• ePaper
Tuesday, April 21, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

DK. SAMIA APOKEA HATI ZA MABALOZI, ATEUA VIGOGO PSSSF, TANESCO 

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 12, 2025
in Habari, Kitaifa
0
DK. SAMIA APOKEA HATI ZA MABALOZI, ATEUA VIGOGO PSSSF, TANESCO 

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Jamhuri ya Slovakia hapa nchini, Ivan Lancaric, Ikulu Chamwino mkoani Dodoma Desemba 11, 2025.

0
SHARES
11
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

DODOMA
NA MWANDISHI WETU

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amepokea hati za utambulisho kutoka kwa mabalozi watano walioteuliwa kuziwakilisha nchi zao ambapo amesisitiza dhamira ya Tanzania kuimarisha ushirikiano unaojengwa kwa  misingi ya kuheshimiana, maendeleo ya pamoja na mahusiano mema.

Katika halfa hiyo iliyofanyika Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma, Dk. Samia aliweka msisitizo kwamba Tanzania na serikali wanazotoka mabalozi hao, zinachangia dhamira ya pamoja katika kukuza biashara, uwekezaji na maendeleo.

Pia, alisisitiza umuhimu wa ushirikiano wa kidiplomasia katika kukuza sekta muhimu za biashara na uwekezaji, kilimo, afya, elimu, nishati, uchumi wa buluu, utalii na teknolojia.

Mabalozi na waliowasilisha hati zao ni Domingos de Almeida da Silva Coelho, Balozi wa Angola, Marjo Johanna Jacoba Crompvoets, Balozi wa Ufalme wa Uholanzi na Mohammad Javad Hemmatpanah, Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.

Wengine ni Ivan Lančarič, Balozi wa Jamhuri ya Slovakia na Gabriel Pandureni Sinimbo, Balozi wa Jamhuri ya Namibia.

Rais Dk. Samia pia alisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano katika sekta za afya, elimu, uchumi wa buluu, utali, teknolojia.

Katika sekta ya elimu, alieleza dhamira ya serikali kuimarisha mafunzo ya ufundi stadi kwa vijana kupitia ushirikiano na nchi zenye utaalamu wa kiteknolojia ili kuwapatia vijana ujuzi utakaowezesha kuajiriwa au kujiajiri.

Vilevile, alizipongeza nchi hizo kwa mchango wao katika safari ya maendeleo ya Tanzania na kuhimiza ushirikiano wa kina zaidi unaoendana na Dira 2050 na Sera ya Mambo ya Nje inayotilia mkazo diplomasia ya uchumi, ushirikiano wa kimkakati na ushiriki hai katika majukwaa ya kikanda na kimataifa.

Katika hatua nyingine, Rais Dk. Samia aliwahakikishia mabalozi hao hali ya amani, utulivu na usalama nchini, akisisitiza kuwa Tanzania inabaki kuwa mahali salama kwa wananchi wake, wawekezaji na wafanyabiashara.

USHIRIKIANO NA ANGOLA

Ushirikiano huo unahusisha sekta za biashara, nishati, madini, uchumi wa buluu, mifugo na utalii,

USHIRIKIANO NA UHOLANZI

Ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na Uholanzi unahusisha sekta za kilimo, afya, elimu, uvuvi, maji na uwekezaji.

USHIRIKIANO NA IRANI

Ushirikiano uliopo baina ya Tanzania  Jamhuri ya Kiislamu ya Iran umejikita katika sekta za biashara, nishati, teknolojia, kilimo, afya na elimu.

USHIRIKIANO NA SLOVAKIA

Ushirikiano na taifa hilo unaakisi maeneo ya nishati jadidifu, ubunifu wa kidijitali, uzalishaji viwandani, usalama wa mtandao, elimu na utalii. 

Slovakia imefungua hivi karibuni ubalozi wake nchini Tanzania, hatua inayochochea ushirikiano wa muda mrefu wa kiuchumi na maendeleo.

USHIRIKIANO NA NAMIBIA

Ushirikiano unahusisha biashara, uchumi wa buluu, nishati, madini, mifugo na utalii. Pia, ugunduzi wa mafuta na gesi nchini Namibia ni fursa ya kujenga uwezo wa pamoja na ushirikiano katika mnyororo wa thamani wa nishati katika siku zijazo.

Wakati huo huo, Rais Dk. Samia amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali ambapo kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dk. Moses Kusiluka, ilisema Fortunatus Makore Magambo ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mifuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF). 

Kabla ya Uteuzi huu, Magambo alikuwa Mkurugenzi wa Mipango, Uwekezaj na Miradi katika mfuko huo huku  Plasduce Mkeli Mbosca ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Previous Post

ONDOENI HOFU

Next Post

WANNE ‘BYE BYE’ YANGA

Next Post
WANNE ‘BYE BYE’ YANGA

WANNE ‘BYE BYE’ YANGA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

6 months ago
TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

6 days ago

Popular News

  • MUDATHIR KUIKOSA SIMBA

    MUDATHIR KUIKOSA SIMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ‘MISS WORLD’ KUIPAISHA TANZANIA DUNIANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • BIL. 195.66/- KUJENGA BONDE MTO MSIMBAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ULEGA AJIBU MAPIGO KUHUSU MTANDAO WA BARABARA NCHINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NEEMA YAJA, MIKAKATI HADHARANI KUINUA VIJANA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?