• ePaper
Saturday, November 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

WATALII WAENDELEA KUFURIKA NGORONGORO, WASIFU AMANI NA VIVUTIO VYA TANZANIA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 6, 2025
in Habari, Kitaifa
0
WATALII WAENDELEA KUFURIKA NGORONGORO, WASIFU AMANI NA VIVUTIO VYA TANZANIA
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na LILIAN JOEL,
ARUSHA

WATALII kutoka mataifa mbalimbali duniani wanaotembelea Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) wameendelea kufanya shughuli zao za utalii kwa amani, usalama na utulivu, huku wakifurahia vivutio lukuki vilivyopo katika hifadhi hiyo maarufu duniani.

Akizungumza katika lango kuu la Laoduare, Ofisa Uhifadhi Mkuu wa Idara ya Huduma za Utalii na Masoko wa NCAA, Peter Makutian, amesema katika kipindi chote cha uchaguzi mkuu wa Tanzania hadi kufikia Novemba 5, 2025, jumla ya wageni takribani 1,200 kutoka mataifa mbalimbali wametembelea hifadhi hiyo na kushiriki shughuli za utalii.

“Hifadhi ya Ngorongoro tunaendelea kupokea watalii wa ndani na wa kimataifa. Kwa sasa tuko katika msimu wa wastani, lakini tunaamini kuelekea sikukuu za mwisho wa mwaka idadi ya watalii itaongezeka zaidi,” amesema Makutian.

Kwa upande wake, Isabella Jerónimol, mtalii kutoka Colombia aliyefika nchini akiwa na familia ya watu 26, alisema walichagua kutembelea Tanzania kwa kuvutiwa na hali ya amani, ukarimu wa wananchi na utajiri wa vivutio vya asili.

“Safari hii tuliipanga kwa muda mrefu. Tumefurahi kufika Tanzania, nchi yenye vivutio vingi vya kipekee. Tulichagua Hifadhi ya Ngorongoro kwa sababu ni sehemu yenye historia kubwa na mandhari ya kuvutia. Tulikaribishwa vizuri na kupewa maelezo kuhusu wanyama na urithi wa hifadhi hii,” amesema Jerónimol.

Previous Post

RAIS DK. SAMIA APOKEA UJUMBE WA RAIS PUTIN

Next Post

CHAMA CHA MAWAKILI WA SERIKALI CHAMPONGEZA JOHARI

Next Post
CHAMA CHA MAWAKILI WA SERIKALI CHAMPONGEZA JOHARI

CHAMA CHA MAWAKILI WA SERIKALI CHAMPONGEZA JOHARI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

RAIS DK. MWINYI AONYA SIASA ZA CHUKI

RAIS DK. MWINYI AONYA SIASA ZA CHUKI

2 months ago
DK. NCHIMBI AGUSIA HISTORIA MPYA ILIYOANDIKWA NA DK. SAMIA

DK. NCHIMBI AGUSIA HISTORIA MPYA ILIYOANDIKWA NA DK. SAMIA

1 month ago

Popular News

  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAAGIZO MATATU KWA DK. NCHEMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NI MARIDHIANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.