• ePaper
Thursday, May 21, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

 DABI YA TANO YANUKIA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
May 19, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
 DABI YA TANO YANUKIA
0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na AMINA KASHEBA

BAADA ya kutinga hatua ya nusu fainali ya Kombe la Shirikisho FA, timu za Yanga na Simba zinaweza kukutana katika mchezo wa fainali.

Timu hizo, zimepangwa kucheza hatua ya nusu fainali  katika michezo miwili tofauti ambapo Yanga itachuana na Azam FC.

Pambano hilo, limepangwa kufanyika Juni 21, mwaka huu katika dimba la CCM Kirumba jijini Mwanza.

Huku Simba yenyewe imepangwa kucheza Juni 20, mwaka huu na Coastal Union katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Kama timu hizo zitatinga fainali, ndani ya msimu huu Yanga na Simba zitakuwa zinapambana mara ya tano.

Awali zilipambana  Septemba 16, mwaka jana ambapo

Yanga iliichapa Simba 1-0 katika mchezo wa Ngao ya Jamii, bao la ushindi lilipachikwa wavuni na Pacome Zouzoua.

Timu hizo, zilipambana tena katika Uwanja wa New Amaan Complex, Machi Mosi, mwaka huu katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara ambapo zilitoka suluhu.

Timu hizo zilipambana tena Aprili 29, mwaka huu katika mchezo wa Kombe la Muungano ambapo Simba ilishinda 1-0 katika Uwanja wa New Amaan Complex visiwani Zanzibar.

Bao pekee la Simba liliwekwa kimiani kwa mkwaju wa penalti katika dakika ya 120 na mchezaji wake Selemani Mwalimu kufuatia Clatous Chama kufanyiwa madhambi na Edmund John katika eneo la hatari.

Mchezo huo ulilazimika kwenda dakika 120 baada ya kumalizika kwa suluhu muda wa kawaida ndani ya dakika 90.

Mei 3, mwaka huu, timu hizo zilipambana katika mchezo wa ligi hiyo, zilitoka sare ya 2-2.

Hata hivyo, mashabiki wengi wa timu hizo wanasubiri kuona kama timu hizo zitakutana tena.

Tayari taarifa iliyotolewa jana na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imeeleza kuwa maandalizi ya michezo hiyo yanaendelea vizuri.

Katika michuano hiyo, Yanga ilitinga nusu fainali baada ya kuichapa JKT Tanzania kwa mabao 2-0.

Azam imeingia hatua hiyo  baada ya  kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mashujaa FC katika Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma.

Kikosi cha Simba kilisonga mbele baada ya kuigagadua TRA mabao 4-0 wakati Coastal Union ilishinda kwa mikwaju ya penati 4-2 dhidi ya Singida Black Stars.

Previous Post

RAIS DK. SAMIA ATOA AGIZO  KOMBE LA DUNIA 2026

Next Post

KOCHA SIMBA KICHEKO  

Next Post
KOCHA SIMBA KICHEKO  

KOCHA SIMBA KICHEKO  

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

RAIS DK. SAMIA AONYA WAVURUGA AMANI

RAIS DK. SAMIA AONYA WAVURUGA AMANI

4 months ago
CCM INASHINDWAJE KIGOMA – DK. SAMIA

CCM INASHINDWAJE KIGOMA – DK. SAMIA

8 months ago

Popular News

  • KUDUMISHA SERA YA CHINA MOJA NA KUIMARISHA URAFIKI KATI YA CHINA NA TANZANIA

    KUDUMISHA SERA YA CHINA MOJA NA KUIMARISHA URAFIKI KATI YA CHINA NA TANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, COASTAL HAPATOSHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RIO USIPIME KABISA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA AWAPA TABASAMU WAPIGANAJI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KOCHA SIMBA KICHEKO  

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?