• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

NCHIMBI AFAFANUA MAFANIKIO SEKTA ZA KILIMO, UFUGAJI, UTALII

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 13, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
NCHIMBI AFAFANUA MAFANIKIO SEKTA ZA KILIMO, UFUGAJI, UTALII

MGOMBEA Mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi

0
SHARES
1
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

NJUMAI NGOTA na 

LILIAN JOEL, Longido

MGOMBEA Mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, amesema mafanikio makubwa yaliyopatikana chini ya uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, katika sekta za kilimo, ufugaji na utalii ni ushahidi wa kutosha wa dhamira ya dhati ya serikali, kuwaletea wananchi maendeleo.

Dk. Nchimbi, alisema hayo, alipohutubia mamia ya wananchi wa Wilaya ya Longido mkoani Arusha, katika mkutano wa kampeni kuelekea Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu.

Alisema pamoja na changamoto za janga la Uviko-19 lililopunguza utalii kwa zaidi ya asilimia 80 kutokana na jitihada za Dk. Samia, ziliwezesha sekta hiyo kuimarika, hivi sasa Tanzania inapokea zaidi ya watalii milioni 4.9 kwa mwaka.

“Rais Samia, hakukata tamaa. Aliamua kupambana kwa nguvu kubwa kuitangaza Tanzania kimataifa kupitia filamu ya ‘The Royal Tour,’ leo matokeo tunayashuhudia.

“Watalii wameongezeka, biashara zimeongezeka, mapato ya taifa yameongezeka,” alisema.

UFUGAJI

Akizungumzia mafanikio yaliyopatikana miaka minne iliyopita katika sekta ya ufugaji, Dk. Nchimbi, alisema serikali imejenga majosho mapya 16 ya kuogeshea mifugo na zaidi ya lita 874 za dawa, zimetolewa kwa wafugaji wa Longido.

Kwa mujibu wa Dk. Nchimbi, serikali imetoa dozi 550,880 za chanjo kwa mifugo, kuzuia magonjwa na kuongeza tija katika uzalishaji.

MAJI

Kuhusu miundombinu ya maji, alieleza miradi tisa ya maji, imekamilika kwa gharama ya zaidi ya sh. bilioni tisa, huku miradi mingine 11 ikiendelea kutekelezwa.

ELIMU

Alisema kuna ongezeko la shule za msingi kutoka 49 hadi 59, sekondari 10 hadi 16 katika kipindi cha miaka mitano.

Hata hivyo, aliwahimiza wakazi wa wilaya hiyo, kuwapeleka watoto shule.

“Wamasai lazima wasome. Tunahitaji Wamasai wasomi kama ilivyokuwa enzi za Sokoine (Hayati Edward). Elimu ndiyo msingi wa maendeleo ya kweli,” alisema.

AFYA

Alisema katika kipindi cha miaka hiyo, zahanati zimeongezeka kutoka 23 hadi 30, vituo vya afya kutoka vinne hadi saba, hali inayoboresha upatikanaji huduma za afya kwa wakazi wa Longido.

 UMEME

Dk. Nchimbi, alisema kati ya vitongoji 112 vya Longido, 34 vimepata nishati hiyo na kazi ya kufikisha katika vitongoji vilivyosalia, inaendelea.

“Tuna imani kubwa na Rais wetu. Ana nia, ana uwezo, ana dhamira ya kweli ya kuifikisha Tanzania katika uchumi wa kati wa juu kupitia maendeleo ya watu,” alisema.

Alisema Dk. Samia, ameendelea kuonesha dhamira ya kweli ya kuwaletea Watanzania maendeleo shirikishi na endelevu huku moja ya maeneo aliyoyapa kipaumbele ni kuboresha mazingira ya wafugaji nchini.

Alieleza kuwa, serikali chini ya Rais Dk. Samia, imejikita kuhakikisha sekta ya mifugo, inapata msukumo mpya kwa kuboresha huduma za afya ya mifugo, maeneo ya malisho na kutatua migogoro ya ardhi kati ya wafugaji na wakulima.

Mbali na sekta ya mifugo, serikali imefanya kazi kubwa katika nyanja nyingine muhimu, ukiwemo uchimbaji madini, nishati ya umeme, afya, elimu, maji safi na salama, miundombinu ya barabara na miradi ambayo imefungua fursa za kiuchumi kwa mamilioni ya Watanzania vijijini na mijini.

