• ePaper
Saturday, May 30, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

DK. YONAZI AIELEZA MSUMBIJI UZOEFU WA TANZANIA INAVYOKABILI UKAME

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
May 26, 2026
in Habari, Kitaifa
0
DK. YONAZI AIELEZA MSUMBIJI UZOEFU WA TANZANIA INAVYOKABILI UKAME
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI MAALUMU, Msumbiji

TANZANIA inaandaa mpango wa kitaifa wa hatua za mapema za kujiandaa kukabiliana na ukame kwa maeneo yanayokabiliwa na janga hilo kwa kushirikiana na Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP).

Mpango huo ni jitihada za kupunguza athari za janga hilo nchini hali inayoonesha dhamira ya serikali kuacha utaratibu wa kusubiri madhara yatokee ndipo ichukue hatua.

Hayo yalielezwa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Dk. Jim Yonazi, katika ziara ya kubadilishana uzoefu kati ya Tanzania na Msumbiji kuhusu hatua za mapema kabla ya majanga iliyofanyika Mei 25, 2026, mjini Maputo nchini Msumbiji.

Alisema ukame una madhara makubwa katika kilimo, mifugo, rasilimali za maji, usalama wa chakula, maisha ya wananchi, maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa ujumla.

“Kwa sasa Tanzania inaendelea kuandaa mpango wa kitaifa wa hatua za mapema dhidi ya ukame kwa msaada wa WFP, kwa kutambua bado ni moja ya majanga makubwa yanayoathiri nchi yetu,” alisema Dk. Yonazi.

Alifafanua mpango huo utawezesha kuwepo mifumo imara ya tahadhari na utekelezaji wa hatua za mapema kabla majanga hayajatokea.

Dk. Yonazi alieleza Tanzania imechagua kujifunza kutoka Msumbiji kutokana na mafanikio yake katika kuanzisha na kutekeleza mifumo ya hatua za mapema dhidi ya majanga, hususan ukame, mafuriko na vimbunga.

Alisema kupitia ushirikiano huo, Tanzania itanufaika kwa kubadilishana uzoefu na mbinu bora, kujifunza mifumo ya uratibu wa taasisi, vigezo vya kuanzisha hatua za mapema pamoja na namna ya kugharimia hatua hizo.

Katibu mkuu huyo alieleza uzoefu huo utasaidia kuunganisha hatua za mapema ndani ya mifumo ya hifadhi ya jamii kuongeza ufanisi katika kukabiliana na majanga.

AUPONGEZA UBALOZI WA TANZANIA

Katika hatua nyingine, Dk. Yonazi ameupongeza ubalozi wa Tanzania nchini Msumbiji kwa namna unavyoendelea kutekeleza majukumu yake na kuimarisha uhusiano baina ya nchi hizo mbili.

Alisema hayo jana alipotembelea ofisi hizo pamoja na ujumbe alioongozana nao kwa lengo la kushiriki katika ziara ya kubadilishana uzoefu kati ya Tanzania na Msumbiji kuhusu hatua za mapema kabla ya majanga.

Dk. Yonazi alizungumza na watumishi wa ubalozi huo na kupokea taarifa fupi ya utekelezaji wa majukumu iliyotolewa na Mwambata Fedha, Samson Marwa kwa niaba ya Hamad Khamis Hamad, Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji aliyekuwa katika majukumu mengine.

“Ninawapongeza namna mnavyoendelea kuiwakilisha nchi yetu, ni vyema kuendelea kuangalia fursa zilizopo na kuzitangaza hususan za kiuchumi zitakazowavutia kuja kuwekeza Tanzania, niwasihi kuendelea kuwa mabalozi wazuri wa nchi yetu,” alisema Dk. Yonazi

Mwambata Fedha, Marwa aliahidi kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kuhakikisha jukumu la msingi la uhusiano kati ya Tanzania na Msumbiji linaendelea kuimarika kwa manufaa ya nchi hizo mbili.

Previous Post

NEEMA YA AJIRA MAMBO YA NDANI

Next Post

DK. MWIGULU ASHIRIKI MKUTANO WA NGAZI YA WAKUU WA NCHI JIJINI BRAZZAVILLE

Next Post
DK. MWIGULU ASHIRIKI MKUTANO WA NGAZI YA WAKUU WA NCHI JIJINI BRAZZAVILLE

DK. MWIGULU ASHIRIKI MKUTANO WA NGAZI YA WAKUU WA NCHI JIJINI BRAZZAVILLE

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WASIRA AWATOLEA UVIVU WALIOANZA MBIO ZA URAIS

WASIRA AWATOLEA UVIVU WALIOANZA MBIO ZA URAIS

2 months ago
TAIFA STARS KUKIPIGA FIFA SERIES 2026

TAIFA STARS KUKIPIGA FIFA SERIES 2026

3 months ago

Popular News

  • RAS: UTUNZAJI MAZINGIRA AJENDA YA KIPAUMBELE KWA MKOA WA MWANZA

    RAS: UTUNZAJI MAZINGIRA AJENDA YA KIPAUMBELE KWA MKOA WA MWANZA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • UPELE UMEPATA MKUNAJI STARS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ‎ RAIS DK. SAMIA: POLISI MSIDHARAU TAARIFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWIGULU ATETA NA WAZIRI MKUU WA CONGO BRAZZAVILLE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MASTAA YANGA WAUTAJA UBINGWA LIGI KUU BARA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?