• ePaper
Saturday, May 30, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

SERIKALI YAITA SEKTA BINAFSI KUWEKEZA SGR

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 27, 2025
in Habari, Kitaifa
0
SERIKALI YAITA SEKTA BINAFSI KUWEKEZA SGR
0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ATHNATH MKIRAMWENI

SERIKALI imetoa wito kwa sekta binafsi kujitokeza kwa wingi kuwekeza katika usafiri wa reli ya kisasa (SGR).

Pia, serikali imesisitiza kuongeza ushiriki wa wawekezaji, ndilo suluhisho la kuhakikisha mfumo huo, unakuwa endelevu na wenye tija kwa taifa.

Kauli hiyo, ilitolewa jijini Dar es Salaam na Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa, alipotembelea maonesho ya kwanza ya wiki ya usafiri endelevu ardhini, yanayofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja.

Alisema serikali inafungua mfumo wa ‘open access’ kuruhusu kampuni binafsi kuleta mabehewa na vichwa  vya treni, hatua itakayoongeza ufanisi wa huduma na matumizi ya reli hiyo.

Alieleza ujenzi wa SGR kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma kwa upande wa nje, umekamilika kwa kiasi kikubwa, tayari safari za abiria, zimeanza kufanyika kwa mafanikio.

Profesa Mbarawa, alisema abiria wengi, wameridhishwa na huduma hiyo mpya, inachangia kwa kiasi kikubwa, mabadiliko katika sekta ya usafiri nchini.

Waziri huyo, alisisitiza ili reli hiyo itumike kwa saa 24 kama inavyokusudiwa, sekta binafsi zinapaswa kujumuishwa kikamilifu.

“Hatupaswi kuwa na treni inayosimama saa tano asubuhi hadi kesho saa 11. Tunataka treni ziendelee kupita muda wote,” alisema.

Alisema sekta binafsi, zinaweza kuwekeza katika mabehewa, vichwa vya treni na kuanza kutoa huduma za kusafirisha mizigo kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma na maeneo mengine.

“Tanzania inalenga kuwa na mfumo wa reli usio na ajali kwa kutegemea utaratibu wa kufuata kanuni. Tukifuata miongozo tuliyonayo, tutakuwa na ‘zero accident’, ajali hazitatokea kama kila mmoja atafuata taratibu,” alisema.

Profesa Mbarawa, alisema SGR itadumu na kufanya kazi kwa ufanisi wa juu kwa miaka mingi, ikiwa nidhamu ya uendeshaji, uwekezaji wa sekta binafsi na ufuataji wa kanuni, utaendelea kupewa kipaumbele.

Previous Post

DK. MWIGULU AWAONYA MADEREVA WA SERIKALI

Next Post

SIMBACHAWENE AHIMIZA KUDUMISHA ZAIDI AMANI

Next Post
SIMBACHAWENE AHIMIZA KUDUMISHA ZAIDI AMANI

SIMBACHAWENE AHIMIZA KUDUMISHA ZAIDI AMANI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

RAIS DK. SAMIA AGEUKIA VITA DHIDI YA MALARIA 

RAIS DK. SAMIA AGEUKIA VITA DHIDI YA MALARIA 

3 months ago
ESPERANCE, SIMBA MECHI YA HESABU

ESPERANCE, SIMBA MECHI YA HESABU

4 months ago

Popular News

  • RAS: UTUNZAJI MAZINGIRA AJENDA YA KIPAUMBELE KWA MKOA WA MWANZA

    RAS: UTUNZAJI MAZINGIRA AJENDA YA KIPAUMBELE KWA MKOA WA MWANZA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • UPELE UMEPATA MKUNAJI STARS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ‎ RAIS DK. SAMIA: POLISI MSIDHARAU TAARIFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWIGULU ATETA NA WAZIRI MKUU WA CONGO BRAZZAVILLE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MASTAA YANGA WAUTAJA UBINGWA LIGI KUU BARA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?