• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Burudani

‘GOLI LA MAMA’ LAIPA MORALI YANGA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 21, 2025
in Burudani, Michezo
0
‘GOLI LA MAMA’ LAIPA MORALI YANGA
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na AMINA KASHEBA

UONGOZI wa Yanga umesema morali imepanda kushinda mechi nne za mwanzo katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika ili  kuchukua zawadi ya ‘Goli la Mama’ shilingi milioni 100.

Alisema hayo Dar es Salaam, Ofisa Habari na Mawasiliano wa Yanga, Ally Kamwe alisema malengo yao ni kuhakikisha wanashinda kila mchezo kwa lengo la kuwapa furaha mashabiki na kuchukua fedha za ‘Goli la Mama’ zinatolewa na Rais Dk.Samia Suluhu Hassan.

“Sisi msimu huu wa 2025/26, tunahitaji kitu cha tofauti katika aina ya uchezaji kwa kila mechi ambazo tutacheza katika michuano ya kimataifa,hamasa ya Rais kupitia ‘Goli la Mama’imeleta morali kubwa,”alisema.

“Kocha aina kama Folz wanapiga hesabu ya mbali ya kushinda kila mchezo na ndiyo malengo yetu hivi sasa ya kufanya vizuri kwa kila mechi ambayo tutacheza,” alisema Kamwe.

Ofisa huyo alifafanua kuwa mpira wa hivi sasa kila timu inakuwa na mpango kabambe wa kuhakikisha inafanya vyema katika mechi zao za kimataifa.

“Watu wanasema Yanga haijacheza vizuri katika mechi ya Ligi ya Mabingwa, michuano hii tutaenda nayo mpaka mwisho kabisa kwa kutumia hesabu  kali,” alisema.

Kamwe alisema miongoni mwa timu ambazo zimepata kocha mzuri ni Yanga kutokana na aina ufundishaji wake wa kisasa tofauti na mwalimu mwingine.

“Hivi sasa tunahitaji kucheza mechi na kushinda na kuendelea na mambo mengine, mchezo wetu  Pamba ambao utafanya kesho utaona kitu cha tofauti kabisa,” alisema Kamwe.

Alisema kila timu ambayo itakutana na Yanga itegemee kupigwa mabao mengi bila kuonewa huruma ya aina yoyote ile.

Pia, ofisa huyo alimshukuru Rais Samia kwa kuweka hamasa ya fedha katika kila goli litalofungwa na timu za Tanzania kwa vile zimeongeza ushindani.

Kauli hiyo, imekuja baada ya mwishoni mwa wiki, Yanga ilianza michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL),  kwa kuichapa timu ya Wiliete ya Angola kwa mabao 3-0.

Pambano hilo, lilipigwa katika Uwanja wa  11 de Novembro jijini Luanda.Lakini timu hizo zitarudiana Septemba 27, mwaka huu  katika  Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam na mshindi wa jumla atapambana na mshindi wa jumla kati ya Elgeco Plus ya Madagascar na Silver Strikers ya Malawi.

Ushindi huo umeipa Yanga  kupata shilingi milioni 15 ikiwa ni zawadi kutoka kwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan maarufu kama ‘Goli la Mama’, ikiwa ni motisha ya kila goli shilingi milioni tano katika hatua ya awali ya mashindano hayo.

Katika michuano hiyo, timu zote zinazoshiriki hatua ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL), zitavuna dola za Marekani 100,000 ambazo ni zaidi ya sh. milioni 244 za Tanzania.

Katika CAFCL, timu zitakazotinga hatua ya makundi zitakuwa na uhakika wa kuvuna dola za Marekani 700,000 ambazo ni zaidi ya sh. bilioni 1.7 za Tanzania.

Timu zitakazotinga robo fainali, kila moja itakuwa na uhakika wa kuvuna dola za Marekani 900,000 ambazo ni zaidi ya sh. bilioni 2.2 wakati zitakazoishia nusu fainali zikivuna dola za Marekani milioni 1.2 ambazo ni zaidi ya sh. bilioni 2.9 za Tanzania.

Bingwa wa CAFCL msimu huu, anatarajiwa kuondoka na dola za Marekani milioni 4 ambazo ni zaidi ya sh. bilioni 9.7 za Tanzania wakati mshindi wa pili ikiondoka na dola za Marekani milioni mbili ambazo ni zaidi ya sh. bilioni 4.9 za Tanzania.

Previous Post

DK. NCHIMBI : WANANCHI MIKOA 11 KUMPA RAHA DK. SAMIA

Next Post

SIRI YA SIMBA YAVUJA

Next Post
SIRI YA SIMBA YAVUJA

SIRI YA SIMBA YAVUJA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. MWINYI AFUNGUKA MALENGO SERA YA NISHATI

DK. MWINYI AFUNGUKA MALENGO SERA YA NISHATI

1 month ago
DK. MWINYI: SITAKI KUACHA DENI

DK. MWINYI: SITAKI KUACHA DENI

1 month ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.