Na SELINA MATHEW
KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Kenani Kihongosi, amewasihi Watanzania, hususan vijana kutokubali kutumika kubeba ajenda za watu wasiofahamu malengo yao.
Amewasisitiza kukiamini Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwa kuwa ni Chama pekee kinachohubiri amani, akisisitiza kulinda utulivu huo, maendeleo yazidi kuja katika Mkoa wa Shinyanga.
Kihongosi alitoa kauli hiyo, alipohutubia wananchi wa Kata ya Isaka, Jimbo la Msalala, baada ya kuwasili kwa ziara ya kukagua miradi ya maendeleo, kusikiliza changamoto za wananchi na kuimarisha Chama.
Kwa mujibu wa Kihongosi, vijana wanapaswa kuwa makini na kulinda mustakabali wa taifa, badala ya kushawishika kujiingiza katika vitendo vitakavyovuruga amani.
“Msidanganywe mkaleta vurugu ndani ya maeneo yenu kwa sababu wanaofanya hivyo hawatoki hapa nchini, lindeni amani na utulivu mlionao,”alisema.
Kihongosi alisisitiza kuwa, amani ya Tanzania ni mtaji mkubwa unaowezesha wananchi kufanya shughuli zao za kiuchumi kwa utulivu na mafanikio.
Alisema hakuna maendeleo yatakayoipatikana bila kuwepo kwa amani, umoja na mshikamano miongoni mwa wananchi.
“Tunashuhudia baadhi ya mataifa yakikumbwa na machafuko makubwa yanayosababisha vifo vya watoto, wanawake na wazee kwa sababu ya kukosekana kwa utulivu,” alisema.
Kihongosi alisema Tanzania imejaliwa amani na umoja, hivyo ni wajibu wa kila Mtanzania kuhakikisha tunu hiyo inalindwa kwa gharama yoyote.
Alisema vijana wanapaswa kutambua kuwa wao ni nguvu kazi ya taifa na msingi wa maendeleo endelevu, hivyo wasikubali kupotoshwa.
Katibu huyo aliwataka waendelee kushiriki katika shughuli halali za kiuchumi na kijamii zitakazochochea ustawi wa taifa badala ya kushiriki katika vitendo vya migawanyiko.
Aliwasisitiza kukiamini Chama kwa kuwa ni Chama pekee kinachohubiri aman, hivyo aliwasisitiza kulinda utulivu huo , maendeleo yazidi kuja katika mkoa huo.
“Msidanganywe mkaleta vurugu ndani ya maeneo yenu kwa sababu aanaofanya hivyo hawatoki hapa nchini, lindeni amani na utulivu mlionao,”alisema.
Kihongosi alisema amani ya nchi ikichafuka watakaopata tabu ni wanawake na watoto, aliwasihi Watanzania kutambua kuwa, amani ni maisha na uhai.
“Amani ikitoweka hakuna umeme, barabara wala maendeleo yoyote, asije mtu yeyote wa kabila lolote akakusihi uharibu amani iliyopo, kuna watu wapo radhi nchi iharibike kwa maslahi yao binafsi.
“Wanaofanya hivyo wanaishi ulaya wakishaharibu wanaondoka, wanapenda kuwatumia vijana kwamba komaa, pambana, Mwenyezi Mungu alikupa mwili kwa baraka, utunze utumie kutafuta fedha,”alisema.
Kihongosi aliwasihi kutambua kuwa maisha yao ni mali yao, hivyo asitokee mtu akawadhihaki kwa kutaka kuandamana na kwamba kama wanataka kufanya hivyo ni vyema wakaandamana kuleta maendeleo nyumbeni siyo kuchoma miundombinu ya serikali.
“Wanaowashawishi mchome shule, hospitali wanapata huduma nje ya nchi, tulinde miundombinu yetu ya serikali, usikubali kupambana ndani ya ardhi uliyozaliwa,”alisema.
Aliwasihi Watanzania kuendelea kumwombea Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, aendelee kuijenga nchi kupitia utekelezaji miradi.
Kihongosi alisema katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wake miradi mingine imetekelezwa kupitia ujenzi wa shule, reli na hospitali zimejengwa.
“Dk. Samia mapenzi yake kwa nchi ni makubwa, kaa jiulize kosa la Rais ni nini… utakuta ni chuki za kuambukizwa ziliopo miongoni mwa watu dhidi yake, jambo la kujiuliza hata ukimuuliza mtu anasema unajua..sunajua…usicheze ngoma usiyoijua.