Alisema kutokana sifa kubwa zaidi aliyonayo Dk. Samia ni uwezo wake wa kusikiliza matatizo ya wananchi wa kawaida na kuyafanyia kazi kwa vitendo.

“Hatuna Rais mbishi, hatuna Rais muongo. Tunaye Rais msikivu, mnyenyekevu, anayeguswa na shida za wananchi wake.

“Ndiyo maana, makabila yote nchini, kuanzia Kaskazini hadi Kusini, Mashariki hadi Magharibi, watu wanapopata shida, Rais wetu ama huenda mwenyewe, au hutuma wawakilishi wake waaminifu kuwasikiliza wananchi,” alisema.

MIAKA MITANO IJAYO

Balozi Dk. Nchimbi, alisema Chama kama kitapewa ridhaa ya kuongoza nchi kwa miaka mitano ijayo,  kitaendelea kuboresha sekta hizo kwa kiwango kikubwa zaidi.

Pia, alisema katika miaka hiyo, wameahidi kujenga zahanati tano na vituo vya afya vinne, shule za msingi 26, kuongeza madarasa 88, kuimarisha miundombinu ya barabara na kuongeza maofisa mifugo.

Aidha, alisema wataweka mpango wa matumizi bora ya ardhi, utakaohakikisha kila kundi la wafugaji, wakulima na wafanyabiashara, wanapata maeneo maalumu ya shughuli zao.

NAMELOCK SOKOINE
Naye, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi, Namelock Sokoine, alisema Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya uongozi wa Rais Dk. Samia, imeleta mabadiliko makubwa ya kiuchumi katika Jimbo la Longido kwa kuleta umeme wa Gridi ya Taifa katika vijiji vyote.

Alisema Dk. Samia, amewatua ndoo kichwani wanawake wa jimbo hilo, kwa kuleta miradi mikubwa ya maji ambayo imewezesha wanawake kujikwamua kiuchumi kwa kuanzisha miradi mbalimbali ya maendeleo tofauti na awali.

“Ninajua Wilaya ya Longido ni ngome ya CCM, niwaombe sana Oktoba 29, mwaka huu, tujitokeze kwa wingi kwenda kuwachagua viongozi wanaotokana na CCM kwa maendeleo zaidi,” alisema.

DK. KIRUSWA

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Longido, Dk. Steven Kiruswa, alisema wilaya hiyo, imepata miradi mikubwa ya maendeleo, katika sekta ya elimu, wamepata zaidi ya sh. bilioni 4.

“Tunamshukuru Dk. Samia kwa kurejesha ardhi za wafugaji katika jimbo letu, japo kuna changamoto ndogo katika baadhi ya maeneo, hasa mashamba ya NAFCO,”alisema.

FREDY LOWASA

Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Monduli, Fredy Lowassa, alisema Dk. Samia, alipokea nchi katika kipindi kigumu cha janga la Uviko 19, ila aliendeleza miradi mikubwa ya kimkakati iliyoanzishwa na mtangulizi wake, Dk. John Magufuli, ameikamilisha kwa asilimia 100 ndani ya kipindi kifupi cha uongozi wake.

MGOMBEA JIMBO LA NGORONGORO

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Ngorongoro, Yaniki Ndoinyo, alisema Serikali ya Awamu ya Sita, imetekeleza miradi mikubwa ya maendeleo na kwamba, shukrani yao, ni kuhakikisha wanaongoza kwa kura za Dk. Samia.

Previous Post

CCM Z’BAR YAAHIDI KAMPENI ZA KISTAARABU

Next Post

KAMPENI YA DK. SAMIA YAACHA GUMZO TABORA

Next Post
KAMPENI YA DK. SAMIA YAACHA GUMZO TABORA

KAMPENI YA DK. SAMIA YAACHA GUMZO TABORA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WASIRA : TUSAHAU MCHAKATO WA UCHAGUZI, SASA TUUNGANE KUSAKA DOLA

WASIRA : TUSAHAU MCHAKATO WA UCHAGUZI, SASA TUUNGANE KUSAKA DOLA

1 month ago
WAKAZI WA RUKWA WAAHIDI ‘MITANO TENA’ KWA DK. SAMIA

WAKAZI WA RUKWA WAAHIDI ‘MITANO TENA’ KWA DK. SAMIA

1 month ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.