• ePaper
Tuesday, April 21, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

YANGA, SIMBA MECHI YA KISASI NA HESHIMA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
August 30, 2025
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
Wachezaji wa SIMBA na YANGA
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

NI wiki mbili pekee zimesalia kabla ya kushuhudia mtanange kati ya watani wa jadi, Simba na Yanga katika mchezo wa Ngao ya Jamii kuashiria kufungua msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara, huku kila moja ikitamba mechi itakuwa ya kisasi na rekodi.

Simba na Yanga zinatarajiwa kushuka dimbani katika mchezo wa Ngao ya Jamii utakaochezwa Septemba 16, mwaka huu katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.,

Yanga imeifunga Simba mara tano mfululizo, mara nne katika mechi za Ligi Kuu kwa misimu miwili mfululizo na mchezo mmoja wa nusu fainali ya Ngao ya Jamii uliochezwa, Agosti 8, mwaka jana.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti viongozi wa timu hizo, kila mmoja alitamba kufanya vyema kutokana na maandalizi aliyoyafanya.

Kocha wa Simba, Fadlu Davids, amesema kuwa anajua mchezo utakuwa mgumu na wenye changamoto nyingi lakini anahitaji kuibuka kidedea na kulipa kisasi.

Amesema wamekuwa wakipoteza dhidi ya wapinzani wao mara kwa mara, hivyo hawataingia kinyonge kwani wanataka ushindi kwa namna yoyote.

Fadlu amesema ana imani na kikosi chake kuwa kitafanya vizuri na kulipa kisasi kwani hataki kuona timu yake inaendelea kufungwa na wapinzani wao.

“Ni mchezo mgumu kwetu na wenye ushindani mkubwa lakini safari hii hatutakubali kupoteza, tunahitaji kupata ushindi na kulipa kisasi, tunahitaji kushinda na kubeba taji hilo,” alisema Fadlu.

Naye Meneja wa kikosi cha Yanga, Walter Harrson alisema kuwa Kocha wao Romain Folz anaendelea kufanya kazi kubwa kuhakikisha timu inapata ushindi na kuendeleza rekodi walizoweka awali.

Amesema kuwa msimu huu hawataki masihara wanahitaji kubeba mataji yote wakianza na Ngao ya Jamii kwa kumfunga Simba.

“Furaha yetu sisi ni kuendeleza rekodi ambayo tumeiweka kwa kumfunga Simba kila tunapokutana naye, mwalimu anaendelea na mipango na ameshawasoma Simba, hivyo tuna imani ataingia na mbinu mbadala ili kuweza kupata ushindi,” amesema Walter.

Meneja huyo amesema kuwa timu yao inaendelea na maandalizi yake kuelekea katika mchezo huo muhimu wakiwa katika kambi yao ya Avic Town jijini Dar es Salaam.

Amesema anajua mchezo utakuwa mgumu na wenye upinzani, lakini wana imani ya kupata ushindi na kuendelea kuwapa burudani mashabiki wao.


Msimu uliopita, Yanga ilitwaa Ngao ya Jamii kwa kuichakaza Azam, mabao 4-1 yaliyofungwa na Prince Dube, Yoro Diaby aliyejifunga, Stephane Aziz Ki na Clement Mzize, huku bao la Azam likiwekwa kimiani na Feisal Salum ‘Fei Toto’ mechi ilipigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Previous Post

GAVU ATAJA SIFA ZA NAFASI URAIS, UBUNGE, UDIWANI

Next Post

IBENGE ATAMBIA KIKOSI

Next Post
IBENGE ATAMBIA KIKOSI

IBENGE ATAMBIA KIKOSI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. NCHIMBI KUONGOZA KUAGWA JENISTA MHAGAMA

DK. NCHIMBI KUONGOZA KUAGWA JENISTA MHAGAMA

4 months ago
NEEMA LUKUKI BANDARI KILWA

NEEMA LUKUKI BANDARI KILWA

4 months ago

Popular News

  • MUDATHIR KUIKOSA SIMBA

    MUDATHIR KUIKOSA SIMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ‘MISS WORLD’ KUIPAISHA TANZANIA DUNIANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • BIL. 195.66/- KUJENGA BONDE MTO MSIMBAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ULEGA AJIBU MAPIGO KUHUSU MTANDAO WA BARABARA NCHINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NEEMA YAJA, MIKAKATI HADHARANI KUINUA VIJANA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?