• ePaper
Saturday, November 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

SADC WAMPONGEZA RAIS DK. SAMIA KWA USHINDI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 2025

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 8, 2025
in Habari, Kimataifa, Kitaifa, Siasa
0
SADC WAMPONGEZA RAIS DK. SAMIA KWA USHINDI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 2025
0
SHARES
10
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,
DODOMA

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, amesema Serikali inayoongozwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan imechukua hatua madhubuti za kurejesha utengamano wa kitaifa na kuhakikisha wananchi wanaishi chini ya misingi ya utawala wa sheria.

Dk. Nchimbi ametoa kauli hiyo akiwa mkoani Dodoma wakati akimwakilisha Rais Dk. Samia katika Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) uliofanyika kwa njia ya mtandao.

Amesema dhamira ya Rais Dk. Samia ni kuhakikisha mchakato wa mazungumzo ya maridhiano unafanikiwa ili kujenga taifa lenye amani, umoja na mshikamano na kuendelea kuwa mfano wa utulivu barani Afrika na duniani kwa ujumla.

Aidha, Makamu wa Rais amesisitiza kuwa Tanzania inaendelea kuwa nchi salama na tulivu na ipo tayari kupokea wageni kutoka mataifa mbalimbali kwa manufaa ya nchi na wananchi wake.

Aidha, Makamu wa Rais, amewashukuru viongozi wa SADC walioshiriki uapisho wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na wote waliotoa pongezi za dhati.

Amesema jitihada zote zitatumika kuhakikisha Tanzania inapata maendeleo na amani kuendelezwa.

Mkutano huo umempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan kwa ushindi aliyoupata na uchaguzi wenye mafanikio.

Mkutano huo ulilenga kujadili kujiondoa kwa nchi ya Madagascar kama nchi Mwenyekiti wa SADC, ambapo nchi ya Afrika Kusini imependekezwa kuwa Mwenyekiti kwa kipindi cha mpito mpaka kufikia mwezi Agosti 2026.

Mkutano huo umekubaliana kuendelea kutumia kauli mbiu ya Mkutano wa 45 wa SADC uliyofanyika nchini Madagascar ambayo ni “Kuimarisha Viwanda, Mapinduzi ya Kilimo, Mabadiliko ya Nishati kwa SADC yenye Uhimilivu”

Mkutano huo umeongozwa na Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa na kuhudhuriwa na Wakuu wa Nchi na Serikali pamoja na Wawakilishi kutoka Nchi 15 za SADC.

Previous Post

JKT TZ, SIMBA BALAA LIPO HAPA

Next Post

WASOMI, VIONGOZI WA DINI WAGUSIA UZALENDO, AMANI  

Next Post
WASOMI, VIONGOZI WA DINI WAGUSIA UZALENDO, AMANI  

WASOMI, VIONGOZI WA DINI WAGUSIA UZALENDO, AMANI  

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. CHIMBI AFICHUA KIINI ONGEZEKO LA WAWEKEZAJI

DK. CHIMBI AFICHUA KIINI ONGEZEKO LA WAWEKEZAJI

2 months ago
DK. SAMIA ATANGAZA HATUA ZA MWISHO UTEKELEZAJI MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA

DK. SAMIA ATANGAZA HATUA ZA MWISHO UTEKELEZAJI MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA

1 month ago

Popular News

  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    YANGA, SIMBA KAZI KAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KETE YA KWANZA KWA GAMONDI STARS LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TRA YAHAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO USALAMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAAGIZO MATATU KWA DK. NCHEMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NI MARIDHIANO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.