• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

CCM YATAJA VIPAUMBELE VYAKE WILAYA YA KALAMBO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 10, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
CCM YATAJA VIPAUMBELE VYAKE WILAYA YA KALAMBO

Mgombea Mwenza wa Urais wa CCM, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi

0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NJUMAI NGOTA, 

Rukwa

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimetaja baadhi ya vipaumbele vyake vya maendeleo, itakavyotekeleza kwa kipindi cha miaka mitano ijayo katika Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo, mkoani Rukwa.

Vipaumbele hivyo ni pamoja na uanzishwaji kongani ya viwanda vya kusindika samaki na mazao ya maziwa.

Pia, uboreshaji wa huduma za jamii na uimarishaji miundombinu ya uzalishaji.

Lengo la kuanzishwa viwanda hivyo ni kukuza uchumi wa wananchi kupitia sekta za kimkakati.

Hayo yalibainishwa na Mgombea Mwenza wa Urais wa CCM, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, katika mkutano wa hadhara wa kampeni, uliofanyika, wilayani Kalambo.

Chama, kilianza kampeni zake Agosti 28, mwaka huu na kuelezea utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2030 na kuinadi Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2025-2030.

Aidha, kuwaombea kura za kishindo wagombea wanaotokana na Chama akiwemo Mgombea Urais wa CCM, Dk. Samia Suluhu Hassan, katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu.

Dk. Nchimbi, alisema katika kipindi cha miaka mitano ijayo, iwapo watapewa ridhaa ya kuongoza nchi, wamekusudia kuanzisha kongani ya viwanda vya kusindika samaki na mazao ya maziwa katika halmashauri hiyo.

“Katika eneo la viwanda, tumekusudia kuanzisha kongani ya viwanda vya kusindika samaki na mazao ya maziwa. “Kalambo ni eneo mojawapo linalopewa nafasi ya ujenzi wa kongani hiyo,” alisema.

Alisema hiyo ni hatua kubwa ya kuhakikisha uvuvi na mazao ya mifugo kama maziwa, yanapata thamani ya ziada.

Kwa mujibu wa Dk. Nchimbi, wamejipanga kikamilifu kuhakikisha maendeleo hayo, yanawafikia wananchi wa Kalambo.

Alitaja kipaumbele kingine kinachokusudiwa kutekelezwa katika halmashauri hiyo ni kujengwa mabwawa mapya ya uvuvi na vizimba vya kufugia samaki.

Alisema kitaanzishwa kituo cha ukuzaji viumbe vya majini na kuwa, mbegu za samaki zitapatikana katika kituo kipya cha kitakachojengwa Kalambo.

AFYA

Dk. Nchimbi, alisema serikali ijayo, imekusudia kujenga zahanati 16 mpya na vituo vya afya vitano ndani ya halmashauri hiyo, ukiwa ni mkakati wa kupeleka huduma karibu zaidi na wananchi.

ELIMU

Alisema katika sekta ya afya, wamedhamiria kujenga sekondari 14 mpya na madarasa zaidi ya 80 pamoja na kuboresha miundombinu ya shule zilizopo.

MAJI SAFI NA SALAMA

Dk. Nchimbi, alisema katika miaka hiyo ijayo, wanatarajia kupeleka maji safi na salama katika vijiji 83.

Hatua hiyo, itaongeza upatikanaji wa huduma hiyo, kutoka asilimia 62 hadi 92 na kuwezesha takriban watu 92 kati ya kila 100 kupata maji safi.

MIUNDOMBINU NA NISHATI

Pia, alisema kwa upande wa barabara na madaraja, watakamilisha na kuimarisha yote yaliyopo ndani ya wilaya hiyo.

Alisema serikali ijayo, imekusudia kukamilisha kituo cha kupoza umeme cha Kalambo, kukomesha tatizo la umeme wa mgawo na kuwawezesha wananchi kuwa na uhakika wa nishati hiyo kwa shughuli za uzalishaji.

SIKU 100 ZA KWANZA

Vilevile, Balozi Dk. Nchimbi, alisema katika siku 100 za kwanza, Dk. Samia, ameweka dhamira ya dhati kuhakikisha kila Mtanzania, anasikilizwa na kupatiwa majibu ya changamoto zake kwa wakati, kupitia njia ya mtandao.

Alisema serikali ijayo, imejipanga kutekeleza mpango wa kuanzisha mfumo huo kutoka ngazi ya kijiji hadi taifa, lengo likiwa ni kurahisisha mawasiliano kati ya wananchi na serikali, kuongeza uwajibikaji kwa watendaji.

 “Mgombea urais, anatuambia mara nyingi, Watanzania wana changamoto, wana kero, zinasikilizwa muda mrefu hazipati majibu.

“Dk. Samia Suluhu Hassan, katika siku 100 za kwanza, ameahidi atakwenda kutengeneza utaratibu, raia kuanzia ngazi ya kijiji, vitongoji watafikisha kero zao serikalini kwa njia ya mtandao.

“Pia, kuanzia ngazi zote, zitaona tatizo lililowasilisha saa ngapi, tarehe ngapi na ngazi zote, zitajua nani hakutimiza wajibu wake, kama ofisa tarafa, mkuu wa mkoa, mkuu wa wilaya, mkurugenzi, mkuu wa mkoa kama waziri, tutaona hadi ngazi ya taifa,”aliseama.

Alisema njia hiyo itakuwa rahisi kuwaajibisha kwa kutotimiza wajibu wao kwa wananchi.

“Dk. Samia anataka serikali yake, iende ikawatumikie Watanzania, anataka serikali ya CCM iwatumikie Watanzania kwa haraka, wajue hii ni serikali yao,”alisema.

Previous Post

WAKAZI WA RUKWA WAAHIDI ‘MITANO TENA’ KWA DK. SAMIA

Next Post

DK. SAMIA AELEZA MAFANIKIO YA UONGOZI WAKE

Next Post
DK. SAMIA  AELEZA MAFANIKIO YA UONGOZI WAKE

DK. SAMIA AELEZA MAFANIKIO YA UONGOZI WAKE

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

‘WALIPENI WAKULIMA, WAFANYAKAZI’

‘WALIPENI WAKULIMA, WAFANYAKAZI’

1 month ago
CHAMA MENO NJE SINGIDA BLACK STARS

CHAMA MENO NJE SINGIDA BLACK STARS

1 month ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.