• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

KIHONGOSI AFICHUA SIRI MIKUTANO YA MGOMBEA URAIS CCM ‘KUFURIKA’

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 4, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
KIHONGOSI AFICHUA SIRI MIKUTANO YA MGOMBEA URAIS CCM ‘KUFURIKA’

KATIBU wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kenani Kihongosi

0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MUSSA YUSUPH

KATIBU wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kenani Kihongosi, ametaja sababu za mikutano ya mgombea Urais kupitia CCM, Dk. Samia Suluhu Hassan, kufurika maelfu ya wananchi kumsikiliza kiongozi huyo akinadi Ilani ya Uchaguzi ya CCM (2025 – 2030).

Amesema kukubalika kwa mgombea huyo wa Urais kupitia CCM, ndiyo, sababu ya mikutano yake kujaza wananchi tofauti na mikutano ya vyama vingine vya siasa nchini.

Akizungumza katika mahojiano maalumu kabla ya kuanza mkutano wa kampeni uliofanyika Mlima wa Reli, Mji mdogo wa Mbalizi mkoani Mbeya, Kihongosi amesema hakuna mgombea mwingine wa Urais kutoka vyama vingine vya siasa mwenye uwezo wa kumfikia Dk. Samia.

“Samia ni mgombea wa mfano, ana uzoefu wa ndani na nje ya nchi. Anayejua kazi, anapendwa na wananchi na ndiyo sababu mikutano ya kampeni ya CCM inajaza watu wengi tofauti na vyama vingine.

“Wananchi wanakipenda CCM na  wagombea wake, wanapenda kiendelee kuwepo madarakani kiendekee kuwatumikia, sasa ukija na hoja dhaifu kuwa CCM inabeba watu, CCM haijibu hoja dhaifu bali tunajibu hoja nzito ambazo zinakwenda kutoa majawabu kwa Watanzania, wajibu wa CCM ni kutatua kero za wananchi,” amesema.

Kihongosi amebainisha kuwa, ndani ya miaka minne, Dk. Samia amefanya mambo makubwa na kila kata, wilaya, mikoa imepelekewa fedha za kutekeleza miradi katika sekta mbalimbali.

Katika kuthibitisha hilo katika mkutano huo wa kampeni, idadi kubwa ya wananchi walimiminika katika uwanja wa Mlima wa Reli hali ambayo iliwalazimu wengine kubaki nje ya uwanja kufuatilia mkutano huo.

Shauku ya wananchi hao ilijikita zaidi kumshuhudia kiongozi huyo ambaye ameleta mapinduzi makubwa katika wilaya hiyo ambayo tangu ilipoanzishwa miaka ya 1980 haikuwa na hospitali ya wilaya, ndani ya miaka minne ya uongozi wa Dk. Samia, imejengwa hospitali ya kisasa yenye kutoa huduma mbalimbali zikiwemo za mama na mtoto.

Pia, mji huo mdogo umenufaika na ujenzi katika sekta ya maji, amesema sh. bilioni 4.8 zimewekezwa katika mradi wa Ilulu utakaoleta maji safi na salama katika eneo la Mbalizi.

Kuhusu elimu, amesema sh. bilioni 9.3 zimetumika kujenga shule na nyumba za walimu huku sh. bilioni 13.9 zimetumika kujenga madarasa 29 na maabara 14.

Previous Post

ILANI MPYA YA CCM IMEZINGATIA AMANI, USALAMA – DK. NCHIMBI

Next Post

CCM YATAJA SABABU MBILI KUOMBA KURA SONGWE

Next Post
CCM YATAJA SABABU MBILI KUOMBA KURA SONGWE

CCM YATAJA SABABU MBILI KUOMBA KURA SONGWE

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA ASISITIZA VIJANA KULINDA AMANI

DK. SAMIA ASISITIZA VIJANA KULINDA AMANI

6 months ago
DK. SAMIA AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM

DK. SAMIA AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI KUU YA CCM

5 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?