBE LA MAPINDUZI

MOROCCO ATOA TANO KOMBE LA MAPINDUZI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

NITASHIRIKIANA NAYE KULETA MAENDELEO

NITASHIRIKIANA NAYE KULETA MAENDELEO

7 months ago
CHANETA IMANI KIBAO NA TUME HURU YA UCHUNGUZI

CHANETA IMANI KIBAO NA TUME HURU YA UCHUNGUZI

2 weeks ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?