• ePaper
Tuesday, April 21, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

SAFARI KUMALIZA CHANGAMOTO UMEME IRINGA, DODOMA YAIVA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 18, 2026
in Habari, Kitaifa
0
SAFARI KUMALIZA CHANGAMOTO UMEME IRINGA, DODOMA YAIVA
0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na FRED ALFRED, Dodoma 

‎SERIKALI imezindua kituo cha kupoza umeme Mtera, chenye thamani ya sh. bilioni 9.7, kitakacho hudumia Mkoa wa Iringa na wilaya mbili mkoani Dodoma, ambazo zilikabiliwa na changamoto ya kukatika kwa umeme.

‎‎Akizungumza katika uzinduzi wa kituo hicho, Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi alisema kuanza kazi kwa kituo hicho kutasaidia hali ya umeme kutengamaa katika mikoa ya Iringa na Wilaya za Kongwa na Mpwapwa, ambazo zilikabiliwa na changamoto ya kukatika kwa umeme mara kwa mara.

‎‎Alisema hiyo ilitokana na umbali mrefu wa kusambaza umeme katika maeneo hayo, kwani uliozalishwa Mtera ulisafirishwa hadi kituo cha kupozea umeme cha Zuzu, ambacho ni umbali wa kilometa 150 hali iliyosababisha kukatika au kukosa nguvu unapowafikia wananchi.

‎‎”Lakini sasa kuzinduliwa kwa kituo hiki kunamaanisha kuwa umeme utazalishwa na kupozwa hapa hapa, hivyo wananchi wa maeneo ya Iringa na Wilaya za Kongwa na Mpwapwa wataondokana na tatizo la kukatika kwa umeme, ambalo lilikwamisha viwanda vikubwa kufunguliwa kwenye wilaya hizo,” alisema Ndejembi.

‎‎Aliongeza kuwa :”Kuzinduliwa kwa kituo hicho ni juhudi za serikali kuhakikisha wananchi wanafikiwa na maendeleo ya kweli, kwa kupitia nishati ya umeme ikiwemo uwekezaji wa viwanda vikubwa na vidogo ambavyo vinahitaji umeme wa uhakika.”

‎Kwa mujibu wa Ndejembi, hadi sasa  vijiji vyote nchini vimefikiwa na hivi karibuni watasaini mkataba wa kupeleka umeme katika vitongoji 9,009, katika kuhakikisha vijiji na vitongoji vyote vinafikiwa na nishati hiyo.

‎‎MRAMBA

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Felchesmi Mramba, alisema Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imefanya kazi kubwa ya kusambaza umeme vijijini.

‎‎Alisema lengo la kuimarisha huduma za umeme nchini ni kuhakikisha inakuwa ya uhakika, siyo ya kukatika ili wananchi wafanye shughuli zao za maendeleo bila bughudha

‎REA 

‎Awali, Mkurugenzi Mkuu wa REA, Hassan Saidy, alisema umeme unaopozwa katika  kituo hicho ulishaanza kufanya kazi, kwa Mkoa wa Iringa kuhudumiwa na megawati tatu huku Mkoa wa Dodoma ukihudumiwa kwa megawati sita.

‎‎Alisema hali hiyo imepunguza muda wa wananchi kukosa umeme kutoka saa 18 kwa mwezi hadi kufikia dakika 40 kwa mwezi, hali inayowafanya wananchi kufanya shughuli zao za maendeleo kwa wakati.

‎RC DODOMA

‎Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule alisema mkoa huo una ziada ya umeme kwani unaozalishwa ni megawati 200, huku matumizi ya mkoa yakiwa megawati 86 na hivyo, kuwa na ziada ambayo haitumiki.

Previous Post

TANZANIA YAINGIA 10 BORA KUVUTIA UWEKEZAJI AFRIKA

Next Post

MIGIRO KATIBU MKUU WA  KWANZA MWANAMKE NA MIKAKATI YA KUIMARISHA MASHINA KATIKA MITAA

Next Post
MIGIRO KATIBU MKUU WA  KWANZA MWANAMKE NA MIKAKATI YA KUIMARISHA MASHINA KATIKA MITAA

MIGIRO KATIBU MKUU WA  KWANZA MWANAMKE NA MIKAKATI YA KUIMARISHA MASHINA KATIKA MITAA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. MWINYI : YAJAYO YANAFURAHISHA KASKAZINI UNGUJA

DK. MWINYI : YAJAYO YANAFURAHISHA KASKAZINI UNGUJA

7 months ago
SIMBA YAKIMBILIA MAFICHONI

SIMBA YAKIMBILIA MAFICHONI

2 months ago

Popular News

  • MAAJABU YA DP WORLD SIKU 730 BANDARINI DAR

    MAAJABU YA DP WORLD SIKU 730 BANDARINI DAR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MUDATHIR KUIKOSA SIMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ‘MISS WORLD’ KUIPAISHA TANZANIA DUNIANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • BIL. 195.66/- KUJENGA BONDE MTO MSIMBAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ULEGA AJIBU MAPIGO KUHUSU MTANDAO WA BARABARA NCHINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?