• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Burudani

KIBU DENIS, MANULA WATEMWA STARS

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 1, 2025
in Burudani, Michezo
0
KIBU DENIS, MANULA WATEMWA STARS
0
SHARES
10
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na AMINA KASHEBA

WAKATI Kocha wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Hemed Suleiman ‘Morocco’, akitangaza kikosi cha wachezaji 23, wachezaji wa Simba, Kibu Denis, Abdulrazack Hamza na kipa wa Azam FC, Aishi Manula wameachwa.

Pia, katika kikosi hicho wamo wachezaji walioitwa kwa mara ya kwanza ambao ni Antony Remy (Azam FC) na Edmund John (Yanga) huku Abdul Hamis (Azam FC) akirejeshwa kwa mara nyingine.

Akizungumza alipokuwa akitangaza kikosi hicho, Kocha Morocco amesema ameita wachezaji wenye uwezo wa kuisaidia timu kufanya vizuri katika michuano ya kufuzu kucheza Kombe la Dunia mwaka 2026.

Amesema kikosi chake kinatarajia kuingia kambini kesho kujiandaa na michezo miwili ya kuwania kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Congo Brazzavile utakaochezwa Septemba 5, mwaka huu kabla ya kuikabili Niger, Septemba 9, mwaka huu mechi zote Stars itakuwa ugenini.

“Nina imani na wachezaji niliowaita katika kikosi hiki wana kiwango bora na wanaweza kutusaidia kufanya vyema katika michuano ya kufuzu Kombe la Dunia.

“Tunatarajia kuingia kambini kujiandaa na michezo miwili ambayo tutakuwa ugenini dhidi ya Congo Brazzavile na Niger, malengo yetu ni kufanya vyema na kufikia malengo tuliyojiwekea,” alisema Kocha Morocco.

Amewataja wachezaji waliotwa katika kikosi hicho ni Yakoub Suleiman na  Wilson Nangu (JKT Tanzania), Shomari Kapombe, Yusuph Kagoma na Selemani Mwalimu (Simba), Mohamed Hussein, Mudathir Yahya, Clement Mzize, Edmund John, Ibrahim Abdullah na Dickson Job (Yanga), Lusajo Mwaikenda, Pascal Msindo, Yahya Zaid, Abdul Hamis, Feisal Salum na Iddy Selemani (Azam FC).

Wengine ni Saimon Msuva (Al-Talaba SC- Iraq), Novatus Dismas (Goztepe FC, Uturuki), Mbwana Samtta (Le Havre AC, Ufaransa), Charles M’mombwa(Florian FC, Malta) na Antony Remmy (Azam FC U-20).

Katika michuano ya kufuzu Kombe la Dunia 2026, Tanzania imepangwa kundi E na timu za Moroco, Zambia, Congo Brazaville, Niger na Eritrea.

Katika msimamo wa kundi hilo, Tanzania ipo nafasi ya tatu ikiwa na pointi sita sawa na Niger iliyopo nafasi ya pili, Morocco inaongoza kundi akiwa na pointi tisa, Zambia pointi tatu nafasi ya nne huku Congo Brazzaville na Eritrea zikiburuza mkia.

Previous Post

MAELFU WAJITOKEZA KUMSIKILIZA DK. SAMIA

Next Post

DK. SAMIA AAHIDI UWANJA WA SOKA DODOMA KUKAMILIKA MWAKA 2027

Next Post
DK. SAMIA AAHIDI UWANJA WA SOKA DODOMA KUKAMILIKA MWAKA 2027

DK. SAMIA AAHIDI UWANJA WA SOKA DODOMA KUKAMILIKA MWAKA 2027

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

JK AMWOMBEA KURA DK. SAMIA

JK AMWOMBEA KURA DK. SAMIA

1 month ago
DK. SAMIA AMETEKELEZA MIRADI MINGI YA MAENDELEO – DK. NCHIMBI

DK. SAMIA AMETEKELEZA MIRADI MINGI YA MAENDELEO – DK. NCHIMBI

1 month ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.