• ePaper
Thursday, June 25, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

DIAMOND, HARMONIZE, MISO MISONDO WATIKISA UZINDUZI KAMPENI CCM

admin by admin
August 29, 2025
in Burudani
0
DIAMOND, HARMONIZE, MISO MISONDO WATIKISA UZINDUZI KAMPENI CCM
0
SHARES
29
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na AMINA KASHEBA

WASANII wa muziki bongo, Nasib Abdul ‘Diamond’, Rajab Kahali ‘Harmonise’ na kundi la singeli la Miso Misondo, jana walifunika kwa kutoa burudani ya aina yake katika uzinduzi wa kampeni ya uchaguzi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), uliofanyika Uwanja wa Tanganyika Packers, Kawe, jijini Dar es Salaam.

Wasanii hao walitoa burudani ya aina yake na kukonga nyoyo za maelfu ya watu waliojitokeza katika uzinduzi huo ambapo walionekana kuimba nao nyimbo mbalimbali.

Mastaa hao wa muziki, waliporomosha burudani ya aina yake kwa kuimba nyimbo tofauti zikiwemo zitakazotumika katika kipindi cha kampeni na kuwafanya waliohudhuria kucheza nao sambamba muda wote.

Miso Misondo walionyesha umahiri mkubwa wa kulitawala jukwaa kutokana na staili yao ya kipekee ya kucheza na makoti kitu kilichoibua shangwe uwanja mzima.

Miso Misondo waliibua shangwe baada ya kupanda jukwaani kutoa burudani kwa kucheza staili mbalimbali za muziki wa aina ya singeli na kuwavutia mashabiki wao.

Kutokana na staili hiyo uwanjani hapo watu ambao walijitokeza katika ufunguzi huo walionekana kuwafurahia zaidi wasanii kwa burudani ya aina yake.

Baada ya kushuka jukwaani, kiongozi wa kundi hilo anayejulikana kwa jina la Miso, alisieitiza kwamba amefarijika kuona umati wa watu ukiwashangilia kwani wanaonekana wanakubalika na kwa kiasi kikubwa.

Alisema walipata nafasi ya kufanya onyesho hilo katika uzinduzi wa kampeni, hivyo wataendelea kumuunga mkono Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kusambaza ujumbe kwa jamii ili wamchague katika uchaguzi utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu.

“Kwetu ni furaha kuona watu wengi kiasi hichi wanafurahia burudani yetu tuliyoitoa, hivyo tutaendelea kueneza ujumbe kwa jamii kuhakikisha tunamchagua Rais Dk. Samia kwa kishindo,” alisema.

Mbali na wasanii hao, wengine waliotoa burudani ni Mbwana Kilungi ‘Mbosso’, Rashid Makwiro ‘Chid Benzi’, Barobaro, bendi ya T.O. T, Mrisho Mpoto, Zanzibar One, Kidene Fighter na Raymond Mwakyusa ‘Ravyann’.

Previous Post

WASIRA : DK. SAMIA ANASTAHILI ‘MITANO TENA’

Next Post

DK. SAMIA KUUNGURUMA MOROGORO

Next Post
DK. SAMIA KUUNGURUMA MOROGORO

DK. SAMIA KUUNGURUMA MOROGORO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SADIO MANE, SHUJAA WA SENEGAL AFCON 2025

SADIO MANE, SHUJAA WA SENEGAL AFCON 2025

5 months ago
UPATIKANAJI MAJI DAR SASA KWA USAWA

UPATIKANAJI MAJI DAR SASA KWA USAWA

6 months ago

Popular News

  • SERIKALI YAZITAKA TAASISI ZOTE KUJIANDAA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL-NINO

    SERIKALI YAZITAKA TAASISI ZOTE KUJIANDAA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL-NINO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SAMAMBA AWAFUNDA WAKAGUZI MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RUNGU ZITO KUWASHUKIA WAWEKEZAJI ‘JANJAJANJA’

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI UBINGWA LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, AZAM FC HAIJAISHA HADI IISHE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?