• ePaper
Sunday, March 8, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

YANGA, SIMBA TAMBO TUPU

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
February 28, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
YANGA, SIMBA TAMBO TUPU
0
SHARES
8
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

WAKATI joto la pambano watani wa jadi, Yanga na Simba likizidi kupanda, makocha wa timu hizo wametambiana huku kila mmoja akisisitiza kuibuka na ushindi kutokana na ubora wa kikosi chake.

Yanga na Simba zinatarajiwa kushuka dimbani kesho katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaochezwa Uwanja wa New Amaan, Complex, visiwani Zanzibar.

Yanga itaingia katika mchezo huo ikiwa na kumbukumbu ya kushinda mabao 5-0 mbele ya JKT Tanzania huku Simba ikitoka suluhu dhidi ya Dodoma Jiji.

Pia Yanga itaingia uwanjani ikiwa na kumbukumbu nzuri ya kuifunga Simba mechi sita mfululizo za mashindano tofauti.

Mara ya mwisho Simba kuifunga Yanga ilikuwa katika Ngao ya Jamii iliyochezwa Agosti 13, 2023 kwa mikwaju ya penalti 3-1, baada ya hapo, Yanga imetembeza vipigo vinne katika Ligi na Ngao ya Jamii mara mbili.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana Kocha wa Yanga, Pedro Goncalves, alisema kuwa kila mchezo kwake ni kama fainali, hivyo hatokubali kuona wanapoteza kwani wanahitaji pointi tatu muhimu na kuendelea kujikita kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Alisema kuwa ni mechi nzuri dhidi ya Simba na kila mmoja anaisubiria kwa muda mrefu, lakini wao wamepata motisha kueleka mchezo huo kutokana na ushindi wa mabao 5-0 waliyopata dhidi ya JKT Tanzania.

“Kilichopo ni kufikiria namna ya kiwango cha timu, mpaka hivi sasa tunaendelea vizuri na maandalizi hata mabeki wetu wanajipanga vizuri kuzuia mashambulizi, ninafurahi sana kwani ninaamini tutaibuka na ushindi.

“Tangu nilipofika hapa visiwani Zanzibar, mashabiki wetu wamekuwa wakituunga mkono kila wakati na hata tunapotoka nje ya Dar es Salaam, tunapata ushirikiano wa kutosha.

“Tunawaomba mashabiki wajitokeze kwa wingi kuhakikisha wanatupa sapoti ya kutosha ili tuweze kuwapa burudani ya aina yake,” alisema.

Hata hivvyo kocha huyo alisema kuwa hana hofu na wachezaji wake kwani wanaendelea kufanya marekebisho katika mapugufu yaliojitokeza katika mechi za awali ili kufanya vizuri zaidi katika mchezo huo.

Kwa upande wa Kocha wa Simba, Steve Barker alisema walikuwa wanahitaji kupata ushindi dhidi ya Dodoma Jiji lakini haikuwezekana, hivyo watapambana kuhakikisha wanapata ushindi katika mchezo huo.

Barker alisema kuwa hana hofu na kikosi alichokuwa nacho kwani kila mchezaji yupo vizuri na anamorari ya kutosha kuelekea katika mchezo huo muhimu.

Alisema kuwa anajua utakuwa mchezo mgumu na wenye changamoto kubwa huku ukifuatiliwa na mashabiki lukuki, watapambana kuhakikisha wanapata ushindi wa kishindo.

Alisisitiza wamejipanga kupata matokeo mazuri na kuendelea kusogea nafasi za juu katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

“Kila mechi ina presha yake, tumejipanga kufanya vyema baada ya kuboresha kikosi chetu kutokana na mapungufu tuliyoyaona katika mchezo uliopita dhidi ya Dodoma Jiji.

“Tunahitaji kushinda mechi iliyopo mbele yetu kuhakikisha tunaendelea kujiweka katika mazingira mazuri ya kusogea juu ya msimamo.

“Itakuwa mechi ngumu, Yanga ina timu nzuri na sisi pia tuna timu nzuri, ni mechi kubwa hapa nchini na Afrika kwa ujumla, matumaini yetu ni kwamba mashabiki watafurahia burudani tutakayoitoa tukiwa uwanjani,” alisema.

WAAMUZI HADHARANI

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), jana lilitangaza waamuzi wa mchezo huo ambapo mwamuzi wa kati atakuwa ni Nassoro Mwinchui kutoka Tanga, akisaidiana na Kassim Mpanga wa Dar es Salaam, Hamdan Said wa Mtwara na Ramadhani Kayoko wa  Dar es Salaam.

REKODI ZA TIMU HIZO ZIPO HIVI

Rekodi zinaonyesha, Yanga imeifunga Simba mara sita mfululizo katika mashindano tofauti timu hizo zilipokutana Ligi Kuu Bara mechi nne na Ngao ya Jamii mara mbili.

Mara ya mwisho Simba kuifunga Yanga ilikuwa katika Ngao ya Jamii iliyochezwa Agosti 13, 2023 kwa penalti 3-1.

Baada ya hapo, matokeo ya Ligi Kuu Bara yalikuwa Simba 1-5 Yanga (Novemba 5, 2023), Yanga 2-1 Simba (Aprili 20, 2024), Simba 0-1 Yanga (Oktoba 19, 2024) na Yanga 2-0 Simba (Juni 25, 2025).

Pia mechi mbili za Ngao ya Jamii Yanga 1-0 Simba na Yanga 1-0 Simba.

Previous Post

MWISHO WA ENZI

Next Post

IMEISHA HIYO

Next Post
IMEISHA HIYO

IMEISHA HIYO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA BARABARA ZA NDANI KWA KIWANGO CHA LAMI PANGAWE

DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA BARABARA ZA NDANI KWA KIWANGO CHA LAMI PANGAWE

5 months ago
TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

TANZANIA YAIHAKIKISHIA DUNIA HALI YA UTALII IKO SALAMA

4 months ago

Popular News

  • SALOME AIBANA KAMPUNI YA DONGFANG KWA KASI ISIYORIDHISHA MRADI WA UMEME MALAGARASI

    SALOME AIBANA KAMPUNI YA DONGFANG KWA KASI ISIYORIDHISHA MRADI WA UMEME MALAGARASI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MASAUNI AZINDUA BODI YA KABONI, AIPA MAAGIZO MATANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • FCC, TCRA KUCHUNGUZA GHARAMA ZA BANDO NCHINI 

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA AIPA HESHIMA DIPLOMASIA YA TANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ULINZI, USALAMA KUIMARISHWA AFCON

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?