Na MWANDISHI WETU
WASHINDI wa Kampeni ya ‘Chanja Kijanja, Dili Ndio Hili’ wamepatikana na kukabidhiwa zawadi zao za fedha taslim.
Akizungumza katika hafla ya kukabidhi zawadi kwa washindi jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim, Stanley Kafu, alisema kampeni hiyo imekuwa njia ya kuonesha kuthamini wateja wa benki hiyo na kuimarisha uelewa wa faida za malipo ya kidijitali.
Amesisitiza kuwa matumizi ya kadi si tu rahisi na salama, bali pia yanaweza kuwa na manufaa kwa mteja.
Naye Mkuu wa Kitengo cha Mifumo Mbadala na Mabadiliko ya Kidijitali wa benki hiyo, Silas Matoi, alieleza kuwa mwitikio wa wateja umeonesha mabadiliko chanya katika namna wanavyoipokea teknolojia ya fedha.
Amebainisha kuwa ongezeko la matumizi ya kadi ni ishara ya safari inayoendelea kuelekea uchumi usiotegemea fedha taslimu.
Kwa upande wake, mshindi wa sh. milioni 15, Asif K. Dhalla alisema ushindi huo umempa furaha na kwamba atazipangilia feaha hizo kufanya maendeleo.
”Nimefurahi kuwa mmoja wa washindi na ninaamini fedha hizi zitanisaidia katika kufanya maendeleo mbalimbali,” amesema.
Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Neema Tatock, amethibitisha kuwa droo zote ziliendeshwa kwa uwazi na haki na kutoa uhakika kwa washiriki wote.




