• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

KAMATI KUU CCM YATEUA, WAMO MAKONDA, LUSINDE

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 26, 2026
in Habari, Kitaifa
0
KAMATI KUU CCM YATEUA, WAMO MAKONDA, LUSINDE
0
SHARES
13
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

KAMATI Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, katika kikao chake kilichofanyika jana Zanzibar, pamoja na mambo mengine, imepitia, kujadili na kufanya uteuzi wa wagombea uongozi wa CCM wanaotokana na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa nafasi mbalimbali.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na kutiwa saini na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa (NEC) Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Kenani Kihongosi, ilisema, Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa wanaotokana na Bunge kutoka Tanzania Bara nafasi tatu ambao ni Paul Christian Makonda, Livingstone Joseph Lusinde na Asia Abdulkarim Halanga.

Taarifa hiyo ilieleza zaidi kuwa Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa wanaotokana na Bunge kutoka Zanzibar, walioteuliwa ni Khamis Mussa Omar na Tauhida Cassian Galos.

Pia, katibu wa wabunge wote wa CCM, ameteuliwa Agnes Elias Hokororo.

Wenyeviti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, wameteuliwa watatu ambao ni Najma Murtaza Giga, Deodatus Philipo Mwanyika na Cecilia Daniel Pareso

Aidha, Kamati Kuu ya Halmashauri ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, pia imefanya uteuzi wa wagombea uongozi wa CCM wanaotokana na Baraza la Wawakilishi ambao ni Said Ali Juma, Hamza Hassan Juma na  Lela Muhamed Mussa.

Wawakilishi wa CCM watakaoingia bungeni kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Bakar Hamad Bakar, Dk. Shaame Ali Ali, Simai Mohammed Said na Fatma Ramadhan Mandoba.

Katibu wa Wawakilishi wote wa CCM, ameteuliwa Machano Othman Said huku wenyeviti wa Baraza la Wawakilishi ni Mahmoud Omar Hamad na Hudhaima Mbarak Tahir

UCHAGUZI MDOGO PERAMIHO

Kuhusu mchakato wa uchaguzi wa ubunge, Jimbo la Peramiho,

kwa kuzingatia mamlaka iliyopewa chini ya Ibara ya 105 (7)(f) ya Katiba ya CCM ya Mwaka 1977 Toleo la Julai 2025, Kamati Kuu imefanya uteuzi wa Dk. Lazaro Killian Kombakuwa mgombea wa CCM katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Peramiho, lililopo Wilaya ya Songea Vijijini.

Previous Post

BODABODA, MACHINGA, MAMA LISHE SHANGWE

Next Post

YANGA, SIMBA ZAPEWA MBINU KULIPA KISASI 

Next Post
YANGA, SIMBA ZAPEWA MBINU KULIPA KISASI 

YANGA, SIMBA ZAPEWA MBINU KULIPA KISASI 

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

RAIS DK. SAMIA ASISITIZA UWEKEZAJI WA KIMKAKATI

RAIS DK. SAMIA ASISITIZA UWEKEZAJI WA KIMKAKATI

2 weeks ago
PM MWIGULU KUVALIA NJUGA MIGOGORO YA ARDHI

PM MWIGULU KUVALIA NJUGA MIGOGORO YA ARDHI

4 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?