• ePaper
Saturday, May 30, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

MASTAA YANGA WAUTAJA UBINGWA LIGI KUU BARA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
May 27, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
MASTAA YANGA WAUTAJA UBINGWA LIGI KUU BARA
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na VICTOR MKUMBO

MASTAA wa klabu ya Yanga, wameibuka na kutaja kwamba ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, bado upo wazi, lakini wamejipanga kupata ushindi katika mechi tano zilizobaki ili kuchukua tena taji hilo.

Katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga ipo kileleni ikiwa na alama  60, ikifuatiwa na Simba yenye pointi 58 ambapo timu zote zimecheza mechi 25 hadi hivi sasa.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam, mastaa wa Yanga walisema kuwa kusema wao wametwaa taji hilo ni mapema kwani wana mechi tano na lolote linaweza kutokea.

Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ alisema mbio za ubingwa bado zipo wazi, lakini Yanga wana nafasi kubwa ya kutwaa taji hilo kwa mara nyingine msimu huu.

Alifafan ua kuwa anaamini hadi mwishoni mwa msimu huu watatangaza ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa mara nyingine.

Tshabalala alisisitiza kuwa Yanga imekuwa ikicheza kwa ushirikiano katika kila mechi kitu ambacho kimesababisha kupata matokeo chanya.

“Mbio za ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara bado zinaendelea na hadi muda huu, sisi tuna nafasi kubwa ya kuchukua ubingwa.

“Tunaamini hadi kufikia mwishoni mwa msimu tutatangazazwa mabingwa wa michuano hii kwa mara nyingine,” alisema Tshabalala.

Kwa upande wake, Maxi Nzengeli alisema wataendelea kuhakikisha wanashinda katika mechi zote tano zilizobaki.

Hata hivyo, mchezaji huyo amekiri kuwepo kwa ushindani mkubwa wanaoupata kutoka kwa timu pinzani.

“Mechi zilizobaki hazitakuwa rahisi kwani kila timu itapambana kupata matokeo mazuri na sisi tutahakikisha tunafanya vizuri,” alisema.

Nzengeli alisema wachezaji wote wameahidi kuendelea kupambana kuhakikisha timu inabakia katika kilele cha ligi hiyo.

“Tutaendelea kupambana kuhakikisha tunazilinda pointi mbili zilizopo japokuwa mechi tano zilizobakia hazitakuwa rahisi.

“Kila timu imekuwa ikipambana kupata matokeo mazuri, tunaendelea kuhamasishana mazoezini kuhakikisha tunafikia malengo tuliyojiwekea,” alisema Maxi.

Naye Bakari Mwamnyeto alisisitiza kwamba ligi  hiyo ni ngumu lakini wamejipanga kusikiliza  maelekezo ya benchi la ufundi na kuhamishia wanafuata ili kupata ushindi.

Pia, alisema mashabiki wamekuwa wakiwapa hamasa kwa kufika kwa wingi viwanjani, hivyo wachezaji hawana cha kuwalipa zaidi ya kuwapa furaha ya ushindi.

“Ligi ni ngumu kwa hapa ilipofikia kwani kila timu imebakisha mechi tano na kila mmoja anapambana kutaka kutimiza malengo aliyojiwekea.

“Tunawaomba mashabiki waendelee kutusapoti kwa kujitokeza kwa wingi uwanjani na kutupa hamasa zaidi kuhakikisha tunatetea ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu,” alisema Mwamnyeto.

Previous Post

RAIS DK. SAMIA AWAFUNDA MAJAJI ALIOWAAPISHA

Next Post

DK. MWIGULU ATETA NA WAZIRI MKUU WA CONGO BRAZZAVILLE

Next Post
DK. MWIGULU ATETA NA WAZIRI MKUU WA CONGO BRAZZAVILLE

DK. MWIGULU ATETA NA WAZIRI MKUU WA CONGO BRAZZAVILLE

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. NCHIMBI AELEZA DK. SAMIA  ALIVYOSIMAMIA USALAMA NCHINI

DK. NCHIMBI AELEZA DK. SAMIA  ALIVYOSIMAMIA USALAMA NCHINI

8 months ago
YANGA, AZAM FC FAINALI YA KIBABE

YANGA, AZAM FC FAINALI YA KIBABE

5 months ago

Popular News

  • RAS: UTUNZAJI MAZINGIRA AJENDA YA KIPAUMBELE KWA MKOA WA MWANZA

    RAS: UTUNZAJI MAZINGIRA AJENDA YA KIPAUMBELE KWA MKOA WA MWANZA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • UPELE UMEPATA MKUNAJI STARS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ‎ RAIS DK. SAMIA: POLISI MSIDHARAU TAARIFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWIGULU ATETA NA WAZIRI MKUU WA CONGO BRAZZAVILLE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MASTAA YANGA WAUTAJA UBINGWA LIGI KUU BARA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?