• ePaper
Saturday, May 2, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

TFF. BMT WANOGESHA SAFARI MASHABIKI AFCON

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 13, 2025
in Burudani, Michezo
0
TFF. BMT WANOGESHA SAFARI MASHABIKI AFCON

MASHABIKI Stars

0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania ( TFF), kwa kushirikiana na Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na Wakala wa Usafirishaji (Blueberry Travels) wameandaa mchakato wa kurahisisha usafiri wa mashabiki ambao watakwenda nchini Morocco kuiunga mkono Taifa Stars, katika mashindano ya Kombe la ataifa ya Afrika (AFCON 2025).

Fainali hizo zinatarajiwa kuanza kufanyika Desemba 21 hadi Januari 18, mwaka huu nchini Morocco ambapo Taifa Stars imepangwa kundi C ikiwa na timu za Uganda, Nigeria na Tunisia.

Stars ambayo ipo nchini Misri kwa ajili ya kambi ya maandalizi ya mashindano ya hayo, itaanza kucheza mchezo wake wa kwanza dhidi ya Nigeria, unatarajiwa kufanyika Desemba 23, mwaka huu.

Akizungumza Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Maendeleo ya Michezo wa BMT, Benson Chacha alisema mchakato huo, umefanyika baada ya kupokea barua na simu nyingi kutoka kwa mashabiki wakitaka kufahamu jinsi ambavyo watasafiri ili kuisapoti timu yao.

“Sisi BMT pamoja na TFF tumekuwa tukipokea barua na simu nyingi kutoka kwa mashabiki wakitaka kufahamu jinsi ya kusafiri kwa pamoja, tumefanya mchakato na kutafuta kampuni ya Blueberry ambayo itarahisisha mashabiki wengi kwenda Morocco kuishangilia Stars,” alisema Chacha.

Kwa upande wake Ofisa Masoko Blueberry Travel, Kelvin Charles alisema kuwa anaishukuru BMT na TFF kuwapa nafasi ya kuwapeleka Watanzania nchini Morocco kwa ajili ya kuishangilia Taifa Stars.

Alisema wameandaa vifurushi rafiki kwa kuangalia vipato vya Watanzania ambapo vitawasaidia kwenda na kurudi ikiwemo malazi na usafiri wa ndani wakiwa nchini humo.

“Kifurushi cha mchezo wa kwanza kati ya Tanzania dhidi ya Nigeria kwa mtu mmoja atalipa dola 2,535, wakati kwa watu wawili watalipa dola 2,320, kifurushi kingine ni ule mchezo wa Desemba 27 utakaoikutanisha Tanzania na Uganda mtu mmoja atalipa dola 2,970 wakiwa wawili watalipa dola 2,700.

“Pia mchezo wa Desemba 30, mwaka huu wa Stars dhidi ya Tunisia, mtu mmoja atalipa dola 3,000 kwa wawili ni dola 2,780 huku kwa upande kifurushi cha wale ambao wanataka kuangalia michezo yote watalipa dola 4,400 mtu mmoja itakuwa dola 5,250,” alisema Charles.

Ofisa Habari wa TFF, Cliford  Ndimbo alisema kikosi hicho kinaendelea vizuri na maandalizi kuhakikisha kinafanya vizuri katika mashindano hayo.

Alisema kila mchezaji yupo vizuri huku wale waliokuwa nje ya nchi wakiendelea kuripoti kambini kujiunga na wenzao.

“Timu yetu inaendelea vizuri malengo kufanya vyema katika michuano ya AFCON msimu huu,” alisema Ndimbo.

Previous Post

‘MSAUZI’, MHISPANIA WACHUANA UKOCHA SIMBA

Next Post

NADO, MASAGALA WATOA NENO STARS

Next Post
NADO, MASAGALA WATOA NENO STARS

NADO, MASAGALA WATOA NENO STARS

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. NCHIMBI : CCM INAJIVUNIA MTAJI MKUBWA WA WANACHAMA

DK. NCHIMBI : CCM INAJIVUNIA MTAJI MKUBWA WA WANACHAMA

8 months ago
DK. SAMIA AFUNDA VIJANA

DK. SAMIA AFUNDA VIJANA

6 months ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?