• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

YANGA, SIMBA ZAPEWA MBINU KULIPA KISASI 

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 26, 2026
in Burudani, Michezo
0
YANGA, SIMBA ZAPEWA MBINU KULIPA KISASI 
0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

KOCHA Amri Said  ametaja mbinu tatu za kuhakikisha timu za Yanga na Simba zinashinda mechi zijazo za Ligi ya Mabingwa Afrika.

Akizungumza UHURU jijini Dar es Salaam, Said  maarufu kwa jina la ‘Jap Stam ‘alisema Yanga na Simba zina wachezaji wazuri wenye uwezo wa kupindua meza.

“Timu zipo vizuri lakini kuna changamoto kadhaa ambazo zikifanyiwa kazi na makocha ushindi unapatikana,”alisema.

Amri Said ambaye aliwahi kuichezea Simba kwa mafanikio makubwa, alisema timu hizo zikiimarisha sehemu ya ulinzi na ushambuliaji mambo yatakauwa mazuri.

Alisema jambo jingine la pili ni kuhakikisha mashabiki wanawapa sapoti ya kutosha ili ziweze kushinda.

Sababu nyingi alisema ni vyema wachezaji wote wa timu hizo wakacheza kwa tahadhari kutokana na mbinu za timu za ukanda wa Kaskazini mwa Afrika kuwa wajanja wa kupoteza muda na kuwatafutia kadi wachezaji wa timu pinzani.

Yanga inatarajiwa kucheza na Al Ahly visiwani Zanzibar huku Simba nayo ikicheza na timu ya Esperance Tunis jijini Dar es Salaam.

YANGA

Akizungumzia kuhusu kikosi cha Yanga, Amri Saidi alisema timu hiyo ilicheza vizuri kulingana na mpango wa kocha , Pedro Goncalves.

“Unajua ule mchezo ulikuwa na hesabu mbili za kulinda na kushambulia kwa kushtukiza, walicheza vizuri,”alisema.

Beki huyo wa zamani wa Simba alisema kasoro ilikuwa kuna muda walinzi wa Yanga walijisahau kuwahi kurudi nyuma kuziba nafasi ambazo wachezaji wa Al Ahly walitumia vizuri kupata  ushindi.

“Angalia bao la kwanza lilifungwa kutokana na beki mmoja wa Yanga kushindwa kuondoa mpira kwa kichwa  ambapo mchezaji wa Al Ahly alitumia nafasi kufunga,” alisema.

Kocha huyo alisema bao la pili lilitokana na kosa la mchezaji moja kutoa mpira kwa mchezaji wa Al Ahly kitu ambacho kilisababisha  timu hiyo ya Misri kupata bao la pili.

“Naamini makocha wa Yanga wameona kasoro hizo , najua watazifanyia kazi na kisha kusuka wembe wa pale mbele mipira ikija waitumie kuwaadhibu Al Ahly katika mchezo ujao, wanafungika wale,” alisema.

Hata hivyo, Amri Saidi alimsifu kocha wa Yanga kwa jinsi alivyopanga kikosi na kutengeneza nafasi nyingi kama washambuliaji wangekuwa makini timu hiyo ingerudi nchini na ushindi.

“Wachezaji wa Yanga walitengeneza nafasi kadhaa, lakini walikosa mabao, angalia Al Ahly ina wachezaji bora na wana uwezo wa kubadili matokeo muda wowote, walitumia makosa ya wachezaji wa Yanga kushinda mchezo huo,” alisema.

Alisema Yanga ina kazi kubwa kutokana na Al Ahly kuundwa na nyota wenye viwango vikubwa huku wengine wakitoka timu za Barani Ulaya.

“’Quality’ ya wachezaji wa Ahly ni kubwa, lakini wachezaji wa Yanga walipata nafasi nyingi wakashindwa kuzitumia, wenzao walipata nafasi chache wakapata ushindi,ni imani yangu Yanga wakitulia na kujipanga kuondoa kasoro hizo, watashinda mchezo ujao,” alisema Amri.

SIMBA

Kocha Amri Saidi alisema wachezaji wa Simba walicheza vizuri walikuwa na ubora, lakini shida ilikuwa sehemu  ya kiungo, ilishindwa  muda mwingine kuunganisha mipira  kufika lango la Esperance.

“Washambuliaji wa Simba walipoteza nafasi kadhaa kupachika mabao, kuna wakati walipata nafasi wakapoteza,” alisema.

Hata hivyo, kocha huyo alishauri benchi la ufundi la Simba kufanya marekebisho upande wa ushambuliaji.

“Nasema bado Simb a inatakiwa kuwa na mshambuliji wa kupachika mabao, kwani nimejaribu kuangalia pale namba tisa na 10, hakuna mtu wa kusumbua sana, walinzi wa timu pinzani,”alisema.

 Hata hivyo, kocha huyo aliusifu uongozi wa Simba kwa kuongeza nguvu katika kikosi chao.

“Nimeona baadhi ya wachezaji waliosajiliwa hivi karibuni wameonesha uwezo mkubwa,.Chama alifanya kazi nzuri yak ugawa mipira mbele lakini ilikuwa inapotea,” alisema Amri Said.

Pia, kocha huyo alipendekeza makocha wa Simba inabidi wafanyie kazi sehemu ya walinzi wa timu hiyo kuhakikisha wanacheza mipira ya krosi inayopigwa na timu pinzani ili lango liwe salama.

Previous Post

KAMATI KUU CCM YATEUA, WAMO MAKONDA, LUSINDE

Next Post

‘HAPPY BIRTHDAY’ RAIS DK. SAMIA, KINARA WA UTUNZAJI MAZINGIRA

Next Post
‘HAPPY BIRTHDAY’ RAIS DK. SAMIA, KINARA WA UTUNZAJI MAZINGIRA

'HAPPY BIRTHDAY' RAIS DK. SAMIA, KINARA WA UTUNZAJI MAZINGIRA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SERIKALI YAWEKA BAYANA KILICHOJIRI BUNGE LA EU

SERIKALI YAWEKA BAYANA KILICHOJIRI BUNGE LA EU

5 months ago
RAIS DK. SAMIA ATUMA UJUMBE WA AMANI

RAIS DK. SAMIA ATUMA UJUMBE WA AMANI

4 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?