Na AMINA KASHEBA
BAADA ya kutoka sare michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, kikosi cha Simba kimeingia kambini jana kujiandaa na mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya KMC.
Simba itashuka dimbani kesho kupambana na KMC katika mchezo wa ligi utaofanyika saa 1:00 usiku jijini Dar es Salaam.
Akizungumza maandalizi ya mchezo huo, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally amesema kikosi kiliwasili nchini jana alfajiri na kuingia kambini moja kwa moja kujiandaa na mechi hiyo.
“Wachezaji wa Simba wamerudi jana alfajiri wameingia kambini na kuanza mazoezi kwa ajili ya mchezo muhimu na KMC, natoa wito kwa wanachama kuja kwa wingi kuja kuishangilia timu kwa mabadiliko makubwa waliyoyafanya.
“Rai yangu kwa wanachama kuja uwanjani katika mechi yetu na KMC kuja kuipongeza wachezaji kwa mabadiliko makubwa yaliyofanyika hivi pamoja na kushinda kutinga robo fainali Ligi ya Mabingwa Afrika, ” alisema Ally. Meneja huyo aliongeza kuwa wanachama wa Simba wanapaswa kuisapoti timu hiyo ifanye vizuri




