• ePaper
Friday, August 28, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

CCM INAHESHIMU UPINZANI–KIHONGOSI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
August 20, 2026
in Habari, Kitaifa
0
CCM INAHESHIMU UPINZANI–KIHONGOSI
0
SHARES
13
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na REHEMA MAIGALA

KATIBU wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kenani Kihongosi, amesema Chama kinaheshimu maoni ya wanasiasa na vyama vyote vya upinzani.

MAWAZO MBADALA

Pia, CCM imesisitiza iko tayari kuyafanyia kazi mawazo yenye msingi kutoka kwa vyama vya upinzani kwa maslahi mapana ya nchi.

Kihongosi alisema hayo jijini Dar es Salaam, katika kipindi kinachorushwa hewani na Redio Clouds, ambako alizungumzia masuala mbalimbali na hali ya siasa nchini.

Alifafanua, wanasiasa wanapaswa kutumia nafasi walizonazo kutoa ushauri unaolenga kuisaidia serikali na kutatua changamoto zinazowakabili wananchi.

Kihongosi alisema vyama vya upinzani vinapaswa kutoa ushauri kwa serikali kuhusu masuala yanayopaswa kufanyika, badala ya kulalamika bila kueleza sababu na nini kifanyike.

“Kiongozi mzuri ni yule anayelalamikia jambo na wakati huo huo kueleza namna ambavyo changamoto hiyo inaweza kutatuliwa,”alisema Kihongosi.

HALI YA SIASA

Akizungumzia hali ya kisiasa, Kihongosi alisema hali ya siasa nchini kwa sasa ni shwari, hivyo wanasiasa wanapaswa kutumia vyema nafasi hiyo kujenga siasa zenye maelewano mazuri.

“Ni vyema Tanzania kuwa na siasa zinazolenga kuleta maelewano ndani ya nchi, hizo ndizo siasa safi ndani ya taifa,” alisema Kihongosi.

MATUKIO YA OKTOBA 29

Kuhusu matukio ya Oktoba 29, mwaka jana, Kihongosi alisema wanasiasa hawapaswi kuyatumia kama mtaji wa kujijenga kisiasa, kwa kuwa walioathirika ni wananchi na watoto wa kawaida.

“Hakuna mtoto wa mwanasiasa aliyeathirika katika matukio ya Oktoba 29, hivyo wanasiasa tusitumie matukio yale kwa Chama hicho, Tundu Lissu,”aliongeza.

Katika hatua nyingine, Kiongosi alitoa wito kwa wanasiasa kudumisha upendo, amani na mshikamano akisema siasa zinapaswa kuwa sehemu ya kujenga nchi na si kuigawa.

Previous Post

PROF. KABUDI AWATAKA WANANCHI KUZINGATIA TAHADHARI ZA MAAFA

Next Post

CCM YATAKA VIONGOZI WASIOYUMBA -WASIRA

Next Post
CCM YATAKA VIONGOZI WASIOYUMBA -WASIRA

CCM YATAKA VIONGOZI WASIOYUMBA -WASIRA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

UKILA BATA KRISMASI, USISAHAU ADA JANUARI

UKILA BATA KRISMASI, USISAHAU ADA JANUARI

8 months ago
TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA KIMATAIFA KUKABILI UKAME

TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA KIMATAIFA KUKABILI UKAME

4 days ago

Popular News

  • TUME MIPANGO, NIRC WAJADILI UBORA MIRADI YA UMWAGILIAJI

    TUME MIPANGO, NIRC WAJADILI UBORA MIRADI YA UMWAGILIAJI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MASAUNI AANIKA UMAHIRI WA TANZANIA INAVYOLINDA UDONGO, MATUMIZI MBOLEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NDEJEMBI KUMRITHI BALOZI DK. NCHIMBI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUME YA MADINI YATOA SIKU 30 KWA WALIOKIUKA MIKATABA YA MSAADA WA KIUFUNDI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA ARIDHIA DK. NCHIMBI KUJIUZURU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?