• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

DK. BASHIRU AELEZEA UJASIRI WA DK. SAMIA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 11, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
DK. BASHIRU AELEZEA UJASIRI WA DK. SAMIA
0
SHARES
1
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MUSSA YUSUPH,

Singida

KATIBU Mkuu Mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Bashiru Ali, amefunguka kuhusu ujasiri wa Mgombea Urais kupitia CCM, Dk. Samia Suluhu Hassan, ulivyoliwezesha Taifa kuvuka katika kipindi kigumu alipoingia madarakani.

Dk. Bashiru ambaye pia ni Mratibu wa Kampeni za Mgombea Urais Kanda ya Kati, alisema Dk. Samia kwa ujasiri, alifanikiwa kuivusha nchi salama baada ya kifo cha aliyekuwa Rais Dk. John Magufuli na mlipuko wa ugonjwa wa UVIKO -19.

Akizungumza na maelfu ya wananchi waliofurika katika mkutano wa kampeni, uliofanyika Uwanja wa Bombadia, Singida Mjini, alisema hizo ni sababu za kutosha kumpa Dk. Samia, nafasi nyingine ya kuliongoza Taifa.

Katibu mkuu huyo mstaafu wa CCM, alisema alishiriki moja kwa moja katika vikao vya maamuzi ndani ya Chama ni shahidi namna Dk. Samia alivyoivusha nchi.

“Mnanijua mimi siyo mtu wa kupindisha. Hali haikuwa rahisi. Tulimpoteza kiongozi jasiri na wakati huo, tukakumbwa na COVID-19. Lakini, tulivuka salama. Huu ni ushahidi wa ujasiri wake.

“Nilikaa kimya kwa muda, lakini leo (jana), nimeibuka kwa nguvu mpya. Ushuhuda wangu ni wa wazi, Rais Samia ni kiongozi wa mfano.

“Msiwe na mashaka, ameshika nchi wakati mgumu na akatuvusha. Hiyo ni sifa tosha ya kuongezewa muda,”alibainisha.

Aliongeza kuwa, katika mazingira hayo, mataifa mengi huvurugika, ila Tanzania ilibaki yenye mshikamano kwa sababu ya utulivu wa Rais Dk. Samia na misingi imara ya Chama.

Dk. Bashiru, alisema uzoefu wake, unamtosha kusema wazi kwamba, Dk. Samia, ameonesha uongozi wa kiwango cha juu hasa katika usawa wa kijinsia na heshima ya binadamu.

“Usawa wa binadamu haumaanishi wote tuwe na kimo au rangi moja. Usawa ni kuheshimu utu wa kila mtu. Tajiri na maskini wakikosa maji au afya, wote wanadhalilika. 

“Ndiyo maana CCM inajenga shule, zahanati na kusambaza maji kulinda utu wa kila Mtanzania,” alisema.

Dk. Bashiru, alisema kwa muda mrefu, nafasi ya mwanamke imekuwa ya pili, kupitia uongozi wa Rais Dk. Samia, hali imebadilika na wanawake sasa wanaongoza mikoa, wilaya na majimbo kwa mafanikio makubwa.

“Nilikuwa nazungumza na Mwenyekiti wa Mkoa (Martha Mlatha). Singida mna RC (Mkuu wa Mkoa) mwanamke, RAS (Katibu Tawala Mkoa) mwanamke, Mwenyekiti wa CCM ni mwanamke na hakuna kilichoharibika.

Hii ni dalili ya kuaminika kwa wanawake,” alieleza.

Alisema hata katika majimbo ya uchaguzi, wanawake wamepewa nafasi na wanaendelea kuthibitisha uwezo wao wa kiuongozi bila doa.

Alisisitiza kuwa, misingi ya usawa, mshikamano na amani, ndiyo msingi wa umoja wa kitaifa na kwamba, serikali ya CCM, chini ya Dk. Samia, imeendelea kuilinda misingi hiyo.

Previous Post

JK AMWOMBEA KURA DK. SAMIA

Next Post

‘MIFUMO YA UUZAJI MAZAO YA WAKULIMA, WAIMARISHWA’

Next Post
‘MIFUMO YA UUZAJI MAZAO YA WAKULIMA, WAIMARISHWA’

‘MIFUMO YA UUZAJI MAZAO YA WAKULIMA, WAIMARISHWA’

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MGOMBEA Mwenza wa Urais, Dk. Emmanuel Nchimbi, akiweka shada la maua kwenye kaburi la Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, Butiama, mkoani Mara. (Picha na Abdurahman Jumanne)

BALOZI DK. NCHIMBI AZURU KABURI LA HAYATI MWALIMU NYERERE

2 months ago
DK. NCHIMBI AMTAJA DK. SAMIA UJENZI BANDARI YA KWALA

DK. NCHIMBI AMTAJA DK. SAMIA UJENZI BANDARI YA KWALA

4 days ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.