• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

SERIKALI YA DK. SAMIA KUIMARISHA UPATIKANAJI UMEME SONGWE

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 4, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
SERIKALI YA DK. SAMIA KUIMARISHA UPATIKANAJI UMEME SONGWE
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MUSSA YUSUPH,

Songwe

KATIKA kuboresha upatikanaji umeme mkoani Songwe, mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ameahidi kujenga njia ya umeme yenye msongo wa kilovoti 730 itakayokwenda kuimarisha upatikanaji nishati hiyo.

Akihutubia maelfu ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Tunduma mkoani Songwe, Dk. Samia amesema umeme huo pia utauzwa nchini Zambia.

“Serikali imejipanga kutekeleza mradi wa umeme kutoka Iringa – Njombe hadi Tunduma yenye msongo wa kilovoti 730, kati ya hizo kilovoti 400 zitatumika Tunduma na Rukwa huku kilovoti 330 zitakwenda kuuzwa nchini Zambia.

Ameeleza: “Tumeshakamilisha mazungumzo, tumeanza mchakato kujenga njia hii ili umeme ufike kwa uhakika. Hii inakwenda sambamba na uhamasishaji matumizi ya nishati safi kwa sababu umeme pamoja na gesi ni nishati safi,” alieleza.

Dk. Samia ameongeza: “Nataka kuwathibitishia na kuwaahidi, nitaendelea kufanya makubwa katika sekta ya elimu, afya, maji na umeme. Tunakwenda kutoa huduma kwa wananchi, tutaendelea kuongeza shule, elimu bila ada, mikopo kwa wanafunzi wa vyuo na VETA, kujenga vyuo vya VETA kuwawezesha vijana wapate ujuzi na kujiajiri.

Akizungumzia miradi ya maji, amesema serikali yake itahakikisha kila Mtanzania anapata maji safi na salama kama ilivyoelekezwa katika ilani ya uchaguzi.

“Tutaendelea kujenga vituo vya afya na zahanati, tunakwenda kumaliza miradi ya maji lengo kuhakikisha kila Mtanzania apate maji safi na salama kwa asilimia 85 vijijini na asilimia 95 mijini.

Baadhi ya maeneo tumefikia lakini baadhi ya maeneo miradi inaendelea. Umeme tumemaliza vijiji vyote, tupo nusu ya vitongoji na tunakwenda kuunga umeme kila mwananchi afaidike,” amebainisha.

Previous Post

DK. SAMIA NI KIONGOZI MWENYE NGUVU KUIVUSHA TANZANIA – CHONGOLO

Next Post

DK. SAMIA, AHIMIZA WAKULIMA WAJISAJILI KATIKA MFUMO WA RUZUKU YA MBEGU, PEMBEJEO

Next Post
DK. SAMIA, AHIMIZA WAKULIMA WAJISAJILI KATIKA MFUMO WA RUZUKU YA MBEGU, PEMBEJEO

DK. SAMIA, AHIMIZA WAKULIMA WAJISAJILI KATIKA MFUMO WA RUZUKU YA MBEGU, PEMBEJEO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. MWINYI AFUNGUKA MALENGO SERA YA NISHATI

DK. MWINYI AFUNGUKA MALENGO SERA YA NISHATI

1 month ago
WAKAZI WA RUKWA WAAHIDI ‘MITANO TENA’ KWA DK. SAMIA

WAKAZI WA RUKWA WAAHIDI ‘MITANO TENA’ KWA DK. SAMIA

1 month ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.