• ePaper
Saturday, May 2, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

SIRI UTEUZI VIONGOZI CCM

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
March 11, 2026
in Habari, Kitaifa
0
SIRI UTEUZI VIONGOZI CCM
0
SHARES
11
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

KATIBU wa NEC Itikadi, Uenezi, na Mafunzo,  Kenani Kihongosi, amesema heshima ya CCM ni kubwa kuliko fedha na umaarufu, hivyo maamuzi ya chama juu ya wagombea hufanywa kwa kuangalia uadilifu na maadili ya mgombea husika.

Kihongosi ameeleza hayo akizungumza na wananchi wa Kata ya Nyehunge Halmashauri ya Buchosha Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza, ikiwa ni muendeleo wa ziara yake Kanda ya Ziwa.

Kihongosi ameeleza hayo akijibu hoja ya moja wa wananchi, Leonard Methusela iliyeuliza kwanini ngazi za juu za chama zinawakata wagombea ambao wamepitishwa na wajumbe na kuleta majina ya watu wanao wataka wao, hatua ambayo inawagombanisha wananchi na wagombea wao.

Akijibu hoja hiyo Kihongosi amesema majina ya wagombea yanapochujwa huanza kutoka ngazi ya chini na kuendelea hadi Halmashauri Kuu ya Taifa,lakini kuna baadhi ya vitu wakiona si sawa huwa wanawakata ili kuweka wanaofaa.

Amesema chama hakimpi mtu nafasi kwa sababu wanaamini ana nguvu ya fedha au umarufu ndani ya CCM ,hawaangalii vitu hivyo bali wanaangalia heshima ya chama, na kuongeza kuwa wakiendekeza hela, rushwa au kujuana wengi wasingepata nafasi hata yeye asingekuwa mwenezi wa chama.

“Wale wanaotoa rushwa au kujaribu kuathiri mchakato wa uteuzi hawataweza kuleta maendeleo. Heshima ya Chama Cha Mapinduzi ni kubwa kuliko mali au umaarufu wa mtu,” amesema Kihongosi.

Ameongeza; “Tukiendekeza fedha, rushwa au uhusiano binafsi, hata mimi leo nisingekuwa Mwenezi wa CCM, hii ni kwa sababu heshima na nidhamu ya chama ndiyo msingi wa uteuzi wa viongozi”.

Amesisitiza uteuzi wa viongozi ndani ya chama hicho lazima uende sambamba na heshima, uadilifu na kupinga rushwa ili kuhakikisha maendeleo endelevu kwa wananchi, lakini wamekuwa wakibaini kuna wengi wamekuwa wakipita kwa njia zisizo halali.

Previous Post

MAELFU YA WAGONJWA KUTOKA NJE YA NCHI WAMIMINIKA KUPATA HUDUMA

Next Post

DK. MWIGULU AWAVAA WANAOSUBIRI UTEUZI

Next Post
DK. MWIGULU AWAVAA WANAOSUBIRI UTEUZI

DK. MWIGULU AWAVAA WANAOSUBIRI UTEUZI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

HISTORIA ELIMU MSINGI YAANDIKWA

HISTORIA ELIMU MSINGI YAANDIKWA

3 months ago
WAZIRI MKUU AWAPA ‘TANO’ WANAOCHAPAKAZI SERIKALINI

WAZIRI MKUU AWAPA ‘TANO’ WANAOCHAPAKAZI SERIKALINI

2 months ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?