• ePaper
Saturday, June 6, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

DK. MWIGULU ASHUSHA MAAGIZO KWA MA -RC

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 22, 2025
in Habari, Kitaifa
0
DK. MWIGULU ASHUSHA MAAGIZO KWA MA -RC

WAZIRI Mkuu Dk. Mwigulu Nchemba

0
SHARES
13
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI MAALUMU

WAZIRI Mkuu Dk. Mwigulu Nchemba, amemwagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), awaandikie barua wakuu wote wa mikoa, waunde timu za ukaguzi wa majengo.

Pia, miradi katika mikoa yao, kama njia ya kukabiliana na wakandarasi wanaokiuka makadirio ya gharama za ujenzi (BOQ) wa miradi ya serikali.

“Yuko Mhandisi ambaye huwa anakagua miradi wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru.

“Wakuu wote wa mikoa, wawe na timu za vijana wa aina hiyo,  wasiuziwe mbuzi kwenye gunia.

“Uwe ni utamaduni wa serikali kufanya ukaguzi wa aina hiyo,” alisema Waziri Mkuu.

Dk. Mwigulu alitoa agizo hilo, akizungumza na viongozi na wananchi wa Wilaya za Ruangwa na Nachingwea, mkoani Lindi, akiwa katika ziara ya siku tatu ya kukagua miradi ya maendeleo mkoani humo.

Baada ya kukagua ujenzi wa ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea, Dk. Mwigulu, alisema kuna baadhi ya miradi ambayo wakandarasi wake hawafuati BOQ.

“Unakuta BOQ, inataka nondo za mm 16, lakini mkandarasi anaweka za mm 12. “Kuna mahali zinatakiwa nondo sita, yeye anaweka nondo nne. Jengo likikamilika, huwezi kuona na kulinganisha makubaliano ya BOQ.  Nimeelekeza kila mkoa uwe na timu ya wataalamu wa kukagua miradi ya serikali.”

“Mikoa yote wawe na vitengo hivi, wawe pia na vifaa vya kuchunguza majengo na miradi mingine, badala ya kusubiri uchunguzi unaofanywa wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru.

“Vitengo hivyo, kazi yao ya kila siku ni kufuatilia miradi kubaini maeneo ambako serikali imetoa fedha na hazijatumika vizuri, tuchukue hatua,” alisisitiza.

Mapema, Dk. Mwigulu, aliweka jiwe la msingi katika mradi wa maji wa Lindi-Ruangwa- Nachingwea uliojengwa katika Kijiji cha Chimbila A wilayani Ruangwa, mkoani Lindi.

Mradi huo ambao chanzo chake kinatoka mito ya Nyangao na Chilua wilayani Lindi, unatekelezwa na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), utakapokamilka, utanufaisha vijiji 56 katika Wilaya za Ruangwa (vijiji 34), Wilaya ya Nachingwea (vijiji 21) na Wilaya ya Lindi (kijiji kimoja).

Akitoa taarifa ya mradi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa RUWASA, Mhandisi Walter Kirita, alisema mradi huo, unatarajiwa kugharimu sh. bilioni 119, hadi sasa wameshalipa sh. bilioni 49 ambapo ujenzi wake umefikia asilimia 67 ya utekelezaji.

Mradi huo, umeanza kutekelezwa Februari, 2023 na awamu ya kwanza (Lot 1) inatarajiwa kukamilika Juni, 2026.

Hata hivyo, Mhandisi Kirita, alimweleza Waziri Mkuu kuwa, ifikapo Februari, 2026 baadhi ya vijiji vitaanza kupata huduma ya maji.

Akizungumza baada ya kuweka jiwe la msingi, Dk. Mwigulu, alisema ameridhishwa na hatua ya utekelezaji wa miradi ambayo imefikiwa.

“Hivi ndivyo Rais Samia anataka kuona namna kazi inavyofanyika. Hapa tumeona asilimia ya utekelezaji ni kubwa kuliko fedha zilizotolewa hadi sasa. ”

Dk. Mwigulu, alitumia fursa hiyo kumpongeza Waziri Mkuu mstaafu, Kassim Majaliwa, kuasisi mradi huo na kufuatilia fedha za mradi kila mara.

AWESO

Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, alisema mradi huo ulikuwa ombi maalumu la Majaliwa, aliyeomba kutokana na eneo hilo kukosa maji safi na salama.

“Baada ya ombi hilo, Rais Samia, alitoa maelekezo kuhakikisha mradi unaanza mara moja wananchi wa Ruangwa waweze kupata maji safi na salama.

“Mradi huu ni wa sh. bilioni 119 bajeti ya msimu uliopita, ambapo wewe Waziri Mkuu, ulikuwa Waziri wa Fedha, tulipoleta ombi hilo, halikuwa kikwazo na ukatoa fedha zote, mkandarasi hatudai chochote na kabla ya Februari mwakani, kuna baadhi ya vijiji wataanza kunufaika nao,” alisema.

NAIBU WAZIRI WA AFYA

Naibu Waziri wa Afya, Dk. Florence Samizi, alisema alimpongeza Rais Samia kwa mradi huo mkubwa wa maji.

Aidha, alisema kuanzia Januari mwakani, kutakuwa na bima ya afya kwa wote na katika Mkoa wa Lindi, kutakuwa na wanufaika 26,000 kati ya 900,000.

PROFESA MKUMBO

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo, alimpongeza Dk. Mwigulu kwa ziara anazofanya, ambazo zinaonesha umahiri katika utendaji wake.

Previous Post

HADHI YA TANZANIA KIMATAIFA ILINDWE KWA GHARAMA ZOZOTE

Next Post

UKILA BATA KRISMASI, USISAHAU ADA JANUARI

Next Post
UKILA BATA KRISMASI, USISAHAU ADA JANUARI

UKILA BATA KRISMASI, USISAHAU ADA JANUARI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

KIDATO CHA PILI KUANZA MITIHANI NOVEMBA 10

KIDATO CHA PILI KUANZA MITIHANI NOVEMBA 10

7 months ago
‘UONGOZI SIYO HOTUBA ZENYE KUKONGA NYOYO BALI MATOKEO’

‘UONGOZI SIYO HOTUBA ZENYE KUKONGA NYOYO BALI MATOKEO’

5 months ago

Popular News

  • MWANZA KINARA USIMAMIZI MAAFA

    MWANZA KINARA USIMAMIZI MAAFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WFP KUENDELEZA USHIRIKIANO NA TANZANIA USIMAMIZI WA MAAFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • HESHIMA KUBWA KWA TANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU: MAMBO MAZURI YANAKUJA, AIPA TANO SERENGETI BOYS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERENGETI BOYS HESHIMA KILA KONA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?