• ePaper
Saturday, August 15, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

BILIONI 30/- KUJENGA UWANJA WA KISASA SIMBA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
August 10, 2026
in Burudani, Habari, Michezo
0
BILIONI 30/- KUJENGA UWANJA WA KISASA SIMBA
0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

RAIS wa Heshima na mwekezaji wa klabu ya Simba, Mohamed Dewji ‘Mo’, ameweka wazi kuwa ana mpango wa kuweka uwekezaji wa shilingi bilioni 30 kwa ajili ya kujenga uwanja wa mechi na viwanja sita vya mazoezi.

Aliyasema katika Uwanja wa Uhuru,Dar es Salaam, katika kilele cha Simba Day, kuwa mpango huo unalenga kwa ajili ya timu za Simba, Simba Queens, vijana na kuboresha miundombinu ya klabu kuwa ya kisasa.

“Ninaendelea kuahidi kuwa nitajenga uwanja na viwanja sita vya mazoezi kwa ajili ya Simba, Simba Queens, Simba vijana na vituo vya mazoezi ya ndani vya kisasa, yaani gym, kambi ya malazi na ofisi za kisasa,” alisema.

Mo alifafanua kuwa uwekezaji huo, umelenga kuweka msingi imara wa programu ya vijana ndani ya Simba, huku akisisitiza umuhimu wa klabu kuwa na mfumo wa kulea vipaji.

Mwekezaji huyo alisema tayari amepeleka pendekezo la uwekezaji huo katika Bodi ya Wadhamini ya Simba na sasa anasubiri majibu ili kuanza utekelezaji.

“Nimeweka mezani pendekezo la uwekezaji wa takribani shilingi  bilioni 30, nimefikisha kwa Bodi ya Wadhamini ya Simba na nasubiri majibu yao, mimi niko tayari hata kesho,” alisema Mo.

Wakati  huo huo, nyota wa Simba Selemani Mwalimu amewatoa hofu mashabiki wa Simba kuhusu hatma yake ndani ya timu na kuthibitisha kuwepo msimu wa 2026-2027.

Mwalimu, ambaye msimu uliopita aliitumikia Simba kwa mkopo akitokea Wydad Casablanca ya Morocco, amekuwa katika sintofahamu baada ya klabu hizo mbili kutofautiana.

Baada ya msimu wa 2025-2026 kumalizika, Simba ilitangaza kuwa imefikia makubaliano ya kuendelea na Mwalimu, lakini Wydad baadaye ilikanusha taarifa hizo.

Akizungumza kupitia video ilionyeshwa Uwanja wa Uhuru katika kilele hicho, Mwalimu aliwatumia ujumbe mashabiki wa Simba na kuthibitisha kuwa bado ni sehemu ya kikosi hicho.

Previous Post

WAMETISHA AISEE

Next Post

RAIS DK. SAMIA AWAPA RAHA VIGOGO USHIRIKA

Next Post
RAIS DK. SAMIA AWAPA RAHA VIGOGO USHIRIKA

RAIS DK. SAMIA AWAPA RAHA VIGOGO USHIRIKA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MWISHO WA ENZI

MWISHO WA ENZI

6 months ago
WADAU WAMGOMEA SAMATTA

WADAU WAMGOMEA SAMATTA

1 month ago

Popular News

  • KIINI DABI KARIAKOO KUPIGWA ZANZIBAR

    KIINI DABI KARIAKOO KUPIGWA ZANZIBAR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TAMU, CHUNGU DABI YA K’KOO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA AKUTANA NA VIONGOZI WA TEC

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA AWAPA RAHA VIGOGO USHIRIKA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • BILIONI 30/- KUJENGA UWANJA WA KISASA SIMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?