• ePaper
Sunday, May 31, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

HAPATOSHI ‘KNOCKOUT YA MAMA’ KIJITONYAMA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 31, 2025
in Burudani, Kitaifa, Michezo
0
HAPATOSHI ‘KNOCKOUT YA MAMA’ KIJITONYAMA
0
SHARES
12
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na AMINA KASHEBA

BONDIA wa ngumi za kulipwa, Mtanzania Frank Shagembe, leo atapanda ulingoni kuzichapa na Mghana Haruna Osumanu katika pambano la mkanda wa WBO Afrika uzito wa juu mwepesi.

Pambano hilo la raundi 10 litafanyika katika viwanja vya Posta vilivyopo Kijitonyama, Dar es Salaam.

Kabla ya pambano hilo, mabondia mbalimbali Watanzania watapanda ulingoni kuzichapa na wanamasumbwi kutoka ndani na nje ya nchi.

Akizungumza Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Kampuni ya Mafia Boxing Promotions ambayo ndiyo mwandaaji wa mtanange huo, Ally Zayumba, alisema maandalizi yamekamilika na kila bondia amejipanga kuonyesha kiwango kikubwa.

“Kutakuwa na mapambano 14 ndani yake, kutakuwa na mikanda saba ambayo itapiganiwa na mabondia kutoka Tanzania na wapinzani wao kutoka nje ya nchi, nina imani kutakuwa na mambo mazuri.

“Pambano kuu atacheza Frank Shagembe dhidi ya Osumanu kutoka Ghana ambao watagombania mkanda wa WBO Afrika,” alisema.

Zayumba pia alisema Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBRC), itatumia jukwaa hilo kutambulisha mikanda mipya ya ubingwa wa taifa katika masumbwi ya kulipwa.

Bondia Shagembe alisema amejiandaa vyema kuonyesha kiasi gani anahitaji kuweka historia katika masumbwi nchini licha ya mpinzani wake kuwa na rekodi nzuri.

“Ninapanda ulingoni kuzichapa na bondia mahiri mwenye rekodi kubwa, nitahakikisha mkanda wa ubingwa wa WBO Afrika unabaki nyumbani kwani nimejipanga kushinda,” alisema.

Previous Post

UNDANI WA REKODI YA MSUVA AFCON

Next Post

KISA MABAO 1,000, RONALDO AGOMA KUTUNDIKA DARUGA

Next Post
KISA MABAO 1,000, RONALDO AGOMA KUTUNDIKA DARUGA

KISA MABAO 1,000, RONALDO AGOMA KUTUNDIKA DARUGA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

TANZANIA YASISITIZA KUTUMIA AKILI UNDE KUKABILI MAAFA

TANZANIA YASISITIZA KUTUMIA AKILI UNDE KUKABILI MAAFA

3 weeks ago
TAIFA STARS KUTUA MOROCCO KWA KISHINDO

TAIFA STARS KUTUA MOROCCO KWA KISHINDO

6 months ago

Popular News

  • SERENGETI BOYS KILA KONA, RAIS SAMIA AWAPA MILIONI 500/-

    SERENGETI BOYS KILA KONA, RAIS SAMIA AWAPA MILIONI 500/-

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAS: UTUNZAJI MAZINGIRA AJENDA YA KIPAUMBELE KWA MKOA WA MWANZA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • UPELE UMEPATA MKUNAJI STARS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ‎ RAIS DK. SAMIA: POLISI MSIDHARAU TAARIFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWIGULU ATETA NA WAZIRI MKUU WA CONGO BRAZZAVILLE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?