• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Uncategorized

GAVU ATAJA SIFA ZA NAFASI URAIS, UBUNGE, UDIWANI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
August 30, 2025
in Uncategorized
0
Katibu wa Idara ya Organaizesheni ya CCM, Issa Haji Gavu
0
SHARES
1
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

 Na NJUMAI NGOTA,

Mwanza

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesema nafasi za urais, ubunge na udiwani zinahitaji watu wenye utayari, uwezo, dhamira, malengo na kusudio la kulisukuma mbele gurudumu la maendeleo.

Kauli hiyo imetolewa mkoani hapa na Katibu wa Idara ya Organaizesheni ya CCM, Issa Haji Gavu, alipozungumza katika mkutano wa hadhara wa kampeni za CCM zilizofanyika viwanja vya Furahisha, wilayani Nyamanga.

Mgombea Mwenza wa Urais kupitia CCM, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, alizindua kampeni za uchaguzi mkoani humo.

Gavu amesema Chama kinaheshimu nafasi ya kiongozi ya kukiwakilisha.

“Nafasi ya kiongozi wa kuiwakilisha jamii yetu, tunaamini nafasi za uongozi iwe udiwani, ubunge na urais ni nafasi ambazo zinahitaji watu wenye utayari, uwezo, dhamira, malengo na wenye kusudio la kusukuma mbele gurudumu la maendeleo,”amesema.

Amesema yapo mambo ambayo yanabahatishwa, kwa jambo la uongozi wa taifa, majimbo na kata siyo ya fahari, hivyo wanahitaji viongozi wa kulitoa taifa lilipokuwepo jana, leo na kesho.

Gavu alisema hakuna kiongozi wa chama kingine chochote mwenye kujua dhamira hiyo, zaidi ya viongozi wanaotokana na CCM.

Amewaomba wananchi vyama vingine vitakapokuja wavipe nafasi ya kuvisikiliza, wapime na kutazama dhamira zao.

“CCM imejiandaa kwa sera, Ilani na kwa kutambua yapo mafanikio tuliyofanikiwa, zipo changamoto tunazokabiliana nazo na ipo mipango ya kuachana na changamoto hizo.

“Tutakapokuja kwenu, hatuji kulalamika, tutakuja kuwaeleza tumetoka wapi, tupo wapi na tunakwenda wapi, hiyo ni dhamira ya Chama,”amesema.

Previous Post

DK. SAMIA, BALOZI NCHIMBI WAAHIDIWA KURA ZA KISHINDO

Next Post

YANGA, SIMBA MECHI YA KISASI NA HESHIMA

Next Post
Wachezaji wa SIMBA na YANGA

YANGA, SIMBA MECHI YA KISASI NA HESHIMA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

BALOZI NCHIMBI AMSIFU DK. SAMIA KUIMARISHA UHUSIANO

BALOZI NCHIMBI AMSIFU DK. SAMIA KUIMARISHA UHUSIANO

1 month ago
DK. MWINYI ATANGAZA NEEMA WAZEE ZANZIBAR

DK. MWINYI ATANGAZA NEEMA WAZEE ZANZIBAR

1 month ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.