• ePaper
Wednesday, September 9, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

WASIRA ATABIRI RUNDO LA KURA KWA DK. SAMIA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 4, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
WASIRA ATABIRI RUNDO LA KURA KWA DK. SAMIA

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira

0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira, amesema Mgombea Urais kupitia Chama hicho katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, mwaka huu, Dk. Samia Suluhu Hassan, atapigiwa kura nyingi kwa sababu, wananchi wameiona kazi kubwa aliyoifanya kuleta maendeleo kwa miaka minne iliyopita.

Amesema Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2025-2030, imejikita kusimamia uchumi na kuhakikisha inawagusa wananchi kila sekta.

Wasira, amesema hayo jana Simanjiro mkoani Manyara, akiwa katika ziara ya kuitafutia ushindi wa kishindo CCM kupitia Dk. Samia, wagombea ubunge na udiwani.

“Ndiyo maana tunaandika Ilani, ukitazama mafanikio yaliyopatikana wala sihitaji kutumia takwimu, maana Watanzania hata wa Simanjiro wanajua mafanikio yaliyofanyika hapa, wanajua kiwango cha vituo vya afya vilivyojengwa, wanajua madarasa yaliyojengwa hapa, wanajua majosho yaliyojengwa ya wafugaji na juzi Mama Samia ametoa ruzuku ya kuchanja mifugo,” alisema.

Amesema wananchi wa Tanzania wanajua jitihada zilizofanywa na Chama huku akitolea mfano, Simanjiro kumekuwa na matatizo makubwa ya maji na yanashughulikiwa kwa kiasi kikubwa.
“Kwa hiyo, nimekuja kutoa wito kwa wananchi wa Simanjiro, kuhakikisha wapigakura wote wanatoka kwenda kupiga kura, wasisahau na wakumbuke kumpigia kura Dk. Samia Suluhu Hassan.

“Tukamilishe safu kwa mafiga matatu, halafu tukimaliza tunawatuma kusikiliza Ilani.

“Ilani katika siku zijazo, tunataka kusimamia uchumi wa watu wa Tanzania, kama ni wafugaji tunataka kuwasaidia wafugaji ili ufugaji wao uwalipe, kama ni wakulima tunataka kuwasaidia wakulima tuwape zana, tulete miradi ya umwagiliaji  walime waondokane na umaskini, kama ni wavuvi tutawapa vifaa vya kuvua na tunaka kuanzisha viwanda kulingana na malighafi inayopatikana.


“Hapa Simanjiro malighafi yake ni mifugo, kwa hiyo ukitaka kuanzisha viwanda utaanzisha vya nyama,” ameeleza.

Amesema kila wilaya itakuwa na viwanda vyake kutokana na mazao yanayozalishwa eneo husika na kwamba, hivyo ndivyo Ilani ya Uchaguzi ya CCM inavyosema shabaha ikiwa kuleta maendeleo kwa wote.

Amesisitiza kuwa, serikali inatumia fedha na gharama kubwa kwa wananchi wakiwemo wa vijijini kuhakikisha maisha yao yanazidi kuwa bora.

Hivi hapa Simanjiro ambapo vijiji vyenu vipo kilometa 70 kutoka mjini nani alijua umeme utaenea hadi ufike kijijini, lakini umefika vimebaki labda vitongoji tu. Vijiji vyote vya Tanzania vina umeme, tutaendelea kujenga vitu hivi kujenga uchumi na shabaha kubwa ni kusaidia uchumi wa mtu mmoja mmoja.


“Ndugu zangu nilitaka niyaseme hayo na kubwa kuliko yote ni kwamba, lazima tushinde uchaguzi,” ameeleza.

Previous Post

DK. NCHIMBI : SIKU 100 TUME YA MARIDHIANO ITAANZISHWA

Next Post

SERIKALI ITAIMARISHA TIBA ZA KITALII – DK. MPANGO

Next Post
SERIKALI ITAIMARISHA TIBA ZA KITALII – DK. MPANGO

SERIKALI ITAIMARISHA TIBA ZA KITALII – DK. MPANGO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

TRENI ZA JIJI DAR, DODOMA ZANUKIA

TRENI ZA JIJI DAR, DODOMA ZANUKIA

10 months ago
CCM Z’BAR YAAHIDI KAMPENI ZA KISTAARABU

CCM Z’BAR YAAHIDI KAMPENI ZA KISTAARABU

12 months ago

Popular News

  • RAIS DK. SAMIA, NDEJEMBI TURUFU YA MAENDELEO KWA WATANZANIA

    RAIS DK. SAMIA, NDEJEMBI TURUFU YA MAENDELEO KWA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI AONYA, ATOA SIKU 60 WENYE SILAHA HARAMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NDEJEMBI MZIGONI RASMI, AKEMEA KAZI KWA MAZOEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUME MIPANGO, NIRC WAJADILI UBORA MIRADI YA UMWAGILIAJI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MASAUNI AANIKA UMAHIRI WA TANZANIA INAVYOLINDA UDONGO, MATUMIZI MBOLEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?