• ePaper
Wednesday, September 9, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

NDEJEMBI MZIGONI RASMI, AKEMEA KAZI KWA MAZOEA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 1, 2026
in Habari, Kitaifa
0
NDEJEMBI MZIGONI RASMI, AKEMEA KAZI KWA MAZOEA
0
SHARES
10
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI MAALUMU

MAKAMU wa Rais, Deogratius Ndejembi, amewataka watumishi wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira kuongeza bidii, uwajibikaji na kuachana na utendaji kazi kwa mazoea.

Pia, wahakikishe majukumu ya serikali yanatekelezwa kwa ufanisi na kwa wakati.

Ndejembi alitoa wito huo jijini Dodoma, alipofanya ziara yake ya kwanza katika Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), iliyopo Mtumba, ambako alipokelewa na wafanyakazi pamoja na menejimenti ya wizara hiyo.

Alisisitiza umuhimu wa watumishi, kubadili mitazamo na namna ya kufanya kazi, akitaka kila mmoja kuwa mbunifu na kuweka mipango inayolenga kuleta matokeo yanayoonekana kwa wananchi na taifa.

Makamu wa Rais, aliwasihi watumishi kutumia nafasi zao kutoa huduma yenye thamani kwa Watanzania na kutambua dhamana waliyonayo katika kuwahudumia wananchi.

Pia, aliwataka kubadili mitazamo na namna ya kufikiri, kuwa wabunifu na kuhakikisha mipango inayowekwa inakuwa na tija na matokeo chanya katika shughuli zinazotekelezwa kwa maslahi mapana ya Taifa.

Ndejembi aliwataka kuongeza jitihada katika kudumisha Muungano kwa kuwa na mipango endelevu, inayolenga kutatua changamoto mbalimbali na kutoa elimu ya fursa zilizopo katika Muungano.

Aliwasihi viongozi na watumishi wa wizara hiyo, kuwa na mipango endelevu katika utekelezaji wa ajenda ya ulinzi na uhifadhi wa mazingira kwa kutumia vizuri kampeni za upandaji miti, usafi wa majiji na miji kwa kuweka nyenzo zitakazosaidia kufanya hali hiyo kuwa endelevu.

Vilevile, Ndejembi alisisitiza umuhimu wa kuwa na mpango  maalumu utakaosaidia wananchi kuhama katika shughuli za kila siku zinazoharibu mazingira.

MHANDISI HAMAD YUSSUF MASAUNI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad Yussuf Masauni, alimpongeza Makamu wa Rais kwa kuaminiwa na Rais Samia Suluhu Hassan, katika nafasi hiyo na kumhakikishia ushirikiano kutekeleza majukumu mbalimbali yanayohusu Ofisi ya Makamu wa Rais.

DK. RICHARD MUYUNGI

Akiwasilisha taarifa kuhusu shughuli zinazotekelezwa na idara mbalimbali zilizo chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dk. Richard Muyungi, alisema wizara hiyo ina Idara nne, vitengo vinane na taasisi mbili zinazotekeleza majukumu mbalimbali, ukiwemo utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 katika masuala ya Muungano na Mazingira.

Wakati huohuo, Makamu wa Rais, Deogratius Ndejembi, anatarajiwa kuwasili leo mkoani Kilimanjaro kwa ziara binafsi ya kifamilia.

Lengo la ziara hiyo ni kusalimia na kupewa baraka na familia yake iliyopo Kata ya Bondeni, Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro.

Ziara hiyo, imekuja zikiwa zimepita siku mbili tangu kuapishwa kwake kuwa Makamu wa Rais wa Tanzania akichukua nafasi ya Dk. Emmanuel Nchimbi aliyejiuzulu kabla ya Chama Cha Mapinduzi kumfuta uanachama.

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari jana, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu, alisema hiyo ni ziara binafsi ya Makamu wa Rais.

Babu alisema Ndejembi anatarajiwa kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro asubuhi na kwenda moja kwa moja Mbuyuni, Manispaa ya Moshi, Kata ya Bondeni.

Previous Post

TUME MIPANGO, NIRC WAJADILI UBORA MIRADI YA UMWAGILIAJI

Next Post

WAZIRI AONYA, ATOA SIKU 60 WENYE SILAHA HARAMU

Next Post
WAZIRI AONYA, ATOA SIKU 60 WENYE SILAHA HARAMU

WAZIRI AONYA, ATOA SIKU 60 WENYE SILAHA HARAMU

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MABASI YA UMEME REKODI ZANZIBAR

MABASI YA UMEME REKODI ZANZIBAR

2 months ago
DK. SAMIA APOKEA HATI ZA MABALOZI, ATEUA VIGOGO PSSSF, TANESCO 

DK. SAMIA APOKEA HATI ZA MABALOZI, ATEUA VIGOGO PSSSF, TANESCO 

9 months ago

Popular News

  • RAIS DK. SAMIA, NDEJEMBI TURUFU YA MAENDELEO KWA WATANZANIA

    RAIS DK. SAMIA, NDEJEMBI TURUFU YA MAENDELEO KWA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI AONYA, ATOA SIKU 60 WENYE SILAHA HARAMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NDEJEMBI MZIGONI RASMI, AKEMEA KAZI KWA MAZOEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUME MIPANGO, NIRC WAJADILI UBORA MIRADI YA UMWAGILIAJI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MASAUNI AANIKA UMAHIRI WA TANZANIA INAVYOLINDA UDONGO, MATUMIZI MBOLEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?