RABAT, Morocco
TIMU nne vigogo leo zitashuka dimbani katika mechi mbili za nusu fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025, zitakazochezwa nchini Morocco.
Timu hizo ni Misri itakayochuana na Senegel saa 2:00 usiku wakati mwenyeji Morocco ikicheza na Nigeria saa 5:00 usiku.
Misri ambayo ni bingwa mara saba wa michuano hiyo itacheza na Senegal ambayo ni bingwa mara moja katika Uwanja wa Tanger.
Kikosi cha Misri kimetinga hatua hiyo baada ya kuitoa Ivory Coast kwa ushindi wa mabao 3-2 huku Senegal ikiiondosha Mali kwa bao 1-0 katika robo fainali.
Kwa upande wa Morocco ambayo ni bingwa mara moja itachuana na Nigeria ambayo ni bingwa mara tatu katika Uwanja wa Prince Moulay Abdellah jijini Rabat.
Morocco ilifika hatua hiyo baada ya kuitoa Cameroon kwa ushindi wa mabao 2-0 wakati Nigeria ikiifunga Algeria kwa ushindi wa 2-0 katika robo fainali.




