• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

DK. SAMIA KUWAINUA WANANCHI KIUCHUMI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 11, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
DK. SAMIA KUWAINUA WANANCHI KIUCHUMI

MGOMBEA Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan

0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MUSSA YUSUPH,

Musoma

MGOMBEA Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema mkakati wa serikali katika miaka mitano ijayo ni kuendelea kuwawezesha wananchi kiuchumi.

Akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika Musoma Mjini mkoani Mara, Dk. Samia alisema kipaumbele cha serikali ni kuimarisha maisha ya wananchi.

“Kwa upande wa uwezeshaji wa wananchi kiuchumi, serikali inakuja na mradi wa kujenga stendi na masoko nchi nzima kutoa fursa kwa wafanyabiashara ndogondogo.

“Kupitia mfuko wa halmashauri wa asilimia 10 ambao tumeugawa kwa makundi ya wanawake, vijana na wenye ulemavu nayo hiyo ni fursa nyingine ya kuwezesha wananchi kiuchumi,” alisema.

Alisisitiza: “Hivyo kijana jipange ujue unataka kufanya biashara gani, stendi tunajenga, masoko tunajenga, mifuko ya kukuwezesha ipo hivyo sema unataka kufanya biashara gani?

“Kubwa zaidi tumesema katika ilani mpya tunakwenda kurasimisha biashara ndogondogo zitambulike, ziwe rasmi mfaidike sawa na wafanyabiashara wengine.”

Dk. Samia alisema katika kuwawezesha wananchi, serikali pia imekuja na mfumo wa ruzuku katika kilimo na pembejeo.

Alisema serikali inaendeleza mkakati wa kilimo cha umwagiliaji kwa kujenga skimu na mabwawa huku upande wa uvuvi imefanya mengi zaidi ikiwemo ufugaji samaki kwa mabwawa na vizimba.

Previous Post

DK. SAMIA : WANAWAKE TUNA UWEZO KUONGOZA

Next Post

KIHONGOSI AWATAKA VIJANA KUTOKUBALI KUVURUGA AMANI

Next Post
KIHONGOSI AWATAKA VIJANA KUTOKUBALI KUVURUGA AMANI

KIHONGOSI AWATAKA VIJANA KUTOKUBALI KUVURUGA AMANI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

9 hours ago
KIBU DENIS, MANULA WATEMWA STARS

KIBU DENIS, MANULA WATEMWA STARS

1 month ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.