• ePaper
Wednesday, March 18, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

AZAM FC KUANZA TIZI DESEMBA 23

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 15, 2025
in Burudani, Michezo
0
AZAM FC KUANZA TIZI DESEMBA 23
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na DEUSDEDIT UNDOLE

OFISA Habari wa Klabu ya Azam, Hashim Ibwe amesema kikosi chao kimepanga kuanza mazoezi Desemba 23, mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Akizungumza Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita, Ibwe alisema maandalizi hayo yamelenga kujiandaa kikamilifu kwa mechi zijazo za Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Kombe la Shirikisho Afrika (CAFCC) na nyinginezo.

“Baada tu ya kusimama kwa msimu huu Ligi Kuu ili kupisha AFCON, Azam FC tulitoa mapumziko kwa wachezaji na benchi letu la ufundi, ila tumepanga kurejea mazoezini Desemba 23, mwaka huu,” alisema Ibwe.

Alisema kikosi hicho ambacho msimu huu kinanolewa na Florent Ibenge ambaye ni raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo(DRC), kimejipanga kufanya vyema.

Ofisa huyo alisema wamedhamiria kukiongezea nguvu kikosi hicho dirisha dogo la usajili litakapofunguliwa mwezi ujao.

“Kimsingi Azam FC licha ya kuanza kwetu kwa kusuasua mechi zetu mbili za CAFCC za hatua ya makundi. Lakini tutahakikisha tunaimarisha kikosi chetu ili tuhimili ushindani kwenye michuano hiyo ya pili kwa ukubwa inayoandaliwa na Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF),” alisema ofisa huyo.

Mechi za CAFCC ambazo Azam FC imepoteza ni ile ya ugenini dhidi ya AS Maniema ambayo ilipigwa DRC Novemba 23, mwaka huu ambapo kikosi hicho kilala kwa mabao 2-0 na Novemba 28, mwaka huu katika Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar wawakilishi hao wa Tanzania Bara walikubali kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Wydad AC ya Morocco.

Previous Post

STARS YAPEWA NJIA KUTOBOA AFCON 2025

Next Post

NI SAFARI YA MABILIONI YA FEDHA AFCON 2025

Next Post
NI SAFARI YA MABILIONI YA FEDHA AFCON 2025

NI SAFARI YA MABILIONI YA FEDHA AFCON 2025

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. NCHIMBI AELEZA MKAKATI WA RELI SGR HADI KIGOMA

DK. NCHIMBI AELEZA MKAKATI WA RELI SGR HADI KIGOMA

5 months ago
KAPOMBE, DUCHU WATOA MSIMAMO SIMBA

KAPOMBE, DUCHU WATOA MSIMAMO SIMBA

2 months ago

Popular News

  • MANDONGA AJA KIVINGINE

    MANDONGA AJA KIVINGINE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YATUMIA BILIONI 64/- KUBORESHA UWANJA WA NDEGE IRINGA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU AWAWEKA MTEGONI VIGOGO WILAYA, HALMASHAURI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ALAMA TATU KUMUENZI JPM

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI KUIFANYA TANZANIA KITOVU CHA BIASHARA – DK. YONAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?