• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

CCM Z’BAR YAAHIDI KAMPENI ZA KISTAARABU

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 13, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
CCM Z’BAR YAAHIDI KAMPENI ZA KISTAARABU

Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Hussein Ali Mwinyi

0
SHARES
1
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

NA HANIFA RAMADHANI, 

Zanzibar

IKIWA leo Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa upande wa Zanzibar kinazindua kampeni zake, Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama hicho Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesisitiza kuwa, CCM itafanya kampeni za kistaarabu, itahubiri amani, umoja, mshikamano na kuondoa ubaguzi katika jamii.

Amesema, kuna baadhi ya vyama ambavyo havina sera na badala yake, wapo kuhubiri chuki na mgawanyiko jambo, ambalo litasababisha kuivuruga amani iliyopo nchini.

Dk. Mwinyi, aliyasema hayo Mjini Unguja, alipokutana na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari.

“Binafsi mimi niliwahi kusikia watu wapo katika majukwaa, sijawasikia hata siku moja wakinadi sera zao, pengine, hawana kwa sababu serikali ya awamu ya nane, imefanya kila kitu, ndiyo maana wamebaki kuhubiri chuki,” alisema.

Aliongeza kuwa: “Ukipanda katika jukwaa leo kuzungumzia elimu utasema nini? utaishinda vipi CCM katika elimu, badala yake utageuza maneno badala ya kuzungumza elimu, afya, maji na mengineyo utaanza kusema huyu kafanya hivi, sasa hapo unamsaidiaje mzanzibari katika hilo?,” alisema.

Alisema kuna kila dalili kwamba, miaka yote ya uchaguzi kipindi kama hiki kunakuwa na sintofahamu na sasa hivi kumetulia kabisa na kusisitiza kuendelea namna hivyo hadi zitakapomalizika kampeni.

“Kuanzia Kesho (leo) mtawasikia katika majukwaa, badala ya kusema mtafanya nini kuwafanyia wazanzibari basi wao watakuwa wanawasema watu, nyie sikilizeni achaneni nao, tunaomba wasihimize au wasihubiri mgawanyiko, mfarakano, chuki katika nchi,”alisema.

Alieleza kuwa, Wazanzibari wanataka kuendelea kubaki na amani iliyopo hivyo alivisistiza vyama vyengine kuhubiri amani na kuacha kufanya siasa za chuki.

Aidha, Dk. Mwinyi aliwaomba waandishi wa habari kuhubiri na kuandika amani na wale ambao wanahubiri chuki basi kuachana nao.

“Nyinyi waandishi wa habari mna nguvu kubwa sana hivyo nawaomba tuandike amani, wale ambao wanahubiri chuki basi tuachane nao, ukichukua wewe mwandishi ukaandika maneno ya chuki, basi kalamu yako ina nguvu sana,” alisema

Aliongeza kuwa: “Huu kwangu ni wito kwenu nikitambua umuhimu wa ninyi waandishi na vyombo vyenu katika maswala ya amani katika nchi,tujitahidi kuidumisha amani tuliyonayo ili tuweze kupata maendeleo zaidi,” alisistiza Dk. Mwinyi.

Previous Post

AELEZA CCM ITAKAVYO JENGA UCHUMI JUMUISHI

Next Post

NCHIMBI AFAFANUA MAFANIKIO SEKTA ZA KILIMO, UFUGAJI, UTALII

Next Post
NCHIMBI AFAFANUA MAFANIKIO SEKTA ZA KILIMO, UFUGAJI, UTALII

NCHIMBI AFAFANUA MAFANIKIO SEKTA ZA KILIMO, UFUGAJI, UTALII

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WAZIRI MKUU AWAPA ‘TANO’ WANAOCHAPAKAZI SERIKALINI

WAZIRI MKUU AWAPA ‘TANO’ WANAOCHAPAKAZI SERIKALINI

1 month ago
TANZANIA NA CHINA ZAKUBALIANA KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIMKAKATI

TANZANIA NA CHINA ZAKUBALIANA KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIMKAKATI

3 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?