• ePaper
Thursday, June 18, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

STARS YAPEWA NJIA KUTOBOA AFCON 2025

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 29, 2025
in Burudani, Kimataifa, Michezo
0
STARS YAPEWA NJIA KUTOBOA AFCON 2025

STARS

0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na AMINA KASHEBA

WADAU wa soka nchini wamesema timu ya taifa ‘Taifa Stars’ ikiwa na mpango bora, nidhamu na kujituma katika Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025, itakuwa na nafasi kubwa ya kufanya vyema katika michuano hiyo.

Taifa Stars ni moja ya timu 24 zitakazoshiriki AFCON 2024 inayotarajiwa kuanza Jumapili hii nchini Morocco.

Katika michuano hiyo, Taifa Stars ipo kundi imepangwa kundi C na Nigeria, Tunisia pamoja na Uganda.

Tanzania itaanza ratiba yake Desemba 23, mwaka huu dhidi ya Nigeria.

Hiyo ni mara ya nne kwa Tanzania kushiriki fainali za AFCON ambapo mara ya kwanza ilikuwa mwaka 1980 nchini Nigeria kisha mwaka 2019 nchini Misri na 2023 nchini Ivory Coast ambapo fainali zake zilichezwa mwaka jana.

Katika kundi hilo, Taifa Stars ndiyo timu iliyofuzu fainali hizo mara chache (4), Tunisia mara 22, Nigeria mara 21 wakati Uganda ikitinga mara nane.

Katika kundi hilo, Taifa Stars ndiyo timu pekee ambayo haijawahi kupenya hatua ya mtoano wakati Nigeria ikiwa ni bingwa mara tatu mwaka 1980, 1994 na 2013, Tunisia mara moja mwaka 2004 huku Uganda ikiwahi kushika nafasi ya pili mwaka 1978.

Hata hivyo, wadau wa soka nchini wamesema timu hiyo inayonolewa na Miguel Gamondi, awamu hii ina nafasi kubwa ya kufanya vyema na kuvunja mwiko huo ikiwa itaingia na mpango bora, nidhamu na kujituma.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, mchezaji wa zamani wa Simba na Tafa Stars, Zamoyoni Mogella alisema mipango bora, nidhamu na kujitoa kwa wachezaji ndiyo sababu kubwa ya wao kufanya vizuri katika michuano hiyo.

“Sina hofu na ubora wa Kaimu Kocha Mkuu, Miguel Gamondi kwa sababu anatambua wachezaji wa Stars, hivyo ni muda wao kusikiliza maelekezo na mbinu wanazofundisha.

“Maandalizi yakiwa mazuri na wachezaji wakifuata mipango ya mwalimu wakiongeza nidhamu na kujitoa basi watafanya vizuri, haijalishi wanakutana na timu gani,” alisema Mogella.

Mogella aliongeza kuwa, kila nchi inajipanga kuhakikisha inafanya vizuri hivyo Gamondi anatambua ni mipango gani anakwenda nayo katika michuano hiyo.

Kocha wa soka la vijana, Maalim Salehe, alisema mpira sasa umebadilika hivyo hana wasiwasi na Taifa Stars kwa kuwa imejiandaa vyema kufanya vizuri.

“Kuwa na jina kubwa siyo sababu ya kufanya vizuri katika soka kwa sababu baadhi ya mataifa ambayo ni vinara hawajashiriki AFCON, kujipanga, nidhamu ya wachezaji wa Stars italeta matunda kwao.

“Pia, uimara wa mwalimu, Gamondi utaleta picha nzuri kuanza na Nigeria sio sababu ya kusema itashindwa kutamba maana mpira wa hivi sasa umebadilika,” alisema.

Kocha huyo aliongeza kuwa, jambo muhimu kwa wachezaji wanapaswa kuzingatia ni kusikiliza maelekezo ya mwalimu na kuongeza juhudi.

Aliyekuwa kocha wa timu ya taifa ya Watu Wenye Ulemavu ‘Tembo Warriors’, Salvatory Edward alisema Gamondi anafahamu anakwenda katika michuano ya aina gani, hivyo hana shaka na ubora aliokuwa nao.

Alisema hivi sasa Watanzania wanapaswa kuiombea dua timu hiyo kuhakikisha inafanya vyema.

“Kila kitu kinawezekana katika soka kwa sababu kila kocha anajua anakwenda na mipango ya aina gani, kwangu namuamini Gamondi kwa sababu ana mifumo ambayo italeta ushindi kwa Stars,” alisema.

Previous Post

WAZIRI MKUU : WATANZANIA TUNZENI AKIBA YA CHAKULA

Next Post

AZAM FC KUANZA TIZI DESEMBA 23

Next Post
AZAM FC KUANZA TIZI DESEMBA 23

AZAM FC KUANZA TIZI DESEMBA 23

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA AVUNJA NGOME YA UPINZANI MKOANI LINDI

DK. SAMIA AVUNJA NGOME YA UPINZANI MKOANI LINDI

9 months ago
SERIKALI YATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI NISHATI ZA DOLA BIL. 12.9

SERIKALI YATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI NISHATI ZA DOLA BIL. 12.9

3 months ago

Popular News

  • WABUNGE: AMANI ISICHEZEWE

    WABUNGE: AMANI ISICHEZEWE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WABUNGE WAIPONGEZA NSSF NA PSSSF KWA KUANZISHA SKIMU YA HIFADHI KWA WALIOJIAJIRI NA UWEKEZAJI WA KIWANDA CHA NGOZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WABUNGE WAPONGEZA UWEKEZAJI KLICL

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAKAGUZI WA CAF WARIDHISHWA NA MAENDELEO YA VIWANJA VYA AFCON 2027

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MKAKATI KUDHIBITI VIFO WAJAWAZITO WAANIKWA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?