• ePaper
Saturday, June 6, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

KOCHA MPYA ABEBESHWA MZIGO SIMBASC

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 16, 2025
in Burudani, Kitaifa, Michezo
0
KOCHA MPYA ABEBESHWA MZIGO SIMBASC
0
SHARES
28
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ABDUL DUNIA

KLABU ya soka ya Simba inamsubiri kocha wake mpya kutoa mapendekezo ya maboresho ya kikosi hicho kwa mechi zijazo za Ligi Kuu Tanzania Bara, Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) na Kombe la Shirikisho kuhakikisha miamba hiyo inaingia sokoni kuimarisha timu katika dirisha dogo.

Simba ambayo ipo katika hatua za mwisho kumtangaza kocha mpya baada ya kuachana na Meneja Mkuu Dimitar Pantev, inajipanga na usajili katika dirisha dogo linalotarajiwa kufunguliwa mwezi ujao.

Hivi  karibuni, uongozi wa klabu hiyo ulikiri kupokea maombi ya makocha  zaidi ya 100 ambapo majina raia wa Afrika Kusini, Steve Becker ambaye ni Kocha wa Stellenbosch na raia wa Hispania, Antonio Casano anayekinoa kikosi cha Atletico Luanda ya Angola ndio wametajwa sana mmoja wapo kupewa mikoba  ya Pantev.  

Miamba hiyo inahitaji kufanya uboreshaji wa kikosi hicho kwa kuongeza nyota mahiri na kuwakata baadhi ya wachezaji wake wa sasa, lakini kabla ya kuchukua uamuzi huo kwanza itasubiri mapendekezo ya benchi jipya la ufundi.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally, amesema tayari klabu hiyo inaripoti ya kiufundi ya hali ya kikosi chake na nini cha kufanya katika dirisha dogo.

Hata hivyo, Ahmed amesema kabla ya uongozi kushusha mchezaji yoyote kwanza itasubiri mapendekezo ya kocha wake mpya atakayepatikana hivi karibuni kuhakikisha kila mchezaji anayetua anakuwa chaguo lake.

“Maboresho ya kikosi yanasubiri ujio wa mwalimu mpya ndiyo atoe mapendekezo yake kulingana na ripoti za kiufundi zilizopo,” alisema.

Ahmed amesema timu hiyo inarejea mazoezini Desemba 28, mwaka huu kujiweka fiti kwa muendelezo wa Ligi Kuu Bara, Ligi ya Mabingwa Afrika na michuano mingine.

Meneja huyo aliweka wazi kuwa, Simba imepanga kufanya vyema katika michuano yake yote hasa CAFCL ambayo imeanza kwa kusuasua katika hatua ya makundi.

Katika michuano hiyo, Simba inaburuta mkia katika kundi D ikiwa haina pointi baada ya kupokea vichapo viwili mfululizo dhidi ya Petro Atletico ya Angola (1-0) na Stade Malien kutoka Mali (2-1).

Simba katika kundi hilo imebakisha mechi nne dhidi ya Esperance ya Tunisia (nyumbani na ugenini), Petro (ugenini) na Stade Malien (nyumbani).

Katika Ligi Kuu Bara, Wekundu hao wa Msimbazi wamepoteza mechi moja kati ya tano ilizocheza ikianza kwa ushindi dhidi ya Fountain Gate (3-0), Namungo (3-0), JKT Tanzania (2-1) na Mbeya City (3-0) kabla ya kufungwa na Azam FC (2-0).

Previous Post

TANZANIA YANG’ARA MKUTANO MKUU WA KUPAMBANA NA RUSHWA JIJINI DOHA, QATAR

Next Post

TAIFA STARS KUTUA MOROCCO KWA KISHINDO

Next Post
TAIFA STARS KUTUA MOROCCO KWA KISHINDO

TAIFA STARS KUTUA MOROCCO KWA KISHINDO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WENYE UMRI HUU HATARINI KUPATA PRESHA YA MACHO

WENYE UMRI HUU HATARINI KUPATA PRESHA YA MACHO

4 months ago
MWIGULU ATAJA MWAROBAINI MAFURIKO DARAJA LA DUMILA

MWIGULU ATAJA MWAROBAINI MAFURIKO DARAJA LA DUMILA

4 weeks ago

Popular News

  • MWANZA KINARA USIMAMIZI MAAFA

    MWANZA KINARA USIMAMIZI MAAFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WFP KUENDELEZA USHIRIKIANO NA TANZANIA USIMAMIZI WA MAAFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • HESHIMA KUBWA KWA TANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU: MAMBO MAZURI YANAKUJA, AIPA TANO SERENGETI BOYS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERENGETI BOYS HESHIMA KILA KONA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?