• ePaper
Wednesday, March 18, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

MWISHO WA ENZI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
February 28, 2026
in Habari, Kitaifa
0
MWISHO WA ENZI
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

NA WAANDISHI WETU

ASKOFU Mkuu Mstaafu wa Kanisa Katoliki,  Jimbo Kuu la Dar es Salaam, marehemu Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, anatarajiwa kuzikwa leo katika Kituo cha Hija Pugu, Dar es Salaam, huku kanisa hilo likitaja sifa 13 za zilizomtambulisha na kumkumbuka. 

Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, aliungana na mamia ya waombolezaji na viongozi wa kitaifa  kuuaga mwili wa Kardinali Pengo, tukio lililofanyika katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu, Dar es Salaam.

Kardinali Pengo alifariki dunia Februari 19 mwaka huu, katika  Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu ya maradhi ya moyo na mgongo.

Akizungumza jana katika ibada ya kuaga mwili wa Kardinali Pengo,  Askofu Msaidizi Jimbo Kuu Dar es Salaam,  Henry Mchamungu,  alizitaja sifa 13 ambazo Kardinali Pengo atakumbukuwa kuwa ni  kuwa na moyo wa ibada, sala na unyenyekevu.

Alisema sifa ya pili ya marehemu Kardinali Pengo, kupenda   kuishi maisha ya ufukara  kwa sababu hakupenda kujilimbikizia mali.

“Aliishi maisha ya kifukara, hakupenda kabisa kujilimbikizia mali maana kila alichokipata alikitoa kwa kanisa, kwa mfano baada ya kustaafu alichopewa kama zawadi alikitoa mara moja kwa miradi ya kanisa,” alisema. 

Askofu Mchamungu alitaja sifa ya tatu ya marehemu Kardinali Pengo ni  kujinasua  na mambo ya ulimwengu, kwani  hakuwa na akaunti binafsi, wala hakuwahi kumuona na  simu.

“Alitoa nguvu yake katika sala na alijinasua na mambo ya ulimwengu huu, tulisikia alitoa mali zake zote hakuwa na mali binafsi, hakuwa na akaunti binafsi, simu sikuwahi kumuona nayo, sikuwahi kumpigia nilikuwa nampata kupitia simu za wasaidizi,” alisema. 

Alisema  sifa ya nne ya marehemu Kardinali Pengo ni nidhamu binafsi ya pekee hasa katika kusali, kuheshimu muda na kufanya kazi kwa bidii.

Askofu Mchamungu alieleza  sifa  ya tano ni  kujiepusha  na upendeleo, kwa sababu alipenda kusimamia ukweli, haki, amani na maadili.

Alisema sifa ya sita alipenda watoto, aliendeleza kituo cha Hija Pugu na sifa ya saba alisimama katika imani ambayo haikutetereka na iliendelea kukua.

 Alisema sifa ya nane alikuwa mkweli anayezungumza kwa upendo.

CHANZO CHA KIFO

Askofu Mchamungu alisema Kardinali Pengo alipata maradhi ya mgongo na moyo yaliyomsumbua kwa muda mrefu, ambapo alipata matibabu nchini, Ujerumani, Marekani na India.

Alisema matatizo ya kiafya yaliongezeka na kugundulika zaidi kuanzia Novemba mwaka jana, ambapo alianza matibabu  nchini  Desemba 27 mwaka jana alipelekwa  India.

Alisema alifariki dunia Februari 19 saa nne usiku kwa maradhi ya moyo ikiwa ni muda mfupi baada ya kutoka India.

WASIFU WA KARDINALI PENGO

Askofu Mchamungu alisema,  Kardinali Pengo alizaliwa Agosti 5 mwaka 1944, kijiji cha Mwaziya, Wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa, akiwa ni mtoto wa sita kati ya tisa.

Alibatizwa Agosti 6 mwaka 1944, alipata komunio ya kwanza Juni 20, 1952, sakramenti ya kipaimara  Agosti 15, 1952 huko Parokia ya Mwaziya.

Alisema, Kardinali Pengo alisoma elimu ya msingi katika shule mbili tofauti  za Mwaziya -Mpito na Kalema  kuanzia mwaka 1953 hadi 1958.

Aliongeza kuwa, katika kipindi cha mwaka 1959 hadi 1964 alijiunga na seminari ya Mtakatifu Yosefu iliyopo Sumbawanga.

MASOMO YA UPADRI

Askofu Mchamungu  alisema 1965 hadi 1971, alisoma masomo ya falsafa na theolojia katika Seminari Kuu ya Mtakatifu Paulo Kipalapala mkoani Tabora.

Kwa mujibu wa Askofu Mchamungu, Kardinali Pengo alipewa daraja takatifu la ushemasi, Desemba  9, 1970 na Juni 20, 1971 alipewa daraja takatifu la upadri.

Previous Post

DK. NCHIMBI : KUMBUKIZI ZA MAJIMAJI ZIWE CHACHU YA UZALENDO NA UWAJIBIKAJI

Next Post

YANGA, SIMBA TAMBO TUPU

Next Post
YANGA, SIMBA TAMBO TUPU

YANGA, SIMBA TAMBO TUPU

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

TAIFA STARS KATIKA AFCON YA NDOTO

TAIFA STARS KATIKA AFCON YA NDOTO

3 months ago
Wachezaji wa SIMBA na YANGA

YANGA, SIMBA MECHI YA KISASI NA HESHIMA

7 months ago

Popular News

  • MANDONGA AJA KIVINGINE

    MANDONGA AJA KIVINGINE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YATUMIA BILIONI 64/- KUBORESHA UWANJA WA NDEGE IRINGA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU AWAWEKA MTEGONI VIGOGO WILAYA, HALMASHAURI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ALAMA TATU KUMUENZI JPM

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI KUIFANYA TANZANIA KITOVU CHA BIASHARA – DK. YONAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?