• ePaper
Thursday, June 18, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

SERIKALI ZANZIBAR YAONGEZA TEKNOLOJIA KUDHIBITI MAKOSA YA BARABARANI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 6, 2026
in Habari, Kitaifa
0
SERIKALI ZANZIBAR YAONGEZA TEKNOLOJIA KUDHIBITI MAKOSA YA BARABARANI
0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDSIHI WETU

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali inaendelea kuimarisha matumizi ya mifumo ya kidigitali kama mkakati wa kudhibiti vifo vinavyotokana na ajali za barabarani pamoja na makosa ya usalama barabarani.

Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo alipokutana na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. George Simbachawene, aliyefika Ikulu Zanzibar kwa mazungumzo ya kikazi.

Amesema kukamilika kwa mifumo hiyo ya kidigitali, ikiwemo matumizi ya taa za kuongozea magari (Traffic Lights) pamoja na uwekaji wa rada za kudhibiti mwendo kasi, kutasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza makosa ya barabarani, vifo vinavyotokana na ajali pamoja na gharama za huduma za afya zinazobebwa na Serikali baada ya ajali kutokea.

Akizungumzia suala la unyanyasaji na ukatili wa kijinsia, ikiwemo vitendo vya ubakaji, Rais Dk. Mwinyi amesema Serikali imechukua hatua madhubuti kudhibiti vitendo hivyo, ikiwemo kuondoa dhamana kwa watuhumiwa wa makosa hayo pamoja na kuendelea kutoa elimu kwa umma dhidi ya vitendo vya udhalilishaji.

Vilevile, akizungumzia matukio ya uhalifu katika maeneo ya utalii, Rais Dk. Mwinyi amesema Serikali inaendelea kuchukua juhudi za kuimarisha usalama katika maeneo hayo, ikiwemo kuwataka wamiliki wa hoteli kufunga kamera za usalama (CCTV) ili kusaidia kudhibiti vitendo vya kihalifu.

Aidha, Rais Dk. Mwinyi amepongeza ushirikiano uliopo kati ya Wizara ya Mambo ya Ndani na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha utendaji wa pamoja wa taasisi za Uhamiaji, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) na Jeshi la Polisi, na kusisitiza umuhimu wa kuendeleza ushirikiano huo.

Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. George Simbachawene, ameonesha kuridhishwa na mchango pamoja na ushirikiano unaotolewa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha utendaji wa taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo, ikiwemo Uhamiaji, NIDA na Polisi. 

Previous Post

‘UONGOZI SIYO HOTUBA ZENYE KUKONGA NYOYO BALI MATOKEO’

Next Post

TRA INAVYOIMARISHA USHIRIKIANO NA WAFANYABIASHARA KUKUZA UCHUMI

Next Post
TRA INAVYOIMARISHA USHIRIKIANO NA WAFANYABIASHARA KUKUZA UCHUMI

TRA INAVYOIMARISHA USHIRIKIANO NA WAFANYABIASHARA KUKUZA UCHUMI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

ASKOFU MNDOLWA: TUME YA JAJI CHANDE ITAIPELEKA NCHI PAZURI

ASKOFU MNDOLWA: TUME YA JAJI CHANDE ITAIPELEKA NCHI PAZURI

2 months ago
MWIGULU APIGILIA MSUMARI

MWIGULU APIGILIA MSUMARI

5 months ago

Popular News

  • WABUNGE: AMANI ISICHEZEWE

    WABUNGE: AMANI ISICHEZEWE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WABUNGE WAIPONGEZA NSSF NA PSSSF KWA KUANZISHA SKIMU YA HIFADHI KWA WALIOJIAJIRI NA UWEKEZAJI WA KIWANDA CHA NGOZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WABUNGE WAPONGEZA UWEKEZAJI KLICL

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAKAGUZI WA CAF WARIDHISHWA NA MAENDELEO YA VIWANJA VYA AFCON 2027

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MKAKATI KUDHIBITI VIFO WAJAWAZITO WAANIKWA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?