• ePaper
Friday, May 1, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

TEMBO WARRIORS KUFANYIWA MCHUJO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
August 31, 2025
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
WACHEZAJI WA TEMBO WARRIORS
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na AMINA KASHEBA

KOCHA wa timu ya taifa ya Soka kwa Watu Wenye Ulemavu ‘Tembo Warriors’, Ivo Mapunda, anatarajia kufanya mchujo wa wachezaji ambao watakwenda kuwakilisha nchi katika mashindano ya Afrika Mashariki na Kati (CECAFA).

Wachezaji 25 watachujwa na kubakia 15 ambao watasafiri kwenda Burundi katika michuano hiyo itakayofanyika Septemba 6, mwaka huu.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Ufundi wa timu hiyo, Shaban Msangi amesema licha ya changamoto wanazopitia, Kocha Mapunda anatarajia kufanya mchujo wa kupunguza wachezaji ili kubaki na 15 watakakwenda nchini Burundi.

Amesema bado Kocha Mapunda anaendelea kuwanoa wachezaji wote, hivyo watakaoonyesha kiwango bora ndiyo watakaochaguliwa kuunda kikosi hicho.

“Wachezaji 25 watafanyiwa mchujo wiki ijayo kupata wachezaji 15 ambao watawenda Burundi kuiwakilisha Tanzania katika michuano hiyo itakayoshirikisha nchi mbalimbali.

“Kocha anaendelea kuwanoa wachezaji wote, hivyo watakaoonyesha kiwango bora ndiyo watakaochaguliwa kuunda kikosi hicho,” amesema.

Mkurugenzi huyo amesema hivi sasa wanapitia changamoto ya fedha ya usafiri na malazi kipindi watakapofika nchini uko.

Msangi amesisitiza wanawaomba wadau mbalimbali kujitokeza kuwapata sapoti kuhakikisha wanafikia malengo ikiwemo kubeba taji hilo msimu huu.

“Tunawaomba wadau wa michezo kuendelea kutushika mkono tunashukuru Baraza la Michezo la Taifa (BMT) wametupatia usafiri.

“Bado tunakabiliwa na ukata wa fedha, hivyo tunawaomba wadau mbalimbali kujitokeza kutupa sapoti ili tufikie malengo ikiwemo kutwaa ubingwa wa michuano hiyo,” alisema.

Ofisa Habari na Mawasiliano wa timu hiyo, Khalid Msabaha amesema malengo yao ni kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania ikiwemo kurejea nchini na ubingwa.

Amesema wachezaji wanafanya mazoezi kwa morali kubwa kuhakikisha wanafikia malengo ikiwemo kuonyesha kiwango bora.

Previous Post

BALOZI DK. NCHIMBI AZURU KABURI LA HAYATI MWALIMU NYERERE

Next Post

DK. MWINYI ACHUKUA FOMU ZANZIBAR, AHADHARISHA CHUKI

Next Post
DK. MWINYI ACHUKUA FOMU ZANZIBAR, AHADHARISHA CHUKI

DK. MWINYI ACHUKUA FOMU ZANZIBAR, AHADHARISHA CHUKI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

TAIFA STARS KUKIPIGA FIFA SERIES 2026

TAIFA STARS KUKIPIGA FIFA SERIES 2026

2 months ago
TAIFA STARS KATIKA AFCON YA NDOTO

TAIFA STARS KATIKA AFCON YA NDOTO

4 months ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?