• ePaper
Sunday, July 26, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

WANAWAKE WACHANGAMKIA UPASUAJI MAKALIO MLOGANZILA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
July 17, 2026
in Habari, Kitaifa
0
WANAWAKE WACHANGAMKIA UPASUAJI MAKALIO MLOGANZILA
0
SHARES
9
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

HOSPITALI ya Taifa ya Muhimbili-Mloganzila, hapotoshi kutokana na wanawake wengi kuchangamkia kwa kasi kubwa upasuaji wa kuongeza makalio.

Unaambiwa hivi; upasuaji wa makalio hivi sasa umepiku upasuaji wa matiti.

Pia, imesema matokeo ya upasuaji wa matiti huonekana mara moja huku makalio huchukua baada ya siku 21 kupona.

Akizungumza na Uhuru leo, Daktari Bingwa wa Upasuaji na Mkuu wa Idara ya Upasuaji Mloganzila, Dk. Erick Muhumba, amesema huduma ya kuongeza makalio ndiyo inaonekana kuhitajika zaidi tofauti na matiti.

Amesema wagonjwa wengi waliopata huduma hizo wanaonyesha kuridhishwa na matokeo kutokana na huduma nzuri wanazotoa.

“Kwa takwimu zetu tunavyotoa huduma ya upasuaji wa kuongeza makalio inaongoza zaidi kushinda ya matiti, naona ni kutokana na baadhi ya watu wanapenda kubadilisha maumbo yao hata watu maarufu hunufaika na huduma zetu.

“Katika kazi zetu hizi za upasuaji wa kuongeza makalio tuliwahi kupata changamoto moja ambapo mgonjwa alipata maambukizi katika kidonda, lakini baada ya kupatiwa matibabu alirejea katika hali yake ya kawaida na kupona vizuri, tunamshukuru Mwenyezi Mungu tunaendelea kutoa huduma bora kwa wananchi,” amesema.

Akizungumzia maumivu yanayoweza kutokea baada ya upasuaji, amesema hayana tofauti na yale yanayotokea katika upasuaji mwingine wowote, huku akisisitiza wagonjwa wote hufuata taratibu za kawaida za maandalizi kabla ya kufanyiwa upasuaji.

Aidha, amesema kwa wale wanaotumia dawa za kujichubua ngozi, virutubisho mbalimbali au wanaovuta sigara hushauriwa kusitisha matumizi hayo kwa muda kupunguza hatari ya kupata madhara wakati na baada ya upasuaji.

“Kwa kuwa huu sio upasuaji wa dharura, tunampa mgonjwa muda wa kujiandaa, tunashauri aache matumizi ya dawa za kujichubua, kuacha kuvuta sigara kwa kipindi kinachoshauriwa kabla ya kufanyiwa upasuaji,” amesema.

Akifafanua kuhusu matokeo ya upasuaji, amesema kwa upande wa matiti, mabadiliko huanza kuonekana mara moja baada ya upasuaji, huku kwa upande makalio umbo kamili huanza kuonekana baada ya wiki tatu siku 21.

Amesema kidonda cha upasuaji wa makalio huanza kupona ndani ya wiki moja, huku mgonjwa akiendelea kutumia dawa za antibiotiki kwa siku tano hadi saba kulingana na ushauri wa daktari.

Dk. Muhumba, amesema katika upasuaji wa kuongeza makalio, madaktari huchukua mafuta chini ya ngozi ya tumbo, kisha kuyachakata na kuyahamishia katika makalio kupata umbo linalohitajika.

Amesema baada ya upasuaji mgonjwa hatakiwi kukalia moja kwa moja makalio kwa muda wa siku 21, bali anapaswa kutumia mto maalumu au taulo kukalia mapajani kulinda matokeo ya upasuaji.

Aidha, amesisitiza kuwa kidonda cha upasuaji hakipaswi kuloweshwa na maji hadi pale kitakapopona kwa mujibu wa maelekezo ya daktari.

Kuhusu uwezo wa kupata watoto, Dk. Muhumba alisema upasuaji wa kuongeza makalio au matiti haumzuii mwanamke kupata ujauzito wala kunyonyesha, kwani huduma hizo hazina athari kwa uwezo wa uzazi.

Amewashauri wanawake ambao hawaridhiki na maumbo yao na wanahitaji kuyabadilisha kufika Hospitali ya Mloganzila kwa ushauri na huduma kutoka kwa madaktari bingwa kuhakikisha usalama na matokeo bora.

Previous Post

NSSF YAWAPA NAFUU WAAJIRI, YAWATAKA KUCHANGAMKIA MSAMAHA WA TOZO

Next Post

DAKTARI AANIKA UNDANI UPANDIKIZAJI WA UUME

Next Post
DAKTARI AANIKA UNDANI UPANDIKIZAJI WA UUME

DAKTARI AANIKA UNDANI UPANDIKIZAJI WA UUME

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

3 months ago
RAIS DK. SAMIA, DK. NCHIMBI WAIMWAGIA SIFA STARS

RAIS DK. SAMIA, DK. NCHIMBI WAIMWAGIA SIFA STARS

7 months ago

Popular News

  • KATIBA MSINGI WA HAKI – DK. NCHIMBI

    KATIBA MSINGI WA HAKI – DK. NCHIMBI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MABASI YA UMEME REKODI ZANZIBAR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KOCHA AIPA JEURI YANGA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWALIMU, GUEYE WAPO SIMBA SANA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI ASHTUKIA ‘USANII’ WA WACHIMBAJI MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?