• ePaper
Wednesday, September 9, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

GAMONDI ALIA NA MUUNGANIKO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 8, 2025
in Habari, Kitaifa, Michezo
0
GAMONDI ALIA NA MUUNGANIKO
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

LICHA ya kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Polisi ya Kenya katika Kombe la Kagame, Kocha wa Singida Black Stars, Miguel Gamondi, amesema bado kikosi chake hakina muunganiko mzuri.

Singida ilipata ushindi huo katika mchezo wake wa pili wa michuano hiyo uliopigwa katika Uwanja wa KMC jijini Dar es Salaam.

Awali, miamba hiyo ilitoka suluhu ilipovaana na Ethiopia Coffee ya nchini Ethiopia.

Gamondi alisema kutokana na muda mfupi aliokuwa nao tangu ajiunge na timu hiyo, wachezaji bado hawajafikia muunganiko anaoutaka.

Kocha huyo alikiri kwamba kuna wakati wanashindwa kudhibiti mchezo kutokana na wachezaji wake kutozoeana vya kutosha, jambo linalosababisha makosa ya mara kwa mara uwanjani.

“Tumepata ushindi lakini sijapata muunganiko ndani ya kikosi changu, nitaendelea kupambana kuijenga timu iweze kuwa vile ambavyo ninahitaji,” alisema.

Kocha huyo alisema kwamba kadri siku zinavyosonga na wachezaji wakipata mechi zaidi za ushindani, changamoto hizo zitapungua na timu itaonekana bora zaidi.

Wakati huo huo, Gamondi alisema katika mechi mbili zilizopita za mashindano ya Kagame, alikosa huduma za wachezaji wake muhimu akiwemo Khalid Aucho na Marouf Tchakei.

Wachezaji hao kwa mujibu wake wana mchango mkubwa katika kuongeza nguvu na ubora wa kikosi hicho na kurejea kwao kutakuwa na maana kubwa katika malengo ya timu.

Naye kocha wa Polisi Ettiene Ndayiragije alikiri kwamba kuna wakati wanashindwa kudhibiti mchezo kutokana na wachezaji wake kutozoeana vya kutosha, jambo linalosababisha makosa ya mara kwa mara uwanjani.

Alisema kadri siku zinavyosonga na wachezaji wakipata mechi zaidi za ushindani, changamoto hizo zitapungua na timu itaonekana bora zaidi.

“Kikosi changu kimeleta somo baada ya kupoteza mchezo huo hivyo tunakwenda kujipanga upya tupate ushindi katika mchezo unaofuata,” alisema.

Ndayiragije alisema wapinzani wao ni timu yenye uzoefu mkubwa na waliweza kudhibiti mchezo hata walipokuwa chini ya presha.

Previous Post

MBAPPE AMFIKIA HENRY UFARANSA

Next Post

CHAMA MENO NJE SINGIDA BLACK STARS

Next Post
CHAMA MENO NJE SINGIDA BLACK STARS

CHAMA MENO NJE SINGIDA BLACK STARS

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

NI SIKU 100 ZA MAFANIKIO YA UTOAJI TIBA BORA JKCI

NI SIKU 100 ZA MAFANIKIO YA UTOAJI TIBA BORA JKCI

7 months ago
BILIONI 30/- KUJENGA UWANJA WA KISASA SIMBA

BILIONI 30/- KUJENGA UWANJA WA KISASA SIMBA

1 month ago

Popular News

  • RAIS DK. SAMIA, NDEJEMBI TURUFU YA MAENDELEO KWA WATANZANIA

    RAIS DK. SAMIA, NDEJEMBI TURUFU YA MAENDELEO KWA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI AONYA, ATOA SIKU 60 WENYE SILAHA HARAMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NDEJEMBI MZIGONI RASMI, AKEMEA KAZI KWA MAZOEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUME MIPANGO, NIRC WAJADILI UBORA MIRADI YA UMWAGILIAJI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MASAUNI AANIKA UMAHIRI WA TANZANIA INAVYOLINDA UDONGO, MATUMIZI MBOLEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?