• ePaper
Friday, August 28, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

MASAUNI AANIKA UMAHIRI WA TANZANIA INAVYOLINDA UDONGO, MATUMIZI MBOLEA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
August 27, 2026
in Habari, Kitaifa
0
MASAUNI AANIKA UMAHIRI WA TANZANIA INAVYOLINDA UDONGO, MATUMIZI MBOLEA
0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

ULAANBAATAR, Mongolia

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad Yussuf Masauni, amesema Tanzania imeweka mkazo katika elimu ya hali ya hewa, maendeleo na uwekezaji binafsi na ushirikiano kwa umma kwa lengo la kuongeza urejeshaji wa maeneo ya malisho, kila mmoja awe na wajibu wa kulinda udongo.

Pia, inakuza malisho endelevu, mipango shirikishi ya matumizi ya ardhi, urejeshaji maeneo ya malisho, miundombinu iliyoboreshwa ya maji, mifumo ya tahadhari ya mapema ya ukame na uzalishaji bora wa mifugo.

Waziri Masauni ameeleza hayo jijini Ulaanbaatar, Mongolia, Agosti 26, mwaka huu, katika kikao cha viongozi kutoka ndani na nje ya Bara la Afrika cha kujadili kuenea hali ya jangwa na ukame katika eneo la kuboresha afya ya udongo na matumizi sahihi ya mbolea.

Kikao hicho ambacho kimefanyika ofisi za ubalozi wa Uingereza, kimehudhuriwa na Mwakilishi Maalumu wa Uingereza, Ruth Davis, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), Beth Bechdol, Moses Vilakati, Kamishna wa Umoja wa Afrika (AU) anayeshughulikia Kilimo, Maendeleo ya Vijijini, Uchumi wa Bluu na Mazingira Endelevu pamoja na viongozi wengine kutoka mataifa mbalimbali.

“Kwa Tanzania, maeneo ya malisho ni muhimu sana kwa uzalishaji wa mifugo, usalama wa chakula, bayoanuwai, rasilimali za maji na maisha ya watu vijijini. Kutokana na idadi ya watu inayokadiriwa kufikia milioni 61.7, kuna ongezeko la shinikizo kwenye ardhi, maji na rasilimali asili,” amesema Masauni.

Amebainisha kwa mujibu wa Ripoti ya Utafiti wa Sampuli ya Kilimo wa Mwaka 2022/23 iliyotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Tanzania ilikuwa na kaya za wakulima milioni 8.97, ambapo asilimia 60.6 kati ya hizo zilijishughulisha na ufugaji hali inayodhihirisha umuhimu wa maeneo bora ya malisho kwa jamii na uchumi.

Hata hivyo, Masauni amesema maeneo ya malisho yanakabiliwa na shinikizo linaloongezeka kutokana na ukame, uharibifu wa ardhi, ufugaji kupita kiasi, mabadiliko ya matumizi ya ardhi, uhaba wa maji, uchomaji misitu na mabadiliko ya hali ya hewa.

Amefafanua kwa kutambua hilo, Tanzania imejiwekea mikakati kupitia Programu ya Kitaifa ya Kupambana na Kuenea Hali ya Jangwa na Ukame (2025-2030), unaozingatia utayari wa ukame, tahadhari ya mapema na usimamizi endelevu wa ardhi.

Waziri huyo ameeleza jitihada hizo zinaendana na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, hasa Nguzo ya Tatu ya Uhifadhi wa Mazingira na Ustahimilivu wa Mabadiliko ya Tabianchi, inayounganisha urejeshaji maeneo ya malisho na mabadiliko ya mifugo, usalama wa chakula na ustahimilivu wa hali ya hewa.

Mhandisi Masauni yupo Mongolia anakoshiriki Mkutano wa 17 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Kupambana na Kuenea Hali ya Jangwa na Ukame (UNCCD COP 17) ambao umeanza Agosti 24, mwaka huu

Previous Post

NDEJEMBI KUMRITHI BALOZI DK. NCHIMBI

Next Post

TUME MIPANGO, NIRC WAJADILI UBORA MIRADI YA UMWAGILIAJI

Next Post
TUME MIPANGO, NIRC WAJADILI UBORA MIRADI YA UMWAGILIAJI

TUME MIPANGO, NIRC WAJADILI UBORA MIRADI YA UMWAGILIAJI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

AZAM, YANGA MECHI YA KISASI, HESHIMA

AZAM, YANGA MECHI YA KISASI, HESHIMA

6 months ago
KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

10 months ago

Popular News

  • TUME MIPANGO, NIRC WAJADILI UBORA MIRADI YA UMWAGILIAJI

    TUME MIPANGO, NIRC WAJADILI UBORA MIRADI YA UMWAGILIAJI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MASAUNI AANIKA UMAHIRI WA TANZANIA INAVYOLINDA UDONGO, MATUMIZI MBOLEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NDEJEMBI KUMRITHI BALOZI DK. NCHIMBI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUME YA MADINI YATOA SIKU 30 KWA WALIOKIUKA MIKATABA YA MSAADA WA KIUFUNDI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA ARIDHIA DK. NCHIMBI KUJIUZURU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?