• ePaper
Wednesday, April 22, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

NEEMA YA MAJI KILA KIJIJI 2030

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 29, 2026
in Habari, Kimataifa
0
NEEMA YA MAJI KILA KIJIJI 2030
0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na FRED ALFRED,

Dodoma

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan ameagiza Wizara ya Maji, kuhakikisha inafikisha huduma hiyo katika vijiji vyote nchini kabla ya mwaka 2030, ukiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Hayo yalibainishwa na Waziri wa wizara hiyo, Juma Aweso, alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya wizara hiyo, ndani ya siku 100 za uongozi wa Rais Samia.

Alisema hadi sasa, wizara imepeleka maji katika vijiji 10,758 kati ya 12,333 huku maagizo ya Rais Samia ni kuhakikisha vijiji 1,575 vilivyobaki, vinafikishiwa huduma hiyo kabla ya mwaka 2030.

“Rais Dk. Samia, ameagiza kuwa anapomaliza muda wake, vijiji 1,575 ambavyo  havina maji viwe vimefikiwa.  Ndiyo maana ameendelea kutoa fedha za kukamilisha miradi ya maji nchini.

Aliongeza kuwa :”Wizara ya Maji, hatuna kisingizo cha kutokamilisha miradi hiyo, hivi sasa tuna miradi 878 ambayo tunaendelea kuitekeleza vijijini, sisi tutahakikisha inakamilika kwa wakati.

Katika hatua nyingine, Aweso alisema ili kutimiza azma ya Rais Samia, wameanza kutekeleza mpango wa vijiji 9,00 ambapo utahusisha kila mbunge kuainisha vijiji ambavyo havina huduma ya maji, viweze kuwekwa katika mpango huo.

Waziri Aweso alieleza kuwa, kuna miradi zaidi ya miradi 200 ambayo inaendelea kutekelezwa mijini, lengo ni kuhakikisha inakamilika na kutoa huduma kwa wananchi.

GRIDI YA MAJI YA TAIFA.

Kuhusu utekelezaji wa Gridi ya Maji ya Taifa, Aweso alisema tayari wameanza kutekeleza miradi mbalimbali ukiwemo wa kutoa maji Ziwa Victoria hadi Dodoma, hadi sasa umefika Tabora.

Alisema tayari wamemaliza upembuzi yakinifu wa kutoa maji Tabora hadi Dodoma, hivi sasa wanatafuta mkandarasi.

“Tayari tumenza kutekeleza mpango wa kujenga gridi ya maji ya taifa ili kutatua changamoto ya upungufu wa maji nchini kwa kuunganisha miradi yote mikubwa na midogo.

Aliongeza kuwa:”Mpango huu, unalenga kuhakikisha huduma ya maji inapatikana kwa uhakikisha maeneo ya mijini na vijijini, ikiwa na lengo la kukamilisha ifikapo mwaka 2030 kama alivyoahidi Rais Samia.

MAAGIZO DAWASA

Katika hatua nyingine, Aweso alimwagiza Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salam (DAWASA), Mhandisi Mkama Bwire, kuhakikisha wananchi wanalipa bili kulingana na upungufu uliojitokeza katika kipindi cha Desemba mwaka jana.

“Tulipitia changamoto ya kutokuwa na maji kwa wananchi wa Dar es Salaam, itashangaza sana kuona wananchi wanapata bili kubwa kama ana kiwanda.

Previous Post

NI SIKU 100 ZA MAFANIKIO YA UTOAJI TIBA BORA JKCI

Next Post

WAFANYABIASHARA MSIWAUMIZE WANANCHI-DK. MWIGULU

Next Post
WAFANYABIASHARA MSIWAUMIZE WANANCHI-DK. MWIGULU

WAFANYABIASHARA MSIWAUMIZE WANANCHI-DK. MWIGULU

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SERIKALI IMEIMARISHA BARABARA – DK. SAMIA

SERIKALI IMEIMARISHA BARABARA – DK. SAMIA

7 months ago
SIKU 100 ZA KAZI NA UTU

SIKU 100 ZA KAZI NA UTU

2 months ago

Popular News

  • DK.NCHIMBI AMTAJA ASKOFU MFUMBUSA NGUZO YA UMOJA

    DK.NCHIMBI AMTAJA ASKOFU MFUMBUSA NGUZO YA UMOJA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SITAWAANGUSHA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA YATIMUA VUMBI CAF, SIMBA MMH

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA AMPA TANO SIMBU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAAJABU YA DP WORLD SIKU 730 BANDARINI DAR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?