• ePaper
Friday, November 14, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

DK. MWINYI AAHIDI KITUO CHA HUDUMA WENYE ULEMAVU

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 16, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
DK. MWINYI AAHIDI KITUO CHA HUDUMA WENYE ULEMAVU

MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Hussein Ali Mwinyi

0
SHARES
1
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na HANIFA RAMADHANI,

Zanzibar

MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameahidi kuanzisha kituo maalumu cha utoaji huduma za kitabibu kwa watu wenye ulemavu.

Hatua hiyo ni dhamira yake ya kuhakikisha kundi hilo, linapata huduma bora za afya na haki sawa katika jamii.

Dk. Mwinyi aliyasema hayo, wakati akizungumza na kundi la watu wenye ulemavu, ukiwa ni mwendelezo wa kampeni zake za kukutana na makundi mbalimbali, Kikwajuni, Mjini Unguja.

Alisema anatambua kuwa, watu wenye ulemavu, wanahitaji kituo au sehemu maalumu ya kupata matibabu yao, akasisitiza serikali imelifikiria kazi jambo hilo, litatekelezwa.

 “Tutaweza kuanzisha kituo maalumu cha utoaji huduma za watu wenye ulemavu kwa vitu vingi ambavyo wanavihitaji, waweze kuvipata sehemu moja,” alisema.

Alisema kitengo muhimu katika utoaji huduma za watu wenye ulemavu ni kitengo cha tiba ya mazoezi ya viungo ‘physiotherapy’.

Alisema hiyo ni sehemu muhimu katika kusaidia kundi hilo, kurejea katika hali bora ya afya na kushiriki kikamilifu katika shughuli za kijamii na kiuchumi.

Alibainisha kuwa, hatua hiyo inalenga kuboresha huduma za afya na ustawi wa kundi hilo muhimu katika jamii.

Dk. Mwinyi, alisema serikali itahakikisha huduma hizo, zinatolewa katika viwango vya juu na kuendelea kutekeleza sera na mipango inayolenga kuimarisha usawa na fursa kwa watu wote.

UWEZESHAJI KWA WENYE ULEMAVU.

Alisema anatambua kuwa, wenye ulemavu wana mahitaji matatu katika uwezeshaji ambayo ni mafunzo ya ujasiriamali, mazingira mazuri ya kufanyia shughuli na kupatiwa mikopo isiyo na riba.

Alisema hayo yote, serikali yake katika awamu iliyopita imeshayaanza na kuahidi kuyaendeleza katika awamu ijayo kwa nguvu kubwa Zaidi.

Pia, alisema atahakikisha kuwa, mafunzo yanatolewa kwa watu wenye ulamavu ambao ni wajasiriamali waweze kuendesha vizuri shughuli zao.

Vilevile alisema wataendelea kuweka mazingira bora, wajasiriamali wote hususan wenye ulamevu, wapate maeneo ya kufanyia shughuli zao kila eneo lililotengwa.

Kuhusu suala la mitaji, Dk. Mwinyi, alisema serikali inaendelea kutoa mikopo ambapo ipo isiyo na riba, inayozingatia kundi hilo.

Aliahidi kuendelea kuwapatia mikopo hiyo na kuhakikisha kundi kubwa la watu wenye ulemavu, linapata mikopo hiyo.

AJIRA KWA WENYE ULEMAVU

Katika eneo la ajira, alisema katika serikali kuna sera ambayo ina mazingatio maalumu kwa watu wa kundi hilo kupatiwa ajira.

Hivyo, alisema katika vyombo vya utungaji sheria, atahakikisha kuwa kuna idadi nzuri ya watu wenye ulemavu.

Alisema watazingatia suala la ajira kwa watu wenye ulemavu kama ilivyo kwa wengine.

Aidha, alisema hata katika nafasi za uongozi, atahakikisha kundi hilo linakuwa kubwa zaidi.

Dk. Mwinyi, alibainisha kuwa, serikali yake itaendelea kuzingatia mahitaji ya watu wenye ulemavu katika vyuo vya amali.

Aliahidi kuendelea kuweka mkazo wa kuangalia mahitaji maalumu ya wanafunzi wenye ulemavu katika vyuo vya mafunzo ya amali.

KUONDOA USHURU

Kuhusu upatikanaji wa vifaa visaidizi kwa watu wenye ulamvu, Dk. Mwinyi alisema, serikali itaendelea kulisaidia kundi hilo, kupata vifaa hivyo visaidizi bila ya malipo.

Pia, aliahidi kuondoa ushuru kwa wafanyabiashara wanaouza visaidizi vya watu wenye ulemavu ili bei ya visaidizi hivyo ishuke.

Alisema serikali itahakikisha kuwa, kwa kiwango kikubwa, vifaa hivyo vinatolewa kwa watu wenye ulemavu bila malipo yoyote.

Previous Post

DK. SAMIA AMLILIA ODINGA

Next Post

STEVEN WASIRA: TAIFA HILI HALIJAWAHI KUGAWANYIKA

Next Post
STEVEN WASIRA: TAIFA HILI HALIJAWAHI KUGAWANYIKA

STEVEN WASIRA: TAIFA HILI HALIJAWAHI KUGAWANYIKA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

CCM YAWAPONGEZA WANANCHI, YALAANI VITENDO VYA UVUNJIFU WA AMANI

CCM YAWAPONGEZA WANANCHI, YALAANI VITENDO VYA UVUNJIFU WA AMANI

1 week ago
DK. SAMIA : TUNATAKA USHINDI WA HESHIMA

DK. SAMIA : TUNATAKA USHINDI WA HESHIMA

2 months ago

Popular News

  • DK. MWIGULU ATUMA SALAMU KWA WALA RUSHWA, WAZEMBE

    DK. MWIGULU ATUMA SALAMU KWA WALA RUSHWA, WAZEMBE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NYOTA TAIFA STARS  MZUKA UMEPANDA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RONALDO KUTUNDIKA DALUGA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JINA LA WAZIRI MKUU MTEULE KUWASILISHWA BUNGENI LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWAKINYO KUPANDA ULINGONI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.