• ePaper
Wednesday, April 29, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

KAULI UN YAWAKOSHA MABALOZI, WAHADHIRI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 16, 2025
in Habari, Kimataifa, Kitaifa
0
KAULI UN YAWAKOSHA MABALOZI, WAHADHIRI
0
SHARES
9
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

ATHNATH MKIRAMWENI
NA ELIZABETH JOHN

MABALOZI na wanadiplomasia, wamesema hatua ya Umoja wa Mataifa (UN), kuitaja Tanzania kuwa rejea ya amani Afrika na duniani, ni uthibitisho kwamba inakubalika kimataifa.

Juzi, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Antonio Guterres, alisema Tanzania imekuwa rejea muhimu ya amani na mshikamano wa kijamii barani Afrika na duniani kote.

Guterres alisema hayo, baada ya kupokea ujumbe wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, uliowasilishwa kwake na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo.

BALOZI POSI

Akizungumza na UHURU, Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania Ofisi za Umoja wa Mataifa Geneva, Uswisi, Balozi, Dk. Abdallah Possi, alisema hatua ya Rais Samia kutuma ujumbe maalumu kwa Katibu Mkuu wa UN, ni ishara ya kuendeleza ushirikiano wa muda mrefu kati ya pande hizo mbili.

Alisema muda mrefu, Tanzania imejijengea jina katika jumuiya ya kimataifa kuwa taifa la amani, lenye misingi imara ya maridhiano na mshikamano wa kitaifa.

“Nchi imekuwa ikiaminiwa kushiriki katika operesheni mbalimbali za kulinda amani chini ya Umoja wa Mataifa, hali iliyoipa heshima na uaminifu mkubwa duniani

“Ujumbe uliowasilishwa, umejikita katika masuala muhimu ya haki za binadamu na amani,”alisema.

Alisema Tanzania kama baadhi ya mataifa mengine, imewahi kupitia vipindi vigumu katika historia yake, lakini imekuwa ikijifunza na kuimarika kutokana na misingi yake ya amani.

Dk. Possi, alisema kitendo cha kuundwa Tume ya Uchunguzi kuchunguza vurugu za Oktoba 29, mwaka huu ni hatua muhimu ya kujenga imani kwa wananchi na jumuiya ya kimataifa.

Pia, alisema Tanzania imeendelea kushiriki kikamilifu katika Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa.

Alisema serikali imeendelea kufanya mazungumzo na wadau wa kimataifa, wakiwemo wawakilishi wa nchi mbalimbali na taasisi za kiraia, kujenga maelewano na uelewa wa pamoja.

Alieleza kuwa, kauli ya Guterres, inathibitisha dhamira ya Tanzania kuendelea kujenga taifa la amani, lenye mshikamano na heshima kwa jumuiya ya kimataifa.

BALOZI MULAMULA

Kwa upande wake, Mjumbe Maalumu wa Umoja wa Afrika, kuhusu Wanawake, Amani na Usalama, Balozi Liberatha Mulamula, alipongeza hatua ya Rais Samia kutuma ujumbe kwa Katibu Mkuu wa UN.

Alisema anaamini maudhui ya ujumbe huo, yalikuwa kumhakikishia Katibu Mkuu wa UN, Tanzania ni salama.

Alieleza kuwa, Guterres alitambua umuhimu wa Tanzania kama nchi ya amani na mfano wa kuigwa.

BALOZI MSTAAFU LIUNDI

Balozi Mstaafu, Christopher Liundi, alisema kauli iliyotolewa na Katibu Mkuu wa UN ni mtazamo rasmi wa jumuiya hiyo.

Alisema kauli ya Guterres, inaakisi picha halisi ya juhudi zinazofanywa na Tanzania, ambazo zinaendelea kuimarika na kuonesha dhamira ya taifa linalopenda amani.

Aliendelea kusema Tanzania ina utamaduni wa kukaa pamoja, kusikilizana na kufikia mwafaka katika masuala mbalimbali, hatua inayothibitisha misingi ya amani ipo imara na inaendelea kuimarishwa.

MHADHIRI DANINGA

Naye Mhadhiri Mwandamizi wa Uchumi na Uongozi wa Chuo cha Mwalimu Nyerere, Dk. Philip Daninga, alisema Tanznia ni nchi iliyozungukwa na upendo, ndiyo maana amani haiwezi kuvurugika.

MHADHIRI AMANI

Mhadhiri wa Masuala ya Diplomasia kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Godwin Amani, alisema utambulisho wa Tanzania katika mataifa mengine duniani, unatokana na amani na mshikamano.

BALOZI HAJI

Kaimu Mwakilishi wa Kudumu Tanzania, Umoja wa Mataifa, Balozi Dk. Suleiman Haji Suleiman, alisema Tanzania na Umoja wa Mataifa, zimezidi kuimarisha uhusiano kufuatia kikao maalumu kati ya ujumbe wa Tanzania na Katibu Mkuu wa UN.

Dk. Suleimani, alisema anaamini Guterres  amevutiwa na Tanzania kwa kuwa, inatambulika kimataifa kupitia amani pia, alifurahishwa na taarifa kuwa, hali ya utulivu imerejea nchini baada ya kutokea tukio la Oktoba 29, mwaka huu.

Dk. Suleimani, alisema Guterres alisifu uamuzi wa Rais Samia kuunda Tume ya Uchunguzi chini ya Jaji Othman Chande, ambaye anaheshimika kimataifa na ndani ya Umoja wa Mataifa.

Taarifa iliyotolewa juzi na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikino wa Afrika Mashariki, ilisema taswira ya Tanzania ni kielelezo cha amani.

Previous Post

OUNAHI TEGEMEO MOROCCO AFCON 2025

Next Post

DK. NCHIMBI ATOA AGIZO KWA PROF. MKENDA

Next Post
DK. NCHIMBI ATOA AGIZO KWA PROF. MKENDA

DK. NCHIMBI ATOA AGIZO KWA PROF. MKENDA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SIMANZI WATOTO WAKIFIA NDANI YA SWIMMING POOL

SIMANZI WATOTO WAKIFIA NDANI YA SWIMMING POOL

4 months ago
DK. MWIGULU HAPOI

DK. MWIGULU HAPOI

4 months ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?