• ePaper
Wednesday, April 29, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 28, 2026
in Habari, Kitaifa
0
TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

TANZANIA imeendelea kujinadi Kimataifa kwa kuwasilisha mafanikio yake katika Matumizi ya Nishati safi ya kupikia, ambapo hadi kufikia mwaka 2025, asilimia 28.6 ya Wananchi wana nishati safi ya kupikia, hatua inayoonesha ongezeko kubwa la matumizi hayo nchini.

Mafanikio hayo yameelezwa na Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu (Wizara ya Nishati) , Mhandisi Innocent Luoga katika Mkutano wa 5 wa mwaka wa Kamati Maalum ya Wataalamu ya Umoja wa Afrika kuhusu Nishati na Uchukuzi unaoendelea jijini Johannesburg, Afrika Kusini leo tarehe Aprili 28, 2026.

Kamishna Luoga amesema hatua hiyo imechangiwa na juhudi za makusudi za Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia ndani na nje ya nchi.

Ameeleza kuwa pamoja na mafanikio hayo, Serikali imezindua Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia wa mwaka 2024 hadi 2034 unaolenga kufikisha asilimia 80 ya Watanzania kutumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034, huku utekelezaji wake ukijikita katika kampeni za uhamasishaji zinazolenga kuwafikia wananchi hadi ngazi ya vijiji.

Aidha, Serikali inaendelea kutoa ruzuku katika mitungi na majiko banifu ili kupunguza gharama kwa wananchi, sambamba na kuhamasisha taasisi za umma na binafsi zinazohudumia watu zaidi ya 100 kwa siku kutumia nishati safi ya kupikia, ikiwemo gesi, mkaa mbadala, biogesi, na umeme.

Hatua hizo zimepokelewa vyema na nchi wanachama wa Umoja wa Afrika ambazo zimeipongeza Tanzania kwa jitihada zake katika kuendeleza matumizi ya nishati safi ya kupikia na kuwa kinara wa agenda hiyo, hatua inayochangia kulinda mazingira, afya za wananchi na kukuza maendeleo endelevu barani Afrika.

Previous Post

VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

TAHADHARI MAFUA MAKALI, UVIKO – 19

TAHADHARI MAFUA MAKALI, UVIKO – 19

2 months ago
WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA KUANZA MASOMO KWA MKUPUO

WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA KUANZA MASOMO KWA MKUPUO

5 months ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?