• ePaper
Wednesday, April 29, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

WATUMISHI NIRC WASHEREHEKEA MWAKA 2026, WAASWA KUIMARISHA MSHIKAMANO, UWAJIBIKAJI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 25, 2026
in Habari, Kitaifa
0
WATUMISHI NIRC WASHEREHEKEA MWAKA 2026, WAASWA KUIMARISHA MSHIKAMANO, UWAJIBIKAJI
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imefanya tafrija ya mwaka wa fedha 2025/26 huku ikitoa wito kwa watumishi kuongeza umoja, mshikamano na uwajibikaji mahala pa kazi.

Hafla hiyo imefanyika katika jengo jipya ofisi ya Tume makao makuu lililopo Njedengwa mkoani Dodoma, lengo ni kutambua mchango wa watumishi wanaojitoa zaidi katika utendaji kazi pamoja na kuimarisha mahusiano miongoni mwa wafanyakazi wa taasisi hiyo.Tafrija hiyo imehudhriwa na watumishi wa NIRC kutoka nchi nzima.

Akizungumza katika tafrija hiyo iliyokutanisha watumishi zaidi ya 300 ambapo

178 kutoka mikoani na wengine 122 kutoka Makao Makuu na watoa huduma zaidi ya 30, Mkurugenzi Mkuu Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw. Raymond Mndolwa amewapongeza watumishi kwa utendaji kazi, wenye lengo la kuleta matokeo katika sekta ya Kilimo.

Mapema kabla ya hafla hiyo watumishi hao walishiriki vikao vya Baraza la Wafanyakazi na semina za kitaaluma zilizofanyika siku mbili kabla

Amesema kuwa vikao hivyo vimekuwa nyenzo muhimu ya kukumbushana wajibu wa kisheria na kimaadili ambao watumishi hao wana wajibu kwa wananchi wa Tanzania kusimamia sekta ya Umwagiliaji nchini.

Mndolwa ametoa shukrani za dhati kwa Bodi ya Uongozi Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kwa usimamizi thabiti, pamoja na Menejimenti na Wahandisi wa Umwagiliaji wa Mikoa (RIE) na watumishi wote kwa ushirikiano wao uliotukuka.

Aidha, Mndolwa amesisitiza kuwa mafanikio ya taasisi yanategemea uimara wa familia ya watumishi hao ambapo amewaasa kuendelea kufanya kazi kwa bidii na uaminifu ili kufikia malengo ya Serikali kuongeza eneo la Umwagiliaji.

Previous Post

CCM YAFUNGUKA RIPOTI TUME YA JAJI CHANDE

Next Post

TUUNGANE KUJENGA NCHI – BALOZI NYALANDU

Next Post
TUUNGANE KUJENGA NCHI – BALOZI NYALANDU

TUUNGANE KUJENGA NCHI - BALOZI NYALANDU

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

NITASHIRIKIANA NAYE KULETA MAENDELEO

NITASHIRIKIANA NAYE KULETA MAENDELEO

7 months ago
MSIGWA AELEZA MANUFAA UBORESHAJI RELI YA TAZARA

MSIGWA AELEZA MANUFAA UBORESHAJI RELI YA TAZARA

4 months ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?